Moja swali linaweza kujibika kwa urahisi ni hili;
i) ushawai kumwekea Mungu mipaka?
Jibu:
- Nawezaje mimi kumwekea Mungu mipaka wakati ni yeye aliyeniumba na mimi ni kazi ya mikono yake, kwa maana hiyo Mungu ndio mwenye uwezo wakiniwekea mipaka na wala sio mimi kumwekea Mungu mipaka.
Hili swali ukimuuliza mtu yeyote anayeenda kanisani atakujibu pasipo mashaka yoyote:
i) Mungu hana mipaka katika utendaji wake?
- Bila shaka atajibu huyo ni Mungu hakuna kitu kilicho zaidi yake hivyo yeye ndio mwisho hakuna mwingine wala badala yake hatatokea.
ii) Ufahamu wako haujamwekea Mungu mipaka?
- Naam bila shaka anaweza kujibu Mungu anaweza sana naanzaje kumwekea mipaka katika ufahamu wangu mdogo, Mungu ni mkubwa sana hawezi kutosha katika ufahamu wangu.
NI KWELI HATUMWEKEI MUNGU MIPAKA?
Sasa karibu tuingie katika kiini cha somo:
a) Mathalani tarehe za kodi zinapokaribia kuisha na uhakika wa kupata kodi haupo hapo ufahamu wako utaweza kumuona Mungu anaweza!…………..kukupa maji jangwani!
b) Umri unakwenda na uoni mwenzi wa kukuoa au kumuoa bado ufahamu wako utaona Mungu anaweza kukupa mpenzi hata uzeeni!……………………wakati ambao akili yako hawezi kutarajia?
c) Miaka inazidi katika ndoa bila mtoto na wakwe wameanza kuamia hapo na vikao vimeanza kujadili swala kwanini upati mtoto je! Bado ufahamu unaweza kumuona Mungu ni mkubwa na anaweza kukufuta machozi yako kama sio yenu kwa wakati aliopanga?
d) Inawezekana unapata ujauzito mara nyingi lakini inaharibika umejaribu kwenda hospitali mbalimbali pamoja na miti shamba ya kutosha hakuna msaada wala tumaini hata hapo bado ufahamu wako utaona uweza wa Mungu na kukutoa pale ulipo?
Ni kweli ukitaka kuona utendaji wa Mungu mkamilifu unahitaji kuishi katika ufahamu wake na sio ufahamu wako.
Unahitaji kujua unapaswa kujua umezaliwa na umekusudiwa katika Mungu na sio mpango wako hivyo unahitaji kuishi katika ufahamu wake ili umwelewe yeye katika akili yake/mawanda yake ili uweze kuishi vile unavyopaswa sawa na utajiri wake.
Moja ya kitu kitachokusaidia kutomwekea Mungu mipaka ni kutoishi katika hisia zako, usiwe kama muota ndoto za uwoga anaogopa kulala japo anataka kulala hivyo anakuwa katikati pasipo kujua nini cha kufanya.
Hama mtu na mpenzi wake pindi inapotokea tofauti kidogo maswali mengi uweza kutokea mathalani kachelewa kurudi au ajapokea simu kwa wakati, unaweza kuhisi mambo mengi labda ameshaanza dharau au kuna mtu mwingine ameanza kumwelewa vizuri kuliko wewe!
Unapoamua kuingia kwa Mungu hakikisha hauishi katika fahamu zako bali ziruhusu akili za Mungu ziishi ndani ya ufahamu zako na endapo kutakuwa na jambo baya linalotaka kukufikia Mungu atalifunua mapema sio kutembea katika kuhisi hisi tu.
Na unapoamua kuingiza ufahamu wa Mungu katika akili zako ni lazima usome neno la Mungu kwa bidii na uruhusu uhai wake na nafasi yake katika ufahamu wako na kudhihirika katika maisha yako.
Mungu anataka aishi yeye kupitia wewe ili yeye ayaweze mazingira yote yanayo kuzunguka maana yeye anayajua yote na hakuna kitu kigeni kwake ndo maana anatuita sisi kuwa ni mabalozi wake kwa maana inabidi tufanye ya kwake na yeye atafanya ya kwetu kwa kuwa yeye ufanya kupitia sisi.
Watu wanaona ubora wako kupitia utendaji wa ufahamu wako, ufahamu ukiwa bora nawe unakuwa bora kwa kuwa ni yeye anakufanya kuwa bora kupitia ufahamu wake uliondani yako.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………..………………………………………..0764 018535