Ijumaa, 12 Mei 2023

UNAPENDA NINI HASA ZAIDI?

 



Ni kweli unaweza sema unapenda kula, lakini kipo chakula ambacho ukila unasikia burudiko ndani ya moyo wako maana unakipenda zaidi!

Naam, unaweza sema unapenda sana michezo lakini uko mchezo unaopenda sana, na sababu unaweza ukawa unayo moyoni mwako!

Pia unaweza sema natafuta msichana wa kumuoa, bila shaka utakuwa umaanishi ili mradi ni msichana tu bali huyo msichana kuna namna yupo, ambayo ukimuona tu moyo wako unafunguka wenyewe bila kufunguliwa!

Vilevile unaweza sema uwa unasema napenda kijana wa kiume wakunioa na hapo utakuwa umeshamtengeneza handsome wako katika akili yako na pindi picha ya kichwani ikagongana na mtu wa nje, unaweza kujikuta miguu inakuwa mizito kwenda mbele japo moyo wako unakusukuma uendelee tu kutulia na huku akili ikiwa katika bumbuazi!

Na vilevile unaweza kuwa mpenzi wa magari, lakini yako aina ya magari unayoyapendelea sana na pindi ukiyapata basi hapo sasa unaona au unajiona unaendesha gari la ndoto yako, na kupata raha isiyo ya kifani ndani yako.

Naaaam hiyo inaitwa……………..Nguvu ya uchaguzi/upekee wako!

Karibu katika somo!

Unaweza sema unapenda kazi fulani maana ukiipata unaifurahia sana, lakini ni vizuri kujiuliza kitu gani kina kuvutia hasa hata ujumuishe na kusema kazi hile/ hii naipenda sana.

Unapoweza kujibu swala hili kiufasaha, ndilo litakupelekea kudumu hapo au kuwa hapo kwa muda mfupi, mathalani unaweza sema napenda sana kazi ya upolisi labda utrafic kwakuwa unaona pindi utakapo kuwa barabarani elfu tano ( 5,000 ) au elfu kumu ( 10,000 ) hautaweza kukosa, hiyo ni mbali na posho na mshahara na maisha yako ya kasonga kwa wepesi.

Pia, unaweza jikuta unapenda sana kuwa wakili (mwanasheria) lakini hapo unaweza ukawa unalenga upataji wa hela kwa urahisi kwa kiasi kikubwa kutoka kwa waalifu au wasiojua sheria na waoga ili uwafichie maovu yao ili maisha yako yaende, pasipo kujali maumivu ya mwingine, na inawezekana kabisa kuwa mwanzoni ukuipenda kazi hiyo kwa lengo hilo lakini ukakutana na mfumo uliopo pale, na tamaa yako ikavutiwa zaidi ya vitu visivyo sawa, hatimaye ukabadilika.

Mbali na hayo pia unaweza kuta mtu anapenda sana aina fulani ya nyumba lakini inawezekana ni  kuonyesha na ufahari au pesa alizonazo tu.

NOTE; tunaweza sema haya yote ni maisha na kila mtu anapaswa kuishi sawa na aonavyo au awezavyo japo ni muhimu kuzingatia kutokua kero kwa mtu mwingine isiyo na sababu ya msingi.

Tuendelee kidogo………………..

Tukianza kusema na neno KUPENDA kwa tafsiri nyepesi tunasema ni matokeo ya macho kuona au masikio kusikia na kupata nafasi katika akili yako na huku ukiruhusu moyo kuzalisha shauku ya kupata hicho kitu kwa gharama au namna yoyote.

Nakubaliana sana, hasa katika ulimwengu wa sasa msemo unaosema “ easy come easy go” sio kwa watu wote ila kwa kiasi kikubwa huu msemo umebeba uhalisia katika jamii tuliyonayo.

Nakubaliana kabisa kuna raha inazaliwa ndani ya moyo wa mtu pindi anapotambua anapendwa sana na mtu anayependwa uwa hata mwendo wake unaweza badilika, naam hata kupelekea maisha kubadilika kabisa.

NAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAM!

Swali: Ni kweli unampenda mpenzi wako lakini nini hasa kinachosababisha umpende zaidi?

n  Bila shaka hili ni swali linalojibiwa na moyo tu, na mara chache sana ukute limejibiwa na kinywa katika ufasaha/ uhalisia wake.

Kwa kuwa ni jibu lililobeba uhalisia wa hilo penzi.

Napenda kusema swala sio kupenda tu, kwakuwa hata simba wanapendana na kuzaa na baadae wanaweza kula vitoto vyao.

Jambo kubwa ni nini hasa cha zaidi kinachokufanya umpende maana huo ndio msingi wa penzi lenu katika kudumu au kuwa la muda;

-          Unampenda kwa sababu:

a)      Mnaendana,

Pindi mnapo tembea pamoja unaona mfanano katika mwingiliano mzuri wa kimapenzi/mahaba.

Mnakuwa mapacha kwa muda! Pindi mnapotembea………………….!

b)      Unampenda/ unataka mzae watoto wazuri walio na ndoto katika maisha yako.

-          Wako watu wanapenda kuwa na watoto walio chotora wa kiindi, kijerumani, india, Kinyarwanda n.k hivyo utafuta mtu wa namna hiyo sawa na matarajio yake.

-          Pia inawezekana katika upande wa nywele, rangi yake n.k

 

c)      Ukiwa naye matatizo yako na familia yako yatakuwa yamekwisha, zile kero ndogo ndogo zitakoma kabisa.

 

d)     Ukweli huna sababu yoyote ila moyo wako umemuelewa ( umekufa ), ukimuona huyo mtu moyo wako hautulii kabisa unatamani usimame bado unaiona haitoshi unatamani ukae unaona unachelewa na ukiamua kukimbia unaona kama unawai.

Ukweli ziko sababu nyingi zilizo na msingi kwa huyu na kwa mwingine sio za msingi bado zinabaki kuwa ni sababu tu!

Pia ziko sababu nyingi nzuri kuliko hata hizo zinazofanya umpende mtu zaidi,

Katika dunia ya sasa propaganda ( maneno matamu ) ya mwanzoni uwa sio kitu kwa sasa japo anaweza kukusikiliza tu, kwani kuna watu wanauzoefu ( experience ) zaidi ya miaka ya thelathini ( 30 ) hivyo maneno yako sio kitu kwake, ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa ukitaka acheze.

Mapenzi ni kitu kizuri sana ila kinahitaji sana uhalisia wa moyo pamoja na kuruhusu moyo wako utulie hapo.

Ndo maana kwenye mapenzi yenye mwingiliano wa kweli tunaona maendeleo makubwa yakifanyika kutoka hapo, lakini pia tumeshuhudia mateso mengi, talaka hata vifo kutoka katika hali inayosemekana chanzo chake ni mapenzi ( mapenzi yasiyo salama )!

Mapenzi:

i)                    Hayahitaji ushawishi wa mtu/watu ( ndugu, wazazi au marafiki )

-          Wanaweza kukushauri tu lakini kukushurutisha uwe upande fulani au akuchagulie mpenzi lakini maamuzi hilo ni jukumu lako,

ii)                  Yana mwihitaji Mungu, yeye aliyeweka hali ya uhitaji wa ndani yako yeye anajua namna ya kukamilisha huo uhitaji.

iii)                Unahitaji kuelewa ndoa katika hali ya nje na ya ndani, sio kitu kidogo bali ni jambo kubwa linaloweza kuleta usaidizi kuishi katika ndoto zako.

NI HAKI YAKO KUSOMA PIA NI FAIDA YAKO KUAMUA!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………………….……….0764 018535

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni