( Sio kila kitu unavyokiona ndivyo kilivyo )
Watu usema uelewa ( maarifa ) ni nguvu, kweli ni nguvu inayoweza kukupeleka kufanya maamuzi sahihi.
Unapo pambana na jambo pasipo kutafuta muhafaka wa njia itakayokupa utatuzi wa sahihi wa jambo hilo bila shaka hali hiyo inaweza kukupelekea kuchoka kama sio kujichosha.
Wakati mwingi jambo lolote linalokupata au kukutokea kutokana na uelewa sahihi uliojikita katika fahamu zako unajikuta ujasiri na kujiamini unakuwa fungu lako ( endapo ukijitambua ).
Moja ya kitu kinachopelekea kufanya maamuzi mabaya ni ujuaji ( kujiona unajua na hakuna wa kukushauri ).
Ni muhimu utambue maadam unaishi basi jua unayahitaji maarifa ( uelewa ) ili kuleta umaana wa kuwepo na kuishi kwa furaha!
Na muhimu ujifunze maadam upatapo nafasi ya kufanya maamuzi basi ujue wakati au miaka hairudi nyuma.
Ni muhimu uchelewe kufanya maamuzi ukitafuta maamuzi sahihi ili ya kuweka katika nafasi nzuri usalama wa kesho yako.
Ni vizuri upate uelewa sahihi ni kwa ajili ya faida yako na jamii inayokuzunguka.
Hata kama jambo linafanyika kwa namna uliyozoea tambue majira yanabadilika namna ya kuyafanya jambo hilo linaweza kubadilika na kukupa matokeo tofauti.
Mathalani katika mambo ya Mungu…tunamuona musa aliambiwa mara ya kwanza upige mwamba kasha ukatoa maji na mara nyingine aliambiwa ahuamuru mwamba utoe maji ila yeye aliupiga tofauti na maagizo aliyoambiwa/aliyopewa.
Tambua majira yanapita hivyo kukosea kosea kunaweza kufanya kuchelewa kufikia pale ulipokusudiwa, ni vizuri utambue uelewa sahihi ukuwezesha kule ulikokusudiwa ukiwa kamili katika akili na neema kamilifu.
Hali ya kupenda kufanya maamuzi kabla ujatafuta uelewa sahihi wa jambo husika unaweza kukutana na mtihani wa chuo kikuu wewe ukajibu kidarasa la saba ukadhani maadamu ni maandishi yameandikwa kwenye karatasi nyeupe basi majibu yake yatakuwa sawa tu pasipo kujua hayo maswali ni kiwango/kidato gani? Ili uweze kujibu sawa na kidato/kiwango husika.
Ni vizuri kutambua kuwa sio kila maamuzi unaweza kuyafanya matokeo yake yatapotea/kusahaulika kirahisi tu bali yako maamuzi ambayo matokeo yake yanaweza kugharimu maisha yako yote mathalani unapofanya maamuzi ya kuua na ukapatikana na hatia maisha yako yanaweza kuishia jela au kunyongwa hadi kufa.
Uwa atufanyi maamuzi kwa kuangalia watu wanataka tufanye hivyo bali kwa kujali na kuthamini ustawi wa hatma iliyoko ndani yetu.
Ni muhimu kufanya maamuzi kwa kuboresha kesho yako na sio kutimiza matakwa ya mwili wako!
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………………………………0764 018535