Jumatatu, 27 Februari 2023

ASANTE YA SIKU!

 



Moja ya neno zuri ambalo watu wengi upenda kusikia na uwa mioyo ya watu uwa na bashasha na hata kupelekea  hamasa ya kufanya zaidi ni hili neno ASANTE! ( lililo na tafsiri ya maana ya shukrani ).

Ni wazi hili neno linahitajika litumike katika hali ya jambo husika pasipo kujali kuwa ni kubwa au dogo, kwa maana ule moyo utakao kuwa nao kushukuru katika jambo ambalo wewe binafsi unaliona dogo basi hiyo ndiyo ishara kuwa utamshukuru Mungu hata lile linaloonekana kubwa.

Mungu anapofanya jambo kwako uwa haoni kuwa ni kubwa au dogo bali yeye uona ni jambo jema akutendealo hivyo unapaswa kumshukuru kwa moyo wote ili liweke msingi mzuri kwa Mungu kufanya zaidi.

Katika jamii tuliyonayo tumejengewa kumshukuru Mungu au kusema ASANTE kwa Mungu hasa mwisho wa mwaka ( ukiamini amekulinda toka mwezi wa kwanza hadi mwezi wa kumi na mbili na kwa kutambua kuwa wewe hauna upekee sana kuliko watu waliotangulia ( kufariki )

Uwa kila kitu kinakuwa na maana pindi utakapo tambua maana! Usipotambua maana akitakuwa na maana, haijalishi kina thamani kubwa kiasi gani?

Siku uwa ni matokeo ya mambo yaliyofanyika na ndio kiashirio kikubwa cha wakati ujao hivyo ni kiini kikubwa katika maisha yako, hauhitaji uipuuzie kwa namna yoyote.

Ni muhimu kutambua kuwa siku ni fumbo maana kila saa linapopita uwa kuna mambo yanafanyika  yanaweza kuathiri maisha yako kwa namna moja au nyingine.

Siku ni jiko inapika cha jana ( kukitengeneza cha jana ) na kukiona kama kitafaa kuliwa ili kikufae kesho hama kuandaliwa kingine kama hicho akifai.

Ukweli siku moja imebeba maajabu makubwa wako watu wanaanza siku yao kwa furaha lakini baadae wanahitimisha kwa kilio, pia wako watu wanaanza siku yao kwa kilio lakini baadae wanahitimisha kwa tabasamu.

Siku inaweza kukatisha ndoto zako au kuendeleza!

Siku moja ni muhimu sana kwani wako watu wanafanya/wanafanyiwa jambo ambalo awakuwai kuliwaza au kutegemea kufanya mathalani wako watu wanabakwa na kuteswa katika siku na kubadilisha rangi ya siku yake pia wako watu wanachukua jukumu la kutoa uhai wa mtu japo hapo awali akuwai kuwaza wala kufikiria kufanya jambo kama hilo.

Ndomana ni muhimu sana kumshukuru Mungu kwa moyo wako wote haijalishi wengine wanaionaje hiyo siku lakini wewe uonyeshe thamani kwa Mungu kwa kukupa siku hiyo pasipo kujali kama ina utulivu au ina machafuko.

Usiwe na shukrani ya kina pindi utakapo nusulika na majanga makubwa yaliyoshtua moyo wako na kukupa tashwishwi  mathalani mtoto wako kaponea chupuchupu kudumbukia katika shimo la maji taka sasa hapo uishii tu kushukuru hadi sadaka ya shukrani itatolewa kwa kuwa hilo umeliona, pasipo kujua yapo mengi usiyoyaona na pengine yalikuwa na hatari kubwa kuliko hilo uliliona au yale unayaona.

Kumbuka siku ndio msingi wa wiki hatimaye mwezi na mwishoe ukamilisha mwaka, hivyo ukiweza kuitengeneza leo yako vizuri basi umeitengeneza mwaka wako vizuri.

Hivyo usidharau leo kwa sababu ni masaa machache tu na ukaipa thamani kubwa mwaka ( kana kwamba umejitengeneza wenyewe kumbe huo mwaka ni zao la siku ) maana una siku nyingi, ni muhimu kutambua sio kila mtu anapata neema ya kufunga mwaka japo inawezekana walikuwa na malengo yao ya kufika hapo na malengo kama sio mikakati kuweka kwa ajili ya kufunga mwaka, hivyo kila siku utakayoipata ni muhimu umshukuru Mungu maana ujui kesho inaweza kuwa sio siku yako.

Unahitaji kuiona siku kama lulu ambayo thamani imezidi chochote,shukrani ya dhati lazima ionekane kwa Mungu na kuitambua siku Mungu amekupa kwa ajili ya faida yake,

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………..…………0764 018535

Ijumaa, 10 Februari 2023

YAELEWE MAJIRA YAKO:

 



Majira kama vipindi mbalimbali vinavyotokea katika dunia na kukamilisha asili yake, na kwa kiasi kikubwa uchangia maisha ya binadamu kuendelea,

Naam katika dunia tunayoishi kuna majira mbalimbali mathalani majira ya joto,baridi na upepo mkali haya yote uonyesha fahari ya dunia katika asili yake.

Hakika kuna tofauti kubwa kati ya mtu anayeishi anayeelewa majira yake na yule asiyeelewa majira yake, kwa mtu anayeelewa majira uwa anajiandaa na hali ijayo anapojua majira ya baridi yanakaribia basi hapo uweza kuandaa mavazi ya aina fulani katika kukabili na hali hiyo mfano.nguo nzito….. ila kwa mtu asiyejua  hali ya hewa ijayo anaweza akaandaa nguo nzito wakati hali ya hewa ijayo ni ya joto.

