Kuishi ni jambo moja na hatma ni jambo lingine, kwa maana unaweza ukaishi ila usiishi katika hatma yako.
Wakati mwingine kuishi kwenye hatma yako inakuja baada ya kujivumbua kwa walio wengi ila kwa upande wamchao Mungu unajikuta unamsukumo wa ndani zaidi katika jambo fulani kuliko jambo lingine.
Ili uweze kufurahia kuwepo hapa dunia unahitaji kuwa na furaha ya Mungu na furaha ya Mungu inapatikana pindi utakapoishi katika hatma uliyokusudiwa/ aliyokukusudia.
Na hatma ya Mungu inaanza kuchukua nafasi ndani yako mara baada ya wewe kuokoka, hauwezi kutembea katika hatma ya kimungu bila kuokoka!
Naam katika ulimwengu wa sasa na namna dunia ilivyochangamka watu wengi awatafuti hatma zao bali utafuta fursa ili maisha yaende.
Maana fahamu za watu ufikiri kuitafuta sana hatma yako inaweza kupelekea kuishi nje na wakati unaoenda kasi. ( huendi na wakati )!
Na baadhi ya fursa zinaua hatma za watu kwa kujua au kutojua.
Ni kweli hali ya dunia ya sasa ina namna yake ya kuishi ili ukubalike lakini maisha baadae yanategemea namna ulivyouitumikie hatma yako ya sasa na ustawi wake.
Hauwezi kuwa wa maana kwa Mungu kama utaishi nje ya hatma ya kimungu mbele zake.
Ni kweli duniani watu wameumbwa kutegemezana ndo mana kuna watu wako kwa ajili ya wengine zaidi na neema inakuwa juu yao.
v HATMA ni kile kitu kwa hicho uliumbwa au kuzaliwa wengine wanaita “ talent” na kila mtu ana kipawa chake mwingine ni bora katika kuimba, kupiga vyombo vya muziki, wengine kuongea vizuri, kufariji, matendo mema na wengine kufadhiliana.
Wako wengine wanaonekana sana kuwa waongeaji sana, wengine wamepewa jina na kuitwa kilopo au wambea na mengine mengi. Lakini Mungu aliwakusudia kuwa ni watu wamuongelee yeye kwa watu wengine biblia inawahita wainjilisti,
Hatma inafanya kazi kwa ukamilifu mahali ambapo yeye yupo kwa kusema hivyo ni lazima uwe umeokoka ili Mungu ajifunue kupitia wewe.
Unahitaji kusimamia hatma yako haijalishi watu wanakuonaje ili usababishe furaha ya kudumu katika moyo wa Mungu.
Ili uweze kukitumia kipawa chako vizuri unahitaji uwezesho wa Mungu maana kwa yeye ulitokea na kwa ke utarejea.
Namna dunia ya sasa ilivyo na ushawishi mkubwa unaweza kuingia katika mkondo ambao sio wako kutoka na ushawishi unaotoka ndani yako au nje yako, katika hali hiyo unaweza kuwa na furaha kitambo labda kutokana na jambo hilo basi familia yako unaweza kuihudumia na hata watoto kwenda shule pasipo msongo wa mawazo lakini utakosa furaha kamilifu ndani yako.
Unapo pata neema ya kuishi hapa duniani usitake wewe binafsi uyafurahie maisha yako kwa kuishi maisha unayoyataka bali mfurahishe yeye anayekumiliki anapoyaona maisha yako kwa kuyafanya yale uliyokusudiwa,
Unahitaji kujua ni furaha ya Mungu wewe uishi kwenye hatma yake ili ajisikie vizuri kukupa hazina zake uweze kuziwakilisha dunia kama apendavyo yeye.
Unapoamua kuishi maisha ambayo ni burudiko kwa Mungu naye atafanya burudiko katika maisha yako.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson………………………………………………………..0764 018535