Kadili unavyodumu
katika maongozi yake ndivyo hivyo ubora wako unavyo thibitika!
Ubora ni uhitaji wa
dunia!
Ø Makazini
( jeshini, bandarini, viwandani na mashuleni )
Ø kanisani
Ø mwenza
Hata mbingu inataka mtu
aliye bora!
Ndo maana ukienda
kuomba kazi basi wata mwitaji mtu aliye bora na sio mtu anayefanya kazi tu bali
kazi yenye viwango ( ueledi na bidii ) ili wapate tija katika biashara zao, ndo
mana utoa vigezo ukifuatilia kwa umakini vigezo hivyo utajua hapo utafutwa mtu
aliyebeba ubora na sio ubusy usio na tija katika shughuli zao.
Boss urelax pindi
anapompata mtu ambaye anafanya kazi katika ubora anakuwa na imani naye pasipo
mashaka kazi itaenda na faida itapatikana.
Naam…………hivyo
tunakubaliana kuwa ubora ni chaguo la watu wenye akili, sababu ziko nyingi kwa
nini mwenye akili achague kilichobora lakini hizi mbili zinaweza kutupa mwanga,
i.
Tija
Kitu
chochote kilicho bora uwa kinakuwa na ufanisi mkubwa katika utendaji wake, uwa
akisumbuisumbui mara kwa mara.
ii.
Kina dumu
Unaweza
kukitumia kwa muda mrefu mpaka ukasahau kama kunakifaa umekiweka kwa sababu
kina uimara hivyo utatumia muda mrefu kifaa au mashine yako kwakuwa umeweka
kifaa chenye ubora.
Muhimu
ni kutambua kuwa ni Mungu ndiye anayekutengeneza ili uwe bora na ufae katika
jamii, pia unaweza kupitia mikono ya watumishi na ukawa bora.
Kuwa bora sio kitu
rahisi japo kinawezekana kwa kuwa mwezeshaji yupo anasubiri utayari wako ili
akutengeneze uwe kiumbe cha ajabu.
Ni vizuri ujue endapo
usipokubali maongozi yake unaweza kufahamika sana lakini usiwe bora.
Naam ubora sio mtelezo
bali ni matokeo ya kukabiliana na mambo yanayoweza kutingisha imani.
Matendo 21:13 (10-13)………………….
10 Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake
Agabo akashuka kutoka Uyahudi.
11
Alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono, akasema,
Roho Mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga
mtu mwenye mshipi huu, nao watamtia katika mikono ya watu wa Mataifa.
12 Basi
tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda
Yerusalemu.
13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo?
Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa
ajili ya jina lake Bwana Yesu.
“ Ndipo Paulo akajibu,
mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo?..............
Ni muhimu ujue Mungu
anakufanya bora kwa ajili ya utukufu na sio ulete shida katika jamii.
Ø Nitalijenga
kanisani langu na milango ya kuzima haitaishinda!
Naam ni kawaida tu, ili
uweze kupata moyo wa mtu kwa urahisi ni kukubali kuishi katika maongozi yake (
mzazi, boss,mme)- maneno yake.
Na kufanya mambo mengi
nje ya maelekezo/mwelekeo au dira yake ( Mungu ) ni kupoteza muda na kuuchosha
mwili.
Luka 10:40-42
40 Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi;
akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha
nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.
41 Bwana
akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu
vingi;
42 lakini
kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo
hataondolewa.
Endapo ukitaka kuona
mtu anaambatana na wewe siku zote au haukauki kinywani mwake ni kuishi kwa
kufuata maongozi yake.
Yohana 8:29
Naye
aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya
sikuzote yale yampendezayo.
Kwa namna
unavyojigharimu kuishi katika maongozi yake yeye atatengeneza maisha yako ili
yawe bora.
Namna unavyotoa macho
kuangalia mambo yake naye ndio anavyotoa jicho lake kuangalia maisha yako.
Kuishi katika maongozi
ya Mungu kunahitaji MAAMUZI BINAFSI!
Joshua 24:15
Nanyi kama
mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni
miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya
wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu
tutamtumikia Bwana.
“…………….chagueni hivi
leo mtakaye mtumikia;
Hakuna
ushoga/ubest/urafiki katika hili.
NAWEZAJE KUISHI KATIKA
MAONGOZI YAKE:
Mbali ya kuwa na
kiu/shauku juu ya Mungu pia kuna maarifa unatakiwa uwe nayo.
i.
Ipende hatma yako
mbali na kuiombea hatma
yako na kufanya mambo mengine lakini usisahau kuwa hiyo hatma inavumbuliwa
katika kuishi ndani ya maongozi ya Mungu.
Wagalatia
1:16
alipoona
vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake;
mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu;
“ alipoona vema kumdhihirisha mwanawe ndani
yangu,…………………….”
Hatma ni jambo/kitu alichokiweka
na Mungu ndani yako ( ramani ya Mungu inayoongoza maisha yako ) ili dunia iwe
salama na dunia haiwezi kuwa salama nje maongozi yake.
Usipojua njia/mwelekeo
utapotea/kupotezwa na watu wasio na nia njema kwako au walio na maslahi yao.
ii.
Tamani kuona jicho la Mungu
linakufurahia.
Jicho la Mungu pindi
linapokutazama linaweza kuwa sura mbili kukufurahia au kukuhuzunikia, tamani
kufanyika kicheko cha Mungu na atamani kukuona wakati wote.
Hapa duniani jitahidi
sana kuishi maisha yatakayoleta furaha katika macho ya Mungu na sio kwa
wanadamu.
Mathayo
10:32-33
32 Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele
za Baba yangu aliye mbinguni.
33 Bali mtu
ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye
mbinguni.
Pindi Mungu anapotupia
jicho kwako au kukuangalia aseme kweli ana mtoto anayejigharimu kuishi kwa
ajili yake,
Na kufurahisha jicho la
Mungu lazima uwe tayari kwa gharama:
a)
Matakwa binafsi kupoteza/kukiondoa
kipaumbele chako.
I wafalme 17:10-13,9
9 Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama,
nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe.
10 Basi, akaondoka,
akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako
akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni
nipate kunywa.
11 Alipokuwa
akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi
mwako.
12 Naye
akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika
pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie
nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.
13 Eliya
akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza
mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao.
MJANE:
Ø Konzi
ya unga katika pipa
Ø Mafuta
kidogo katika chupa
Mjane “ tuule tukafe”
Katika hali hiyo yote
mjane aliweza kujitoa mwanga maisha, kwakutoa nafasi ya kwanza kwa mtumishi wa
Mungu baadae ajiweke yeye!
Ukimweka Mungu mbele
naye anakuweka mbele.
b)
Kutokuwa kipenzi cha watu
Unaweza kuwa kwa ajili
ya kusaidia jamii husika lakini hao hao wasikupokee au kukubali.
Yohana 1:11
Alikuja
kwake, wala walio wake hawakumpokea.
“ alikuja kwake, walio
wake hawakumpokea”
Ni muhimu kujua kuwa
uwa kusudi ni lazima litimie haijalishi wamekupokea au hawajakupokea.
Kusudi linajitosheleza
lenyewe alihitaji msaada mwingine wowote.
Yohana 11:8
Wale
wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga
kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?
“ wale wanafunzi
wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu wayahudi walikuwa wanakutafuta……………”
Unaweza kuhatarisha
maisha yako ili wengine wawe salama.
iii.
Epuka mazoea
Kila mtu ana ramani
yake katika kuishi katika maongozi ya Mungu akiwepo hapa duniani.
Mungu uwa hana nafasi
ya mbadala vile alivyo ndivyo anakuwa wala sio mjomba au bibi yake ili amtanie.
Ni muhimu ujue pindi
utakapoanza kuishi kwa mazoea hapo ndipo utakapo punguza penzi lako kwake. (
ushirika )!
NDOA: Moja ya sababu
inayopelekea ndoa kuvunjika kumzoea mwenzi hivyo kufanya jambo pasipo kujali
nini kitatokea au atajisikiaje ( kutojali hisia za mwenzako ).
Mazoea pia ndio mwanzo
wa kupoteza njia unayotakiwa kuendea.
KIBURI NA UJUAJI ni
pacha wa mazoea, mathalani nishachoka na mahubiri ngoja mwezi huu ni pumzike nyumbani
kidogo nione nitapungukiwa na nini.
INAITWA SIKU! BARIKIWA
SANA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson…………………………………………….. 0764 018535