Ijumaa, 20 Agosti 2021

MAAMUZI YANGU NDIO HATIMA YANGU

 


Moja ya kitu kinacho kutambulisha kuwa wewe ni mtu huru ni uwezo wa kufanya maamuzi na kuyasimamia hayo maamuzi sawa na utashi wako!

Na kwa maisha ya kawaida kama binadamu uwa unaongozwa na maamuzi maana kila kitu kina bebwa na maamuzi, ili kufanya hiki na kuacha hiki kinategemea maamuzi ya moyo wako,

Maamuzi ni hali ya kukataa hali fulani na kukubaliana na hali fulani ( kukataa na kukubali )!

Japo yote uitwa ni maamuzi lakini kuna maamuzi ya hiari na yasiyo ya hiari, na maamuzi yanaweza kuweka makao katika akili yako hayo ni maamuzi uliyoyafanya kwa utashi wako na ukaona matunda yake kwakuwa ni maamuzi ya kusifia nafsi yako au kulaumu nafsi yako na sio mtu mwingine mathalani wewe ni binti uliye jitunza akatokea kijana mtanashati akakutongoza nawe kwa utashi wako ukamkubali lakini asikwambia kama ameathirika na UKIMWI baada kuingia maisha ya ndoa ukaamua kujikuta umeambikizwa.

Yote juu ya yote jua kila maamuzi yoyote utakavyo yafanya lazima ujue yana mchango mkubwa katika hatima yako kuifikia au kutoifikia hama kuijenga au kuibomoa.

Hivyo mtu anayeipenda hatima yake utamuona umakini anaoutumia katika kufanya maamuzi uwa amui tu kwa sababu anajisikia kuamua.

Hivyo hauwezi kuwa makini na hatima yako pasipo kuwa makini katika maamuzi unayoamua kila siku.

Wakati mwingine mtu wa namna hii uweza kuhatarisha maisha yake lakini kipindi hicho unamuona anahatarisha maisha yake lakini hapo inawezekana analitumikia/kuishi hatima yake.

Pindi utakapo tembea katika maamuzi sahihi au vigumu sana kuona watu kama kizuizi katika kuitumikia hatima yako iliyowekwa na Mungu.

Ukishindwa kusimamia maamuzi sahihi ni ngumu kuitumikia ndoto/hatima yako.

Kumbuka pindi unapochukua hatua ya hatua ya kuitumikia kuna maisha ya wengi watapona: matasa wanaweza kupakata, wajane wanaweza kupa tumaini jipya na hata yatima wakapata faraja ya kweli ya kudumu lakini hayo yote yanajengwa na umakini katika maamuzi yako.

Ni muhimu ujue ustawi wako uko pale utakapolitumikia/kuishi katika hatima yako, hivyo penda sana kuishi hatima yako kwa kuzingatia hatima yako.

Na ni vizuri hata pale utakapoicha dunia ni vizuri uwe ndani ya hatima yako kuliko uwe nje hatima maana usipoitumikia hatima yako unaweza kupoteza maana ya wewe kuwepo duniani na hata kukupelekea kukosa mbingu.

Unapoamua kuitumikia hatima yako hauhitaji kujiona au kujifananisha na watu wengine maana inaweza kupelekea kujiona mnyonge au uko zaidi yao pasipo kutambua kila mtu utembea katika njia yake, hakuna haja ya mashindano.

Unapoitumikia hatima yako ndio furaha ya Mungu lakini hauwezi kuitumikia hatima yako kama haujawa na usahihi katika maamuzi yako.

Lazima utambue/uone kuna muonekano bora wa maisha kikamilifu nje  ya kusimamia hatima yako au ndoto yako!

Uwezi kuwa salama au kuyafurahia maisha kikamilifu nje ya kuisimamia hatima yako!

