Jumanne, 8 Septemba 2015

JANA SIO LEO



JANA SIO LEO


Hakuna leo bila jana na hakuna maana ya jana bila leo!!!!!!!

Jana na leo tunaita utofauti wa siku, kwa maana siku iliyopita tunaita jana na siku iliyopo aua inayoendelea tunaita leo!!

Kwahiyo unaposikia neno jana na leo sio kitu cha kukushtua au kukushangaza kwa maana umekuwa ukisikia na bado unaendelea kusikia na nzuri zaidi wewe mwenyewe umekuwa shuhuda ukiona jana ikibadilika na hatimae ikawa leo……..asante kwa hilo!

Tutakubaliana kwa dhati kabisa kuwa siku inapobadilika inabadilika na mambo yake na unaweza ukagundua sasa au baadae mathalani mtu anapokuwa akikua ni ngumu kutambua sasa mtu ndio ninakua katika kitendo kinachoendelea sasa bali baada ya muda ataona  mabadiliko ndipo unapotambua mtu huyu amekuwa hivyo inakuwa umeweza kuitofautisha jana na leo…..asante sana!

Hakuna kitu kizuri kama kuishi kwingi maana walimwengu wanaamini kuwa kuishi kwingi ni kuona mengi pasipo kujali hayo unayo yaona unakuwa katika nadharia hipi au katika wakati gani, na japo watu wengi wamekuwa wakijivunia katika ongezeko la miaka kutokana na vitu hivi viwili yaani jana na leo ndio maana watu wamekuwa wakifisha miaka fulani basi hapo uweza kufanya sherehe ya kuzaliwa (happy birthday) hasa watu wenye kutambua maana yake na mwenye uwezo huo na hasa mwenye nafasi hiyo.

Unapoangalia katika dunia ya sasa unaweza kushangaza sana watu wengi wanaolia wanasema jana yangu haikuwa hivi inaweza kuwa ilikuwa ni nzuri au mbaya lakini ni muhimu aitaje kuonyesha jana yake ilikuwa vipi ikaazaa leo yake………hivyo kucheka au kulia sio tatizo bali katika kuonyesha kuwa naye alipitia katika mwenendo wa siku.

Ni kweli mambo mengi yaliyofanyika kipindi cha nyuma ni tofauti kabisa na kipindi cha sasa japo watu wengi wanasema kuwa ni maendeleo lakini unaweza kujiuliza ni kweli yanaleta maendeleo hayo yanayosema au ni geresha tu.

Sikatai yako mambo ya jana ambayo leo yanaonekana kuwa hayana nafasi tena na hivyo imeweza kusababisha katika harakati za maendeleo kuongeza mwendo katika kufikia hatua bora zaidi kuliko ya awali mathalani kutokana maendeleo ya sayansi na teknolojia imesaidia kwa kiasi kikubwa  katika kuwasiliana kupitia hiyo watu wamekuwa wakiwasiliana katika njia ya sauti na hata ya video na hivyo kujenga ukaribu zaidi miongoni mwa watu na watu hama jamii na jamii.

Yapo mengi kutokana na maendeleo haya yameibua mausiano ya kujenga na mausiano ya kubomoa lakini yote ni matokeo ya haya maendeleo.

Katika dunia ya sasa kila kitu kimekuwa ni biashara hata vile haviuziki sasa vimekuwa na sokoni na vimekuwa na uwitaji mkubwa wa wateja, watu wamekuwa wakiuza kila kitu kinachoonekana katika macho ya nyama na hata kisichoonekana…………..sikuizi watu awajali nini wanauza bali wanchojali ni kiuza nitapata kiasi gani! Sasa sijajua kuwa hii ni dunia ya kibepari au mmomonyoko wa madili katika dunia ya sasa.

Samahani sana sipati picha dunia ya leo kama kusingekuwa na ukimwi sijui hali ingekuwaje na hasa katika jamii ambayo watu wengi hawana hofu ya Mungu bali wanaenda kanisani.

Katika dunia ya sasa HESHIMA imekuwa bidhaa adimu na sijui kuwa kama watu wenyewe wana jishushia heshima  au wanashushiwa heshima au heshima yenyewe inashuka? Bado sijapata jibu lakini kwa macho yangu naona heshima ikishuka kwa kiwango kikubwa sana sio mtoto wala mkubwa kila mtu anafanya kadiri anavyoona sawa machoni pake na sio kama inavyopaswa kuonekana kuwa sawa machono pa jamii nzima.

Kwa upande wa watumishi wa Mungu mambo mengi yamekuwa tofauti hasa katika zama za manabii wa kina eliya,samweli na wengi walikuwa kweli wana muakilisha Mungu sasa hivi imekuwa ni tofauti…..watumishi wengi wamejiusisha na utapeli waweze kuendesha maisha yao na sio kufanya kazi ya Mungu wengine wamethubutu hata kutumia nguvu za giza katika kutaka watu wawaamini na kuwaogopa.

Sina ugomvi na watumishi wa Mungu mimi na waamini sana na ninawapenda sana hasa wanaojua wajibu wao na kumtumikia Mungu katika kweli tupu na katika udhihirisho wa Mungu mwenyewe!

Sisemi uahache kumwabudu Mungu kutokana na mambo yanayo endelea katika dunia ya leo niseme usalama wako sio kumwamini sana mtumishi wa Mungu bali ni kufahamu kweli ya Mungu ambayo itakutunza na kukulinda na kukupa mwendo mwingine katika Mungu.

Msikilize mtumishi wa Mungu kwani yeye ndiye amewekwa kwaajili yako ili akuongoze katika kweli ya Mungu lakini yeye anasehemu yake lakini wewe unasehemu sana ya kufanya ili uone matunda unayokusudiwa ……………kwani mtumishi wa Mungu anakupa mbegu na maelekezo yake lakini kutafuta shamba, jembe ni wewe mwenyewe na kupanda kwa kufuata maelekezo yake ni muhimu sana! Lakini kumjua Mungu binafsi ni jambo la msingi sana kuliko yote!

Hakikisha moyo wako haujabeba chuki wa kisirani katika yote bali umuone Mungu katika kila jambo naye akupe raha ya kudumu au ya milele…………….mwamini Mungu naye anaweza kukutoa wewe pale ulipo na kukuweka katika hatua nyingine iliyo bora zaidi.

Nibora wakuone uendi na wakati kuliko kwenda na wakati huku unabeba historia mbaya!! Ambayo itakutesa katika kesho yako………………………….!

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………….0764 018535

                           MUNGU AKIKUBARIKI HAKUNA ATAYE KULAANI                          

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni