Yohana
21:1…….
1 Baada ya hayo Yesu
alijidhihirisha tena kwa wanafunzi wake, penye bahari ya Tiberia, naye
alijidhihirisha hivi.
2 Simoni Petro, na Tomaso aitwaye
Pacha, na Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, na wana wa Zebedayo, na wengine
wawili wa wanafunzi wake, walikuwapo pamoja.
3 Simoni Petro aliwaambia, Naenda
kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka,
wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.
4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu
alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.
5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu,
mna kitoweo? Wakamjibu, La.
6 Akawaambia, Litupeni jarife
upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza
kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.
Masumbuko ya wanafunzi wa yesu yalitatuliwa baada ya kufuata neno
lililotoka katika kinywa cha yesu “
litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata”
Moja ya sababu za harakati za wengi hasa katika dunia
tuliyopo ni hali ya kutafuta utoshelevu ( hali ya juu katika kukizi mahitaji
binafsi ).
Kuna aina mbili ya utoshelevu katika dunia ( ulimwengu );
i.
Utoshelevu
wa nafsi
ii.
Utoshelevu
wa mali
Unaweza kuwa na kila kitu lakini bado nafsi ikajisikia bado
ina uhitaji mkubwa, unaweza kuoneka kwa macho au wakufukirika tu lakini uhalisi
unabaki kwako.
Unaweza kukuta mtu atulii kuanzia mwili hata akili, na hali
hii uweza kumtokea katika harakati za kuhitaji kukizi uhitaji alionao ili
utoshelevu uweze kudhihirika katika maisha yake.
Wako watu wanaacha kazi, huduma au shughuli binafsi baada ya
kuona kitu anachokifanya akimletei utoshelevu anaoutaka, na hata wakati
mwingine hata kule alikoamia kunaweza bado pasimpatie utoshelevu
anaoutaka/alioukusudia akabaki kung’ang’ana tu.
Moja ya jambo au kitu kinachoweza kuwafanya watu kushindwa
kufikia katika utoshelevu wa jambo lililokusudiwa ni mtazamo usio sahihi wa
jambo husika ( matarajio ya kufikirika yasio na uhalisia ).
Wakati mwingine unaweza kukuta unaacha kitu sahihi
ulichotakiwa kukifanya kilicho sahihi kabisa na ukaenda kufanya kufanya kitu
kingine kabisa ambacho ukutegemewa kufanya lakini ukaona neema za Mungu
zikizidi kukuzingira na kukupa mkate wa kila siku hali hiyo haina maana kuwa Mungu
anafurahia.
Yohana
21:15…………..
Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni
wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua
kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu.
Baada ya yesu kuhakikisha simon petro ameshakula ndipo
akamuuliza swali “ je! Simon wa yohana, wewe wanipenda…………………. Akamwambia
chunga kondoo zangu” ( maana petro baada ya kupewa samaki na kula ndipo yesu
akamkumbusha jukumu lake la msingi la kukaa na kuendelea kumsubiri bwana hata
ujio wa Roho mtakatifu utakapofika au kuajilia.
-
Ndomana
yesu anajaribu kumsisitizia asisahau kuishi kwenye kusudi lake hata kama hali
ikiwa ngumu kiasi gani? Atulie hapo maana yeye aliyekupa neema ya kuwa hapo
atakupa utoshelevu wake.
Uhitaji wowote ulio katika mwili ( uhitaji wa nafsi ) uwa
hauna kikomo na ukisumbukia hauwezi kudumu katika lengo kuu uliokusudiwa na
hivyo kupelekea kushindwa kupata utoshelevu usioisha.
Ni muhimu utambue utoshelevu uliobebwa na neno lililo katika
kinywa cha yesu, anachosema ndicho kinachobeba utoshelevu kinachoshikiliwa na yeye
mwenyewe.
Penda kuishi sawa na neno linalotoka katika kinywa cha yesu
mwenyewe na sio sawa na wimbi la dunia linavyokwenda, kwakua linavyokwenda
linakwenda na kishindo cha kukutisha
hama kukufanya uweze kupata wasiwasi juu ya mstakabali wa maisha yako husika.
Wewe ni asili ya NENO unapolikubali linaenda kutibua na
kuanzisha utoshelevu wake na sio wa kufikirika katika akili?
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………… 0764
018535