Kwakuwa unapoitumikia hatima furaha ya bwana inakuwa kama chemichem isiyo kauka katika moyo wako hivyo nguvu zako zinakuwa nyingi.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………….……….0764 018535

 

Ijumaa, 6 Agosti 2021

ISHI KATIKA SAUTI YA MUNGU

 



Sauti ya Mungu, uwa inabaki kuwa ni sauti yake iliyojaa ukamilifu wa utimilifu wa ahadi zake au yale anayo yasema, lakini kazi inakuwa kwetu kuendelea kuisikia sauti ya Mungu au kuishi ndani ya sauti yake!

Ni vizuri usiishie kusikia tu bali penda kuishi ndani ya sauti yake Mungu.

Waenda kanisani wengi upenda kusikia sauti ya Mungu kama sio kutoka ndani yake basi itoke kwa mtu anayemuamini.

Ni kweli unaweza kusikia sauti ya Mungu na ukatoka katika hali fulani kama sio jambo fulani lakini usiendelee kuishi katika hiyo sauti japo unaweza kuwa muudhuriaji mzuri wa vipindi kanisani hata mchungaji akakupenda sana, mathalani wana Israel walipofika bahari ya sham na kukosa mwelekeo hapo waliisikia sauti ya Mungu kutoka kwa Musa na kupitia katika bahari sham lakini wengi wao baada ya kuvuka hile bahari awakuendelea kuisikiliza/kuifuata kama sio kuiamini sauti ya Mungu.

Na ndio maana sio wote walioweza kuingia nchi ya kanani,

Lazima utambue lengo la Mungu/tamanio la Mungu ni uishi katika sauti yake zaidi sana maisha yako yatawaliwe na sauti yake.

Ni muhimu uishi katika sauti yake ili uweze kuyaishi maisha uliyokusudiwa na sio ya neema tu.

Ni vizuri kutambua kuishi ndani ya sauti ya Mungu haya ni maamuzi ya mtu yaliyo tayari kubeba gharama zitokanazo na maamuzi aliyoyachukua.

Naam kuishi katika sauti yake ni sawa na samaki kuishi majini yaani maisha yaliyo tengenezwa na Mungu wewe uishi humo.

Na jambo lisilopingika usipoishi katika sauti ya Mungu basi utaishi katika sauti ya dunia na dunia itakutesa japo utakuwa unaenda kanisani.

Moja ya kigezo cha kuonyesha unampenda Mungu ni kukubali kuishi katika sauti yake NO MATTER WHAT! Haijalishi nini kinaendelea katika maisha yako.

Kukubali kuishi kwa sauti ya Mungu ni kukubali kuyateketeza maisha na kuwa majivu ili yaweze kuwa manukato kwa Mungu.

Ili uwe na imani thabiti juu ya Mungu na isiyo na shaka kamwe ni muhimu ujifunze kuishi katika sauti ya Mungu.

Nje ya kuishi katika sauti ya Mungu sahau kuishi katika maisha ya ushindi wa kishindo.

Unahitaji kuishi katika sauti yake ili mahali penye giza pawe na nuru, mahali ambapo wengi wanakimbia basi uwepo wako unaweza fanya jangwa kuwa sehemu yenye rutuba ambapo watu wengi watatamani kuwa hapo.

Maana ya wewe kuwepo hapo inakuja mara tu ya wewe kudumu katika sauti ya Mungu maana hapo utafanyika kuwa majibu katika maswali ya wengi.

Usikubali kizuizi chochote kikizuie kuishi katika sauti ya Mungui haijalishi urafiki,mahusiano au chochote  bali jua wewe kuishi humo vyote vitarudi vyenye utukufu zaidi vilivyobeba hatima njema katika maisha yako.

Usiogope kutoeleweka na watu wako karibu hama kuachwa kwa watu uliowategemea pindi unapochukua maamuzi ya kuishi katika sauti ya Mungu, Mungu anaweza kukuondolea watu/vitu visivyo stahili ili vije vyenye vya kukufaha zaidi.

Usalama wako unaimarishwa pindi utakapoishi ndani ya sauti yake!

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………………….0764 018535