Ijumaa, 29 Julai 2022

HAKUNA KITU KINAKUTOKEA PASIPO SABABU;

 



Ni kweli unaweza usijue kwanini hilo limekupata lakini hilo jambo linasababu yake kuja kwako na kukupata.

Kulia ni jambo linalotokea katika maisha ya kila mwanadamu kutokana na jambo husika lakini huzuni nyingi na ukiwa ulioambata na machozi unakuwa ni kwasababu ya kukosa kujua kwanini jambo hili limekupata wewe na wala sio mwingine.

Kutoka uko liliko toka na kukufikia wewe sio bure ila linakuwa na sababu ya kukufikia wewe! Haijalishi lengo lake kuwa zuri au baya,

Litakuwa tayari lina ramani ya kukufikia au sababu ya kuja kwako!

Inaweza kuwa ni sababu iliyo katika uovu au ni sababu inayotengeneza kesho yako yenye baraka.

Naam kila kitu kinacho kufuatilia kina kuwa na sababu ya kukufuatilia unaweza usiijue lakini uwa kuna sababu ya kukufuatilia pia inaweza kuwa imetumwa na mtu au umeisababisha mwenyewe kikufuate kwa kujua hama kuto kujua.

Laiti tungejua kwasababu gani haya yanakupata au yanatokea kwa asilimia kubwa tusingeweza kujilaumu au kulaumu watu zaidi ya kutafuta namna ya kutoka hapo au kusubiri kwa furaha hadi wakati sahihi wa ustawi wako.

Sio kila kitu ambacho unakiona kuwa ni kizuri na unasababu ya kukipata na endapo ikatokea ukakikosa basi ukaishia kulaumu na hata chuki kuzaliwa ndani yako hali hii sio sawa.

Mambo mengi yanakaa kwa muda mrefu au yanachelewa kwasababu tunakuwa atujui kwanini  yanatokea au kusudi la kutokea.

Mara nyingi yanapotokea mambo mabaya tunakuwa ni watu wakujilaumu au kuwalaumu watu na pengine watu uweza kwenda mbali zaidi hata kumlaumu Mungu lakini mwisho unaweza kumshukuru Mungu, mathalani unaweza kuwa na mtu kwenye mahusiano  na ikatokea umempenda sana hata ukasema hata ikitokea yeye amekufa basi utajiua ili mapenzi yakaendelee peponi ( sijui uko kama mapenzi yanaendelea ) naam ikatokea mahusiano yamekatika/yameisha ukapatwa na bumbuazi /butwaa usijue lakufanya bali machozi yako yakawa chakula chako usiku na mchana, naam ukaone bora ulie siku nzima kuliko ule chakula maana akipandi, muda si mrefu ukapata habari kwamba yule mtu uliyempenda sana  amefriki na ugonjwa wa ukimwi muda si mrefu ( na ulikuwa ujui kama ameathirika ) bila shaka baada kupata pumziko kwa muda bila shaka unaweza kushusha pumzi kuanza kuona thamani ya chakula na kuanza kula.

Sio kila kitu unacho kosa kikupe sababu ya LAWAMA.

Ni kweli mambo mengi yanayo kutokea yanakuwa hayana taarifa za kufanya uweze kujiandaa, ila jambo husika linakuwa katika ratiba yake ambayo wewe uwezi jua kwanini hili lakini wewe unaweza usijue na pengine ukajiona vile unavyojiona sasa.

Lakini katika yote kikubwa jipe nafasi ya kutulia mbele za Mungu, hakikisha nafsi yako inatulia mbele zake kwa ukimya wa tofauti, na hapo fumbo linaweza kutatuliwa na hata kupata amani ya kustahimili kipindi hicho.

Bila shaka ufumbuzi au sababu ya jambo hilo linaweza kuwa kwa njia ya ndoto , sauti mawazoni mwako hama sauti itokayo na neno la Mungu ndani yako.

Usipotafuta sababu zaidi ya kutaka nani wa kumlaumu hauwezi kukata tamaa wala kumbebesha mtu lawama na hapo utaona njia na hatimaye kupita hapo salama.

