MOYO WANGU UMWABUDU MUNGU!
Yohana 4:22
Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka
kwa Wayahudi.
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa
ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana
Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo
yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Kuabudu kwa neno jepesi unaweza kuita/kusema ni ibada hama
namna unavyoishi katika kuinua na kumtukuza/kutukuza miungu hama Mungu
unayemwamini,
Kama unataka kuimarika na kuwa mshindi na hatimaye kuifikia
hatima yako basi penda sana kujua namna ya kumwabudu Mungu katika viwango vyake
yaani namna anavyotaka,
Kati ya kitu ambacho Mungu akipendi ni kuona watu wake
wakiabudu miungu mengine na ukisoma biblia vizuri utaona Mungu tendo la kuabudu
miungu mingine ameliita kuwa UZINZI/UASHERATI
Ezekieli 23:35
Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa umenisahau, na kunitupa nyuma yako, basi
kwa hiyo, uchukue uasherati wako na uzinzi wako.( ukipata muda soma sura 23
yote uone picha kamili kwanini Mungu apendi ibada yake ichanganywe na vitu
vingine).
Majibu mengi ya maswali yanapatikana pale unapoamua kumwabudu
Mungu naam burudiko la moyo wako linalobariki moyo wa Mungu linazaliwa hapo,
maana burudiko linalokuja baada ya kupata hela au kuambiwa asante hama
nakupenda linakuwa sawa na mtu anayejiachia akitegemea kimvuli kitamdaka,
Lakini jambo jema sana hakuna ufundi wa kumwabudu Mungu
kwakua namna yetu sio namna ya Mungu, yeye anajua namna ya kuabudiwa kupitia
Roho yake atatuchukua na kutupeleka kufanya ibada ile tunayopaswa la msingi
wewe uweke tayari mwili na akili yeye adhirishe uweza wake kwakua wewe wake na anaweza kuutumia mwili wako kama
anavyotaka akiamua kuugalagalaza chini, kukurusha juu hama kuupiga magoti awe
na uhuru kwako,
Na mara zote ibada inafanyika pale tu moyo wako
utakapofunguka na kujenga imani ya kile unachokiamini kuwa ni kweli na
kitakusaidia na huku ukiwa na imani kuwa ibada yako inafika sehemu husika,
Katika ibada hama kuabudu haiwezi kufanyika bila MOYO
KUFUNGUKA kwa maana hapo ndipo
kunaruhusu ibada ipite kwenye damu, mifupa na nyama yaani pindi moyo wako
unapokuwa umefunguka basi hapo mwili wako unakuwa sio mali yako tena yeye Mungu
anaweza fanya chochote katika mwili nawe unaweza ukawa unajua hama ujue lakini
kwasababu unakuwa moyo umefunguka kwake basi wewe unakuwa radhi tena katika
hali ya kupenda zaidi sana kuridhika,
Na katika kufanya ibada hama kuabudu ambayo yeye vile
anavyotaka inakuwa ni rahisi yeye kujua wewe ni wake nay eye atawajibika juu
yako kwakua anajua furaha yako ni furaha yake na hata huzuni yako inakuwa yake
kwakua kwake umesha mpa kila kitu na hakuna kificho kwake kwa lugha rahisi wewe kwake hauna kauli hama
pingamizi kwa lile analotaka maana wewe ni mali yako,
Kumbuka kuwa Mungu ni mungu mwenye wivu anajua kila kitu
kinachoendelea mwilini mwako na hata katika mawazo yako na atajisikia vibaya
kuona mali zake zinatumiwa na vitu/ watu wengine na wala sio yeye.( uwa apendi
kuona penzi lake linachanganywa na kitu chochote).
Kuabudu ni hali ya akili kupotea kabisa, mawazo yaliyo jaa
mapenzi kwake na mwili ulitayari kuyafanya yale tu atakayo na wala sio kitu
kingine…………. usijali kama ujafika hatua hii ila jitahidi ufike hapo kwakua
kumfurahisha zaidi ndipo hapo unaweza kumshawishi na yeye ahusike zaidi kwako,
Ni vizuri niseme kuabudu sio kunyoosha mikono hama kutoa
machozi wala kugalagala bali ni kile kinachoendelea ndani yako kinacho mpa
utukufu Mungu, japo kuwa hayo yanaweza kuwa ni ishara ya upendo wako kwa Mungu,
sawasawa na mtu kukuchekea sio kukupenda japo inaweza kuwa ni ishara hama
uongo.
Kuna mambo mengi yanafanyika pindi moyo wako unapoamua
kumwabudu Mungu tu! Yako matengenezo, uimarisho na kuwa namna ya ajabu sana, na
kung’aa sana katika maisha yako
Kuna vifungo vinakuachia, maswali yanapata majibu na moyo
unahimarishwa na nguvu zake.
IBADA YANGU KWAKE NDIO
FURAHA YANGU!
INAITWA SIKU! BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson………………………………………………..0764
0185353