Alhamisi, 21 Septemba 2023

KUMTEGEMEA MUNGU ILI AKUTEGEMEZE!



Ni kweli kabisa unaweza penda sana na kujisikia fahari pale unaposikia neno hili kumtegemea Mungu, kama ngao katika maisha yako………maana hata dunia inatambua ukiweka tumaini kwa Mungu basi maisha yako, yako salama!

Naam ni kweli unaweza kutokuwa halisi katika mambo mengi na watu wasikugundue/kutambua mathalani unaweza ukawa na njaa lakini ukataka watu waamini kuwa umeshiba na watu wakaamini hivyo kwa urahisi kabisa.

Pia unaweza kuwa katika hali mbaya inayoleta au sababisha maumivu katika moyo wako lakini unaweza kujitahidi kuficha huo ukweli usijulikane badala yake ukataka watu wakuone kuwa mwenye furaha isiyo na kifani na kicheko ndio maisha yako…….unaweza ita ni hekima! Sawa.

Lakini twende mbele na kurudi nyuma mtu anayemtegemea Mungu ujue ukimuona huyo ujue umemuona Mungu mwenyewe naam na ni Mungu anaishi kupitia yeye, maana unakuwa ni muunganiko unaozalisha kitu kimoja.

Kwa uhalisia mbele za Mungu uwezi kuonyesha kuwa unamtegemea Mungu na huku haumtegemei yeye ni seme tu udhihirisho wa mtu anayemtegemea Mungu sio swala la kuhisi au kukisikia bali ni kishindo chenye uvivuo wa nguvu za Mungu,

Uwa hatusemi sisi kuwa tuna mtegemea Mungu bali udhihirisho wake ndio utaonyesha kuwa tunamtegemea na sisi kuwa watu wake.

Mambo mengi yanayoendelea katika dunia ya leo kwa asilimia kubwa yanachangia kuondoa uhalisia wa kumtegemea Mungu badala yake kuna na namna ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia uliopo.

Mathalani watu uweza kutoa ongo katika kupata kazi au haki yake na baadae kuona ni Mungu amefanya, watu uweza kusababisha fitina kati ya bosi na mfanyakazi au mtu na mchumba/mke wake ili mradi huyo atoke na aingie yeye…..wakibebwa na kauli ambayo haipo kwenye biblia kuwa” jisaidie nami nitakusaidia”

Ukweli kwamba kumtegemea Mungu sio kujua kuhubiri au kuweza kufungua watu japo hayo yanaweza kuwa ni udhihirisho mdogo wa kumtegemea Mungu, kwani unaweza fanya yote lakini bado usimtegemee Mungu.

Ni vizuri kutambua kuwa Mungu atafuti watunzaji wa zuri wa biblia au waaminifu katika kuudhuria vipindi kanisani bali wanaomtegemea yeye wanao muonyesha kama alivyo katika jamii hata ulimwengu wote katika uweza na nguvu zake.

Unapoishi maisha ya kumtegemea Mungu unakuwa na maisha ambayo yanakufanya kuwa wewe ni kioo kiasi kwamba watu wakikuangalia wewe wanaona utendaji mkamilifu wa Mungu.

Kitu kikubwa kitakacho dhihiirisha kuwa wewe unamtegemea Mungu ni hile hali kamilifu ya kukubali GHARAMA ya kumsikia na kuishi humo ( utii ) kama hakuna utii wa kujidhabihu hapo haiwezekani kumtegemea Mungu.

Kumtegemea Mungu ni kuishi anavyotaka sio kama unavyotaka, kuishi katika sauti yake pasipo kuangalia kushoto au kulia,

Mwanzo 22:12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

Kumtegemea Mungu sio kama dunia inavyoenda/inavyo amini bali neno la Mungu linavyosema na hapa pamekuwa ni tanzi kubwa kwa waliokoka.

Kujiingiza katika ubazilifu wa dunia ( Rushwa ) bila kutoa rushwa hauwezi kupata haki yako.

Hivyo mtu uweza kutoa rushwa na baada ya kupata hicho kitu kwa njia zake na sio za Mungu ukaenda kutoa shukrani kanisani.

Mtegemee Mungu ili akutegemeze!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………….0764 018535

 

Ijumaa, 8 Septemba 2023

GHARAMA YA MSINGI

 



Msingi kama kitu muhimu na cha kwanza cha kufanya/kuzingatia kabla ujafanya jambo lolote……..mathalani unapotaka kufanya biashara lazima uhakikishe una msingi unaokidhi hio biashara naam  unapotaka kujenga nyumba lazima kwanza uanze na ujenzi wa msingi.

Katika ulimwengu wa kuzaliwa………kuna furaha ya kuwa wa kwanza pia kuna gharama za kuwa wa kwanza maana wewe ndio unakuwa kioo cha kufuatwa na wengine.

Moja kilio cha watu wengi kama sio wazazi wote ni kuona mtoto wa kwanza akienda katika njia ambayo mzazi anajua hatakuwa na maisha bora/mazuri baadae…….maana mtoto wa kwanza ndio zao la kwanza la tumbo lake au anaitwa kifungua mimba muda wote wazazi wanatamani wamuone maana ni mtoto wa ujana wao.

Bila shaka ni mtoto pekee anayependwa pasipo kuangalia jinsia yake kwa wazazi wengi japo baadhi ya wazazi au jamii inaweza kutarajia kuwa mtoto wa kwanza msicha au mvulana kutokana na taratibu zake au matarajio yao.

Naam mtoto wa kwanza ni mtoto anayependwa na wazazi wake na kuwekewa matarajio makubwa sawasawa na uwezo walionao au wakati mwingine hata zaidi ya uwezo wao huku waki mwamini Mungu,

Baadhi ya familia mtoto wa kwanza anapozaliwa panaweza kutokea na mkesha usiopangwa na usingizi ukapaa pasipo kutarajia kwa furaha kuu inayotawala mioyoni mwao na umakini uliopitiliza.

Kwa asilimia kubwa inategemewa/inaaminika kuwa mtoto wa kwanza ndio mwangalizi wa wadogo zake na ndio mfano au mwelekeza njia na inawezekana kuwa ndio msimamizi mkuu wa mali za familia, hata katika upande wa urithi anaangaliwa kwa umaalumu wake,

Maana inaaminika kwa kiasi kikubwa yeye anawatambua wazazi wake wanapenda nini na nini hawapendi ( maana alishafundishwa ) hivyo inategemewa yeye kuwa mwalimu wa wadogo zake.

Japo anaweza kukua na ikatokea asiwe vile ambavyo wazazi walitegemea awe, japo ataendelea kuwa mtoto wa kwanza lakini baadhi ya majukumu atanyang’anywa hama kupunguziwa au kupatiwa msaidizi inategemea na uhakika wa wazazi juu ya huyo mtoto.

Karibu sana!

Kwa namna yoyote kitu kikubwa kinachoweza kuumiza kichwa ni namna gani nitaanza na je! Lile ninalolikusudia litakuwa kama ninavyokusudia au itakuwa tofauti.

Mara nyingi katika ujenzi wa nyumba ikitokea fundi ameweza kuset vizuri msingi katika viwango vyake basi kuendelea na ujenzi hilo swala linakuwa hana wasiwasi nalo japo umakini utahitajika kwa kile alichikianzisha ili kiiendelee vizuri zaidi.

Ni kweli kila kitu kina gharama lakini sio gharama ya msingi kuna gharama kubwa ambayo yesu aliingia ili atengeneze msingi wa uwokovu wetu nasi tuweze kuendelea vyema sawa na kusudi lake.

Ni rahisi kurekebisha kitu  kikarekebishika kuliko nyumba kubwa iliyojengwa katika msingi ulikosewa gharama yake inakuwa ni kubwa mathalani unapokuwa safarini pindi ukakosea mwelekeo katikati ya safari unaweza kubadilisha mwelekeo na kuanza upya, kuliko ukamalishe jambo fulani alafu ukagundua msingi umekosewa hivyo inabidi uharibu kila kitu ili uanze moja.

Hauhitaji kulaumu kwanini mchungwa huu umezaa machungwa machachu bali tafuta kujua mbegu yake ilikuwa ya namna gani maana vile mbegu ilivyo ndivyo matokeo yake yatakavyokuwa huna haja ya kulaumu mchungwa bali badilisha mbegu yake basi matokeo yatabadilika sawasawa na radha inayotokana na hiyo mbegu.

Mambo mengi yanapo wakuta watu katika siku za leo kwa asilimia kubwa yanatokana na misingi walio jengewa hapo nyuma au kujijengea wenyewe kwa kujua au kutokujua.

Kwasababu ili mtu abadilishwe ni lazima ubadilishe msingi ( chanzo ) au mfumo unaotawala maisha yake.

Na kwa maana rahisi pindi usipotambua misingi gani inayotawala maisha yako ni vigumu kutoka hapo hata kama wakikuombea kwa namna gani au kwa mtindo wowote maadamu hujui msingi unaoshikilia maisha yako ni ngumu kutoka hapo au kuwa salama katika mazingira hayo.

Unahitaji kufunuliwa na neno la Mungu katika kutambua msingi gani unaotawala maisha yako , na liruhusu neno la Mungu likague moyo wako pindi unaposoma ukiongozwa na Roho mtakatifu maana yeye anaweza kubomoa misingi isiyofaa na kuweka misingi yakewakati mwingine utumia watumishi wake kukuonyesha wapi umeshikiliwa lakini kazi ya ukombozi kamili ni Mungu mwenyewe.

Ni kweli kuna maisha unaweza ukaishi ukaona sawa unaishi kumbe kuna maisha uliyokusudiwa tangu kuumbwa kwa dunia na uwezi kuyaona na kuyaishi kwa kuwa msingi mbovu umeshikilia afya yako, uchumi wako, mahusiano yako na mengine yote.

Ni muhimu kutambua kwamba hatuishi kwasababu wengine wanaishi hivi au vile bali tunaishi kwa mpango kamili wa Mungu sawasawa na ahadi yake na sio tunavyohisi au tunavyojua.

Mungu ajakusudia uishi vyovyote bali katika misingi ya NENO LAKE!

Hili neno ndilo linakutambulisha na kukujuza kujua wapi kuko sawa na wapi hakuko sawa!

Wapi pa bomolewe na wapi pajengwe!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………….……………..0764 018535