Jumanne, 9 Agosti 2016

SUBIRA ISIYO NA KIKOMO!



SUBIRA ISIYO NA KIKOMO!


 Ni vizuri kuwa na moyo wa subira lakini sio kila kitu cha kusibiria mathalani uwezi ukajenga moyo wa subira kuwa labda kuna wakati maji ya bahari yatakuwa hayana chumvi!
 
Uwa sio ajabu kuona mtu anakwambia hapa nimekaa muda wote kuna kitu nasubiri! Au mwingine akasema nasubiri aseme tu mimi nimalize! Na mwingine atasema na subiri ajikwae tu mimi nichukue mzigo! Na mwingine akasema nasubiri ajipendekeze tu ni mpe yake! Na mwingine atasema nasubiri ajikoroge tu alafu ni mnyweshe! Hatari.

Japo tunajua kuwa SUBIRA kama hali ya kungojelea kitu, ila inakuwa na maana sana kama hicho kitu kinachongojelewa kina sifa ya kungojelewa/ kungojewa………usiwe ukawa unaenda mbugani kutaka kumuona simba akila manyasi kwa hiyo ukapoteza muda, fedha ili kwenda kuona tu ipi siku nitamuona akila majani au ukawa unasubiria kwa hamu kubwa kuona bundamilia mwenye mistari siku mistari hiyo itakapofutika kwahiyo ukawa unakesha na kumuomba Mungu ukitarajia kuwa hipo siku utaona mistari ya pundamilia ikifutika kwa hiyo ukajikita katika kusubiri ukatazamia yasiyo tazamika.

Ni kweli sikatai kuwa kweli subira ya vuta heri lakini ni jambo muhimu kujua kitu unachokisubiria kweli kina sifa ya kusubiriwa au kinasifa ya kupotezewa ni muhimu utambue sio kila kitu ambacho watu wanasubiri basi nawe unabidi usubiri mathalani mtu, ndugu yake akiwa amesafiri inawezekana yuko nchi nyingine hivyo anaenda kituo cha basi au cha ndege kwa ajili ya kumpokea ndugu yake basi nawe ukaenda kituoni kwenda kumpokea kitu kisichokuwepo kwa hiyo ukakaa pale kituoni watu wana wapokea ndugu zao lakini wewe upo tu mpaka mwisho unafika bado upo tu.

Ni  vizuri kutambua kuwa subira ni kitu kizuri ila unasubiri nini ni jambo la msingi ilikujua huu ni wakati wake wa mimi kusubiri hichi kitu au nianze shughuli nyingine nachojua mimi hakuna kitu kinacho umiza sana kama kitu unachosubiria kikawa tofauti na vile ulivyo tarajia mathalani mama mjamzito anapokuwa ana hamu ya kumpokea mtoto wake lakini yale matarajio yake yakawa sivyo hivyo akaingia katika ulimwengu wa maumivu makali baada ya kukosa furaha yake, pia katika ulimwengu wa mapenzi unaweza ukasubiri mtu wangu ipo siku tutafunga ndoa lakini ghafla amebadilika atakikusikia tena habari za ndoa hata ukaendelea kusubiria labda kuna siku ataamka vizuri lakini wapi hatimae ukashuhudia bahari na nchi kavu vikiachana.

Wako watu wanasubiri hadi wanapata magonjwa katika miili yao ( pressure,stroke etc.) na wengine hata kuwa vichaa kwa kutegemea ipo siku atabadilika au mazingira yatabadilika na bado yamekuwa magumu tu tofauti na ulivyokusudia  na wengine atakufikia hatua ya kujiua kwa kuona subira yangu haina maaana kwani ninachosubiria sicho kinachotakiwa kusubiriwa.

Kwa kweli watu wamekuwa na hali ya kusubiri kwa vitu vingi pasipo kujua na hivyo vitu kweli vinawasubiri wao , kwani unaweza ukasubiri embe mpaka lina oza bado wewe unasubiri tu kuwa ipo siku embe lile nitakula tu!

Niseme pole sana kwa wale walikuwa wakisubiri vitu vingi pasipo kutokea au vikawa tofauti na matarajio yao, huna haja ya kuchukua maamuzi yatakayo dhuru nafsi yako au kujenga kisirani maadam unaishi jua kila kitu kitakuwa sawa maadam Mungu ( muumbaji wako yuko nawe).

Mambo ya kuzingatia:

l. Jifunze kitu kutokana na hali iliyokutokea 

 ll.tembea katika njia sahihi

lll.weka imani thabiti kwa Mungu

Tambua sote ni kazi ya mikono yake! Anatupenda atakama tukiwa wachafu kiasi gani aliye ruhusu utoke duniani analo jambo jema na maisha yako. Ni kweli watu wanaweza kukukatia tama lakini kamwe si Mungu! Ifurahie siku yako. Asante!
Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………………..0764 018535