Katika dunia ya leo moja ya kitu cha maana kwa watu wengi ni namna anavyotambulishwa, vile unavyo mtambulisha itafanya ajisikie vizuri kuwepo na asijute kwanini nimekuja.
Kuna baadhi ya watu ukikosea kuwatambulisha kwa hadhi waliyonayo, usishangae ghafla akachukua maamuzi ya kuondoka au akavumilia ila baadae akakufuata na kukwambia “ sijapenda jinsi ulivyo nitambulisha “ hivyo utambulisho umekuwa jambo la msingi hata kuliko chakula cha gharama yoyote ulichomwekea.
Na katika dunia hii kuna utambulisho mwingi na wakati mwingine kila utambulisho unakuwa na sababu zake au msingi wake.
Kuna wakati unaweza kutambulishwa hata kama hauna sifa hizo lakini yote ni katika ushawishi ufanye matakwa yao hama katika kukufanya utoe mchango au ahadi kubwa itakayo wafurahisha hao watu, na pindi utakaposhindwa kufanya matakwa yao huo utambulisho hautausikia tena ukitamkwa kinywani mwao.
Kwa asilimia kubwa utambulisho ubadilika kutokana hatua mpya utakayopiga katika maisha yako mathalani ulikuwa binti baada ya kuolewa utaitwa mke na baada ya kuzaa utaitwa mama, ndivyo hivyo hata upande wa elimu kadili unavyozidi kusoma kutoka hatua ya kwanza na kuendelea ndivyo utambulisho wako utakavyobadilika mathalani kutoka shahada moja kwenda shahada ya pili hama kuongeza elimu katika taaluma yako na hata ukawa dokta hivyo ndivyo utambulisho wako utakavyobadilika kadili unavyoongeza elimu yako.
Naam hivyo kuna utambulisho unaotokana na ulimwengu hama dunia pia kuna utambulisho unaotoka mbinguni kila utambulisho una utaratibu wake ili ukufikie lakini utofauti mkubwa katika ya utambulisho wa mbingu na duniani ni kutokuwa na mipaka katika utambulisho wa kimbingu kwakuwa wenyewe ufanya kazi/utawala dunia hata mbinguni.
Ila ni maamuzi binafsi uishi katika utambulisho upi kama wa mbingu au dunia? Kila utambulisho una utaratibu wake, na kila maisha unayoishi yanaonyesha utambulisho gani inabidi uambate katika maisha yako.
Utambulisho wa dunia unahitaji akili nyingi ( za kidunia ) katika kuujenga na kuutetea ili uendelee kuwa nao, ila utambulisho wa mbingu una namna yake wala ahuhitaji usaidizi wako bali unahitaji usaidizi wa kudumu katika maelekezo yake ili nao uzidi kushamiri ndani yako.
Na utambulisho wa kimbingu huu ni utambulisho ambao ulikuwa nawe kabla ujazaliwa au ujaja duniani ulishaunganishwa tangu tumboni mwa mama yako.
Yeremia “ Nalikujua tangu tumboni mwa mama yako………….”
Yeremia 1:5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Ukitaka kuushinda dunia lazima ukubali kuishi katika utambulisho kimbingu maana huo ndio utambulisho ulikuwa nao kabla ujazaliwa na baada ya kuzaliwa na hata hitimisho la maisha yako.
Utambulisho wa kimbingu unakufanya uishi maisha ya ushindi hapa duniani na kufanya uishi maisha yaliyo salama.
Pindi unapoishi maisha ya utambulisho wa kimbingu basi hapo udhihirisho wa nguvu ya Mungu katika hatua za maisha yako unakuwa dhahiri.
Uwezi kuufurahisha moyo wa Mungu endapo hautakubali kuishi katika utambulisho wa mbingu maana hapo hauwezi kutembea katika akili yake hivyo ushindi ni ngumu kudhihirika katika maisha yako.
Tamani na uwe na fahari katika kutembea ndani ya utambulisho wa kimbingu maana kwa huo utambulisho unakuwa vile Mungu anavyotaka uwe.
Utambulisho wa Mungu unatunzwa kwa gharama yoyote kwakuwa usipotunzwa unaondoka kwako hapo ni lazima ukubali kufuata maelekezo yake kwa gharama yoyote ili uendelee kuishi ndani ya utambulisho huo.
INAITWA SIKU| BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson…………………………………………………………….0764 018535