Ijumaa, 23 Oktoba 2020

SWALI LINAKOSA MAANA!

 



 

Kama binadamu uliopata neema kuingia katika mifumo mbalimbali ya elimu na kufanya mitihani, utakuwa ulishakutana na maswali katika mitihani yaliyokosewa au yasiyo na majibu!

Wakati mwingine swali lililokosewa uweza kurekebishwa ili liwe na MAANA au kubadilishwa na pengine kutoa alama za bure (free masks) ikiwa hilo swali alikujulikana mapema wakati wa mtihani ila baada ya kusahihishwa mtihani likagundulika.

Karibu!!!

Maswali yamekuwa ni rafiki wa akili na hasa katika kupasha joto ubongo, na upelekea hali nzuri kwa akili kupanuka na kupata uelewa mwingine.

Na wakati mwingine mtu anapokosa jibu hali hiyo uweza kuingia ndani ya moyo na kuleta usumbufu, usumbufu wa mtu kuwa na maswali mengi kwa kile kinacho mkabili pasipo kujua niende kushoto au kulia, hali ya swali kuwa na jibu zaidi ya moja na hatimaye kushindwa kupata jibu linalojitosheleza na hata kujikuta uko njia panda.

Pindi inapotokea mtu anapokuwa na maswali mengi kichwani mwake kwa kiasi kikubwa inategemea hulka ya mtu husika wako watu wanapokuwa katika hali hii upenda kucheza mziki, au kupiga makelele,kuongea sana, kukaa kimya na mwingine upenda kulala hama kulewa na mambo mengine yafananayo na hayo lakini bado unaweza kukosa jibu sahihi au lililojitosheleza katika swali husika.

SWALI LINAKOSA MAANA PALE UNAPOPATA JIBU!

Kama samaki anapo poteza makeke yake au usumbufu wake ni pale utakapo fanikiwa kumtoa nje ya maji na kumweka nchi kavu………………………………………………..!

Ndivyo ilivyo pindi utakapopata majibu katika maswali yanayo kukabili hapo akili uweza kutulia na hali ya ushwari uweza kuingia ndani ya moyo wako.

Ndomana waswahili usema “ atafutae achoki na akichoka amepata” hivyo utashangaa pindi mtu atakapo choka wakati ajapata japo yote yanawezekana kutegemea na hali ya ndani ya mtu husika .

Na wakati mwingine unaweza pata majibu lakini sio utatuzi wa leo wala kesho bali utakuweka katika hali njema ya matarajio ya uhakika wa kweli katika majira yajayo.

Usiruhusu maswali yawe maisha yako maana yatautesa ufahamu wako! Bali tambua kwa kila jambo/swali linalokuja katika maisha yako uwa tatizo linaisha ni mpaka ujue majibu ya maswali hayo yanapatikana wapi? Maana ukikosa kujua sehemu husika hauwezi pata majibu ya uhakika.

“ hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea”

 

1 Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Endapo ikatokea ukakosa majibu ya maswali yako kwa wanadamu ( watu unao waamini) usihofu wewe fungua hazina ya mbingu hiyo uwa haikosi majibu maadam mbingu hipo basi mwenye mbingu yupo na majibu yapo.

Haya ni majibu yanayoleta amani ya kudumu, maana hicho ndicho chanzo sahihi cha majibu ya maswali yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………0764 018535

Jumanne, 6 Oktoba 2020

SEHEMU SALAMA!

 



 

Sehemu salama ni hitaji la kila binadamu mwenye kujielewa na kujithamini, ni kama fedha isivyokuwa na adui bali kila mmoja uhitaji kwa matumizi yake binafsi sawa na halmashauri ya ulimwengu wa fikra zake.

Wakati mwingine ni ngumu kutambua hapa ni sehemu salama au si salama kwa muonekano tu, kwani kuna mahali panaweza kuonekana kuwa ni sehemu salama kwa macho lakini usalama unaonekana hapo kinaweza kuwa ni kichaka cha kuficha uharibifu.

Ni kweli kuna sehemu panawezeka kuonekana kuwa hapo usalama ulizaliwa hapo kutoka na ulinzi mkali na mitambo ya kutosha iliyopo! Lakini uharibu wa siku moja unaweza ukaharibu hiyo sifa ya sehemu hiyo.

Usalama mbali na sehemu/eneo husika pia unaweza kuhuamishia kwa mtu,ukafikiri ninapokaa au kuongea naye siri zako basi maisha yangu yatakuwa salama hali hiyo inaweza kuwa kwa kitambo tu baadae anaweza asiwe salama kwako bali akatumia nafasi hiyo kukuharibu kabisa.

Katika hali ya dunia inavyoaminika na kusema sehemu hii ni salamu au mtu huyu ni salama hali hii inazidi kupungua kutokana na matokeo yasiyotegemea kutokea na kuzidi kuushangaza ulimwenguni,yale ambayo ukutegemea kutokea sasa yanatokea na kuwa ni mambo ya kawaida.

Mathalani wapo waliweka imani kubwa kwa wazazi wao wakitegemea kwao hapo ni sehemu salama lakini mwisho wakatolewa kafara.

Sasa sehemu salama utaipata wapi? Utaijuaje? Ili uweze kuwa salama isiyokuwa na maswali yoyote!

Ili upate usalama wa kudumu na wa uhakika ni lazima urudi kwa yeye aliye asili ya vyote vinavyoonekana na visivyoonekana “ SIR GOD “

Mbali na usalama huu hakuna mahali pengine penye usalama wa kudumu, kwa maana usalama mwingine utengenezwa na akili za wanadamu au mazingira yanayokushawishi kusema sehemu hii ni salama lakini hali hizo zinaweza kubadilika na kuleta maafa.

Ninao ushuhuda wa mtu aliyefikiri kuwa sehemu hii ni salama kwake au kwa mtu ukafikiri kuna usalama kwake lakini baadae akakengeuka kabisa na kusababisha majeraha makubwa ndani ya moyo wa mtu lakini sijawai kuona kwa mtu aliyemfanya Mungu kuwa ni sehemu salama kwake alafu Mungu akawa si sehemu salama kwake.

Ukimfanya Mungu kuwa ni salama kwako naye atakuletea salama yake katika kila jambo na kamwe hawezi kukudhuru kwa kuwa teso la moyo wako ndio teso lake.

“ Nitakuwa pamoja nawe taabuni”

Mfanye Mungu kuwa salama yako hauwezi juta, atakufanya uyafurahie maisha yako kwa maana ni yeye alikutambua kabla ujatokea duniani na kizuri zaidi anampango mwema juu yako.

Hautaji kuchoka katika usalama wako na Mungu bali wewe kubali kufuata maelekezo yake naye atakupa usalama wake na kuzidi katika maisha yako.

“ msikilize uwe salama ndani yake “

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………0764 018535

 jibu