Uweza wa kufanya mambo na ujasiri unaozaliwa/ kutokana na kujitambua.
Kuna kujitambua kunako zaliwa na vitu vingi mathalani kujitambua kunakotokana na mila na desturi katika jamii husika kujua majukumu yake na kuyatekeleza, mara nyingi utegemea miaka ( rika na umiliki) pamoja na nafasi ya mtu katika ukoo na hata jamii husika.
Pia mtu uweza kujitambua hama kuanza kujitambua kutokana na elimu ( rasmi au isiyo rasmi) au baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalamu au wazee wenye hekima.
Ni ukweli usiopingika kuwa uhuru mkamilifu unakuja baada ya kujitambua na bila shaka kuonewa na kuteseka kunakuwa ni maisha yako baada ya kuishi maisha ya kutojitambua au kukubali kuishi maisha ya kutojitambua.
Maisha ya kutojitambua hayana tofauti sana na maisha ya utumwa japo kwa kiasi kikubwa inaweza kuwa ni zaidi ya utumwa, kwani njia rahisi ya kuchukua haki ya mtu mfanye tu asijitambue.
Wagalatia 4: 1 Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote;
2 bali yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba.
Kujitambua kwa namna zote ( mila na desturi, elimu n.k) vinakikomo chake na kwa kiasi kikubwa haviwezi kukupa maisha uliyokusudiwa kuishi mathalani unaweza kuwa mtu fulani kama vile msomi mwenye daraja la juu sana katika masomo yako na zaidi ukawa unajitambua kutokana na elimu uliyonayo , unajipenda , unajielewa lakini maisha yakaenda pasipo kuona yale uliyotegemea mfano.
Ukosefu wa kazi unayotaka hivyo ukajitahidi kuvumilia kutokana na masharti magumu yakupata kazi unayoitaka lakini mwisho ukakubali aibu ya mwili ( rushwa ya ngono) ili maisha yaendelee.
Pia inawezekana ulipata kazi kwa neema tu ya Mungu ( kwa uhalali) lakini ghafla pakatokea na mtikisiko kazini kuwa bila ya kutoa rushwa ( kwa ujumla ) kibarua kitaota nyasi! Hama kujiingiza katika mfumo fulani.
Karibu……………………!!
Nguvu ya kujitambua kunakotokana na Neno la Mungu!
Ø Unaweza kushangaa kuona mtu anaogelea katika bahari kama samaki badala ya kuzama.
Ø Unaweza kushangaa mtu anakula vizuri na kuishi vizuri na zaidi kunawiri wakati ulitegemea ameze vidonge afe kwa kile kilicho mkuta.
Ø Unaweza kushangaa pia mtu uliyetegemea asuse kula na aondoke lakini ukakuta anajiachia zaidi na kupafurahia na huku akila kwa nafasi.
Kujitambua huku ni zaidi ya kulalia/kumiliki madini ( almasi/ tanzanite n.k) maana ubora unaotokana na hali hii hakuna mfano wake.
Unapojitambua kutokana na hali hii hapo ndipo unaanza kuishi maisha aliyokusudia ( maisha uliyotakiwa/ unayotakiwa kuyaishi ) na unapoliishi kusudi la Mungu kwa ukamilifu unakuwa Mungu duniani ( Mungu kuishi kupitia wewe) na udhihirisho wa Mungu unakuwa juu yako.
Kama kweli unataka kujitambua wewe ni nani basi liruhusu neno la Mungu linalokaa ndani yako likutambulishe. Na sio biblia inayokaa chumbani hama sebuleni pasipo kuwa kiongozi wa maisha yako bali kuwa moja ya pambo la nyumba na zaidi sana wakutambue kuwa wewe ni mkristo.
Huu ni utambulisho usiochuja bali unaongezeka siku kwa siku ( utambulisho unaotokana na Neno la Mungu).
INAITWA SIKU! BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………..0764 018535