Jumanne, 15 Desemba 2015

IRUHUSU JANA IPITE ILI LEO IJE!



ACHA JANA IPITE

Katika maisha ya kila siku ya mwanadamu kuna jana,leo na kesho na katika mfulullizo huu ndipo pazaliwa mwezi, mwaka na hata karne! Na kila siku inayoenda inakuwa na vionjo vyake zipo siku zitaanza na huzuni na baadae zitaenda katika furaha na zipo siku zitaanza na huzuni kuanzia mchana hadi jioni na siku chache sana kwa mwanadamu ambazo zinahesabika kwa mwanadamu kuwa na furaha kuanzia mwanzo wake na hadi mwisho wake.

Ni jambo halisi sana kwa baadhi ya watu katika maamuzi yao ya leo yalitokana na jana yao…mathalani siku moja nilimsikia polisi akisema kipindi sijawa polisi nikiwa mdogo nili nyanyaswa sana na polisi hivyo niliapa kuwa endapo na mimi nikiwa mkubwa lazima niwe polisi na hatimae akawa sawa na na lile kusudi alilowaza katika moyo wake na sio huyo tu bia hata mtu katika kusoma udaktari au sheria kuna mambo walio yapitia katika jana yao na kunuwia kusoma hiyo fani.
Japo ni kweli ni muhimu usome jambo ambalo liko ndani yako ambalo unalolipenda pamoja na hayo pia kuna ushawishi wa kimazingira ambayo yanaweza kusababisha kuingia katika fani hiyo, pia tukubaliane wako watu wengi wanasoma sasa sio kwasababu wanapenda au hiko moyoni ila inawezekana kutokana ndio nafasi iliyopatikana na hata wengine kuona ndio yenye mshahara mkubwa na wengine uweza kuona kuwa ndio fani rahisi katika kupata kazi na kuanza maisha yake binafsi.

Napia kunawakati unaweza ukupenda kuingia sehemu fulani au fani fulani lakini baada ya kuanza kufaidi matunda yake unaweza kusema hivi kwanini sikuwaza jambo hili kama kipaumbele changu cha kwanza kwani sasa nafaidi matunda yake! Inaweza kuwa vizuri ukaanza kuifurahia au kuwa vibaya hata ukaanza kuchukia wakati mwingine yote ni kutokana na matokeo ya hiyo fani katika kazi unayoifanya.

Acha jana ipite maana yake nini?
Ni kwali siku inaweza ikapita lakini wewe bado unaishi katika jana yako japo unahiita leo kutokana kuzama na kuchomoza kwa jua lakini ukweli wewe binafsi bado unaishi jana japo unaonekana leo, yale yote yalioendelea jana katika maisha yako yamekuwa ndio dira ya maisha yako ya sasa kama katika hali ya maumuvu ndio yamekuwa ndo maisha yako ya kujikataa na kuona ndio maisha Mungu alinichagulia ya mimi kuishi.

Mtu kama huyu anayeishi jana katika leo mtizamo wake haubadiliki kile alichojiaminisha ndicho kinachoendelea hadi leo na anakipenda kwakua amekipa nafasi katika maisha yake na kuwa hivyo ndivyo maisha yake.

Kuna watu wakikumbaka jana basi wanalia tu siku nzima inaweza kuwa ilikuwa nzuri kuliko leo mathalani mtu katika maisha yake ya awali alikuwa na kazi yake nzuri na kuishi maisha ya kifahari sana lakini kutokana kuachishwa kazi na ndipo maisha yako yakawa chini hata usijue lakufanya tena bali kilio chako kikawa ndio maisha yake.

Ni vizuri sana kuanza upya hata ukiona itachukua muda gani katika kutimiza malengo yako! Wako wengi wanajihukumu na kujilaumu sana kutokana na yale yaliyosababisha kuwa hapo tena,

Iruhusu jana ipite ili leo ije!
Hizi ni siku mbili tofauti na kamwe hauwezi ukazifananisha na kamwe haziwezi kuingiliana kama leo ipo basi jana ilishapita na kama jana ipo basi leo bado haijaja ziko hivyo hakuna mbadala wake tena hiko kama ilivyo, ndomana wako watu wengi wanatembea leo lakini ukweli hawaoni fahari ya leo zaidi yakujisikia vibaya kwa jana iliyopita.

Usipokuwa makini unaweza ukakuta unamlaumu Mungu muda wa wote kumbe wewe unaishi jana katika leo…………ukapoteza muda na hata kukata tama!

Ni vizuri kutatambua jambo likisha pita limepita hata kama ulikuwa hauamini lakini sasa inabidi uamini tu haijarishi ulikuwa unampenda kiasi gani? Ulikuwa unamwihitaji kiasi gani? Au alikuwa wa muhimu kiasi gani? Au kazi ilikuwa inakunufaisha kiasi gani? Au nyumba ilikuwa inakusitiri na kujivunia kiasi gani?  Lakini jua limeshapita kinachotakiwa hapo ni maisha yaendelee kwakua kwakua kesho itakuja na pindi itakapo fika hautaita kesho bali utaita leo.

Na kila siku kuna baraka zake na hili uzipate unahita uishi kama siku hiyo ilivyo kama ni  jana basi ishi kama jana na kama ni leo ishi kwa siku hiyo ukifuta yaliyopita yaani jana yako, na sio kwa upande wa ubaya tu watu wengine wanajisahau kwakua waliweza jana kufanya jambo fulani basi wanaamini pia hata kesho wataweza pasipo kujua kesho na jana ni vitu tofauti na kamwe haviwezi kulingana, maandalizi ya jana yanaishia jana na maandalizi ya leo yanaishia leo.

lazima uwe mwepesi katika kusoma mabadiliko ili uweze kuimarika na kuwa hodari.

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson……………………………………………0764 018535