Kumtegemea Mungu imekuwa fumbo la maisha ya watu wengi: imekuwa kila mtu upenda kusema anamtegemea Mungu pasipo kujua nini hasa ana maanisha!
Waendao katika nyumba za ibada na wasioenda wote wanasema wanamtegemea Mungu kwa maana Mungu ni mmoja, pia waliookoka na wasio okoka wote wanasema wana mtegemea Mungu.
Hivyo neno hili limekuwa ni la kawaida sana kulisikia kwa mtu, japo wakati mwingine unapolitamka katika mazingira yanayotegemewa kusikiwa hili neno uweza kuonekana kuwa ni mtu mwenye busara.
Hivyo neno hili kumtegemea Mungu limekuwa likitumika kwa watu wote na asilimia kubwa hata awe ameokoka au mwislam wote wanasema neno hili.
Kumtegemea Mungu ni zaidi ya mtoto mdogo kuwa tegemea kwa wazazi wake au mfanyakazi kutegemea mshahara hama mkulima kutegemea mavuno yake ili aishi.
Wengi wao wanasema pasipo kujua hasa maana ya kumtegemea Mungu kwa uhakika, wengine wanasema kwa sababu awamuoni na wanamuogopa, pia kuna jehanam na yeye ndiye muamuzi wa mwisho, hivyo wanadhani kwa kusema hivyo wanaweza kumshawishi Mungu kuiona pepo/kuikwepa jehanamu.
Mathalani unaweza kukuta watu wamekaa wanajadili mambo mbalimbali yawe magumu au mepesi, pale wanapofikia akili zao kutokuwa na majibu ya uhakika basi hapo neno kumtegemea Mungu lina kuwa na maana sana, kwahiyo kumtegemea Mungu inakuja pale akili zao zimefika mwisho kwa maana hiyo kama akili zao zisingefika mwisho wasingeona umuhimu wa kumtegemea Mungu.
Ukweli katika hali ya kumtegemea Mungu kuna mawanda mapana sana, wako wengi hawana uhakika kwamba wanamtumaini/kumtegemea Mungu na wengine wanahisi kuwa wana mtegemea Mungu na wengine uwa wanaambiwa tu ila wenyewe hawajui “ kweli wewe unamtegemea Mungu maana alipokuwepusha pale”
Warumi 8:16…. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
Japo Mungu ndio pekee hajuaye nani amtegemeaye yeye lakini kwa mtu anayemtegemea Mungu Roho mtakatifu umshuhudia toka ndani yake,
Moja ya faida ya kumtegemea Mungu ni hali ya Mungu kukupa uwezesho/kukutegemeza zaidi juu ya dunia tuliyonayo ili tuweze kuyashinda yote kwa njia zake.
Kumtegemea sio swala la tukio gani lililo kukuta bali ni hali ya kukua katika ushirika na Mungu na huku ukitambua pasipo yeye wewe hauna maisha.
Kumtegemea Mungu lazima ukue katika ufahamu wake ongezeko la nguvu ya ndani yako ikupayo kushinda katika yote yanayokuzunguka.
Kumtegemea Mungu haya maisha yaliyo ambatana na furaha, amani, na utulivu ulio katika ukamilifu.
Ni mumhimu kutambua kuwa hauwezi kumtegemea Mungu katika misimu fulani tu baada ya msimu huo hakuna kinachoendelea tena, usimtegemee Mungu katika majira/msimu ambao unaona wewe, Mungu haitaji kuwa mtatuzi wa shida zako tu bali anataka usalama wote wa maisha yako uwe mikononi mwake, uwe chini ya maongozi yake.
Kuna faida kubwa hapa duniani ukitambua siri iliyopo katika maisha ya kumtegemea Mungu, ujasiri juu ya Mungu unakuwa mkubwa sana na unakuwa unajua kile unachokiamini hivyo kufanya wepesi katika kumdhihirisha katika mazingira yako.
Mungu uwa anatambua nani anamtegemea yeye na nani ni anaigiza kumtegemea yeye, kwa yule kweli ambaye Mungu anajua anamtegemea uwa hawezi kushindwa kujidhihirisha kwake.
Usibweteke pindi ukawa unahisi tu unamtegemea Mungu na ikatokea bahati mambo yakaenda sawa ukafikiri sasa wewe unamtegemea Mungu, sio kweli kwani wako watu ambao hawana fikra ya kumtegemea Mungu lakini mambo yao kuna wakati yanaenda sawa.
Unahitaji Roho mtakatifu akushuhudie kama unamtegemea Mungu na mtu anayemtegemea Mungu uwa hanamashindano ila uweza kuisimamia haki yake.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson………………………………………………………..0764 018535