Ni wazi unapoishi bila kujua majira yako basi hapo……………..!

“ wakati wa kucheka wewe utakuwa unalia na wakati wa kulia wewe utataka ucheke”

Kwa asilimia kubwa uwezi kuwa mtu mwenye ubora endapo tu ukiishi nje ya majira,

“ muda wa kufanya kazi utataka kulala na muda wa kulala utataka kufanya kazi”

Unapoishi nje ya majira mateso ( mwili na akili ) yana kuwa ni fungo lako.

Majira kwa asilimia kubwa uwa hayafanani inawezekana ni majira ya mwenzako kuvuna lakini ni majira yako kupanda tofauti na mwenzako hivyo usiwe na haraka.

Mhubiri 3:1-8

1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

 2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;

 3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

 4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

 5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

 6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

 7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

 8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.

 

Maisha ili yaende yanahitaji kufuata majira!

Dunia ili iende inahitaji kufuata majira yake! Kujizungusha kwenye muhimiri wake.

Mkulima ili aweze kulima na kuvuna mavuno yake kwa ajili ya kujikidhi yeye na familia pamoja na jamii yake basi hapo ni muhimu azingatie majira ya kupanda ili aweze kuvuna.

Ni muhimu kuyaelewa vizuri majira yako maana ni kwa faida yako na usipoyaelewa majira basi hapo ni kwa hasara yako, maana hata mkulima akilima nje ya msimu anaweza kupata kidogo mavuno yake au asipate kabisa.

DUNIA INATEMBEA KATIKA MAJIRA YAKE!

a)      Kilimo

Kilimo kinapande mbili kuu: kupanda na kuvuna!, ili uweze kuwa mkulima mwenye tija ni lazima ujue ni majira gani unapaswa kulima hama kupanda ili yakija majira ya kuvuna uweze kuvuna,

Naam kila mazao yana msimu wake ( maembe, machungwa, mananasi n.k ) hivyo ukitaka kufaidi vizuri basi hapo ni muhimu utembee katika msimu wake ili usichangaye mambo.

Wingi na ubora wa mazao yako unategemea vitu vingi mathalani unalima kwa kutumia teknolojia ipi ( kisasa au zamani ), ubora wa mbegu,unalitunzaje hilo shamba ( umwagiliaji,kuweka dawa na mbolea) kila kitu inabidi ifanyike kwa wakati wake pamoja na usimamizi ulioutumia kutoka hatua awali, kuvuna na hata ya mauzo ( faida/hasara ).

b)      Uchumi

Matukio yoyote yanatokea duniani yana mchango mkubwa katika kukuza uchumi au kuharibu uchumi mathalani magonjwa ( CORONA-COVID 19 ), Vita ( urusi dhidi ya ukrain ) na vitu vingine vingi vimechangia uchumi kudorora japo na siasa imejificha ndani yake.

Uchumi unasema bidhaa inapoadimika sokoni basi gharama yake inapanda! ( moja ya kanuni )

Ni muhimu kuelewa mambo ya dunia yanavyoendelea kwa maana baadhi ya matendo yanahusiana na biblia inavyosema.

MBINGU INATEMBEA KATIKA MAJIRA YAKE!

Ili kuyaelewa haya majira kuna vitu viwili vya msingi:

Ø  NENO LA MUNGU (  MSINGI )

Ø  ROHO MTAKATIFU ( MTEMBEO )

Ukiweza kuvielewa vizuri hivi vitu basi hapo utakuwa umeinasa network vizuri kama bar basi zote hapo zimesimama vizuri tayari kwa kupokea mawimbi kwa ukamilifu.

Ni kweli usiopingika wakati mwingine majira ya dunia yanakidhana na majira ya mbingu japo sio mara zote ni kwa kusudi maalum.

Mfano; unapokuwa mwanafunzi alafu usitie jitihada katika masomo yako hivyo ukafanya mitihani na matokeo yakatokea mabaya, usianze kumlaumu shetani na kusema shetani amejiinua dhidi ya elimu yako.

Nilipata nafasi ya kusoma na kiongozi wangu wa fellowship nilipokuwa kidato cha sita alikuwa na jitihada sana katika kazi ya Mungu lakini matokeo ya mwisho yakatoka na kupata division 0,

Hivyo niseme kuwa sio kila kufail ni mapito , mengine ni kutotumia nafasi nzuri uliyopata kwa kuwa kila jambo lina wakati wake japo katika mazingira yoyote neema bado ipo.

NAJUAJE KAMA NATEMBEA KATIKA MAJIRA YA MBINGU:

I.                   AMANI YA KUDUMU

Hata mambo yakikusumbua au kukutingisha ile amani ipitayo ufahamu inakuja kukufunika na kukupa kuendelea mbele.

Wafilipi 4:7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Waamuzi 6:23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.

Ayubu 22:21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.

Yohana 14:27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

 

II.                MNG’AO WA KIMUNGU

Ni kweli mnapitia katika majira ambayo sio sahihi/mazuri inawezekana kuna ukata wewe hivyo mng’ao wa dunia unapoishia basi hapo mng’ao wa kimbingu unachipua.

Ukitegemea  pekee yake dunia icheke ili nawe ucheke basi dunia inapoishia hapo nawe utakuwa umeishia.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………………………..0764 018535