Unapojua sababu ya jambo hapo uwezi kuona kama kunakuchelewa wala kushindwa.

Kujua sababu ya tatizo/jambo hapo ndipo chanzo sahihi na jicho sahihi na jibu la uhakika katika kutoka pale ulipo.

Kila jambo linalo kutokea uwa lina maana yake lakini shida ni pale tu ile maana! Na endapo ukajua hiyo maana basi inakuwa sio shida tena.

Ni sawa na mlango ulifungwa kwa muda mrefu kwa kukosa funguo lakini ikatokea ukaiona fungua yake basi hapo unakuwa sio mlango uliofungwa tena mbele ya macho yako!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………..……….0764 018535

 

Jumamosi, 16 Julai 2022

YAELEWE MAJIRA YAKO!

 



UNDERSTANDING YOUR SEASON!

Usipoyaelewa majira kuna uwezekano mkubwa wa kupishana na ustawi wako,

Unapoishi pasipo kuelewa majira yako unakuwa sawa na:

(a)    Kwenda baharini na uku ukitegemea kumuona mamba akipiga mbizi! Ambacho ni kitu kisichowezekana

(b)   Kupanda mahindi na uku ukitegemea kuvuna maharage.

(c)    Kukaa karibu na bank na uku ukitegemea kuna siku hela zitatoka bank na kuja nyumbani kwako.

(d)   Kuimba mwenyewe chumbani kwako ukafikiri uko studio na kutega sikio au kutazamia nyimbo yako itapigwa radioni.

(e)    Kukaa na sehemu wanaopika chakula kizuri na ukategemea kupitia harufu yake utashiba hata bila ya kukiweka mdomoni.

Kuna maisha unaweza kuishi nje ya utaratibu wa kimungu endapo tu kama hauta kuwa makini na majira.

Wapo watu wamekatisha maisha yao kwa kukosa kuyaelewa majira yao vizuri katika majira ya kuvumilia wenyewe walifikiri ni majira ya kupata hivyo kwa kushindwa kuvumilia walipoteza maisha yao.

Ni muhimu kutambua majira maana ni ramani ya Mungu kwa maisha ya mtu binafsi, kwa kuwa majira yako ya kunyamaza yanawezekana kuwa ni majira ya mwingine kusema.

Unapokosea kuielewa ramani unaweza ukajikuta upo kariakoo badala ya kuwa America!

Moja ya sifa ya mtu anayetambua majira yake kiufasaha hawezi kuweka kinyongo au kisasi na mtu au watu bali furaha ya Mungu ina ushika moyo wake.

Yusufu “ sio ninyi mlionileta hapa “!

Mwanzo 45:1 Hapo Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze.

 2 Akapaza sauti yake akalia, nao Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia.

 3 Yusufu akawaambia ndugu zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake hawakuweza kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake.

 4 Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri.

 5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watu.

Niseme tu unapoamua kutembea katika majira sahihi tegemea kupingwa/kutotiwa moyo na hata kunenewa maneno mabaya na magumu kwakuwa majira yako anayoyaelewa ni Mungu tu na wala sio jirani wala rafiki hama mzazi au mchungaji.

Unahitaji kusimamia majira yako vizuri ili uweze kumpendeza Mungu zaidi ya kufurahisha majirani/watu kwa kitambo kidogo baadae wakakusahau.

Na uzuri wa kitu sio kuwa nacho tu bali ni kuhakikisha umekielewa, hivyo unaweza kuwa huru  katika kukitumia vizuri.

Moja ya kitu kitakachoweza kuondoa vikwazo katika jambo lolote utakalolifanya ni kuelewa majira yako, kuwa wakati huu natakiwa ufanye nini na nisifanye nini hapo utafika kwa haraka na kwa wepesi.

Majira wakati mwingine yanaweza kukupelekea kuchukua maamuzi ambayo yatahatarisha maisha yako kwa kiasi kikubwa kwa kuwa ni ramani inayoonyesha upitie hapo ili ufikie kwenye utukufu mwingine.

  Ni muhimu kujua uliko ili ujue unako kwenda “

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………………….0764 018535