Ø Kufanya kitu sio tatizo maana hayo ndio maisha lakini endapo ukaamua kufanya kitu kwa ajili ya mtu mwingine hilo linakuwa ni jambo lingine na lenye mtazamo mwingine likiambatana na mguso mwingine.
Ø Figo inaposhindwa kufanya katika viwango vyake na unapoenda hospitali kupata matibabu yake hilo ni jambo linalotarajiwa na watu wengi lakini endapo utaenda hospitali kwa ajili ya kutoa figo kwa ajili ya mtu mwingine ili aweze kuishi hilo ni jambo lingine lenye kuonyesha upendo wa namna yake. ( unahatarisha maisha yako kwa ajili ya mtu mwingine )!
Ø Naam…….Kitendo cha kulia kinawezekana kuwa ni jambo la kawaida kutokana na majira na matukio fulani yanayo mkumba mtu lakini inapotokea unalia kwa ajili ya mtu mwingine linakuwa ni swala lingine lenye mtazamo mwingine wenye thamani nyingine,
- Mathalani kumuona mtu analia unaweza kumpita tu au kutoa kauli ya pole kisha kuendelea na shughuli zako lakini pindi utakapojua kuwa analia kwa ajili yako hapo unaweza kuvuta subira na kutaka kuwa naye karibu hasa endapo kama hauta tambua kwanini anakulilia, kwakua utataka kujua kwanini ameamua kulia kwa ajili yako na wala sio mtu mwingine.
Ø Pia………Ni jambo la kawaida kumuona mtu ameshika jembe na kuelekea shambani hasa katika mazingira ya vijijini, wakati mwingine ana kwenda asubuhi sana akiwa amebeba kidumu cha maji na jembe pamoja na panga, anakwenda shambani huku akijua amemuacha mke na watoto wake hivyo amebeba majukumu mabegani mwake akiwa anawaza tu kule aendako na familia aliyoaicha nyumbani na wakati mwingine hata bila kujijali yeye mwenyewe bali wale wanao muhusu tu ( familia ) na wakati mwingine anarudi jioni sana akiwa amechoka sana akili, hisia na kimawazo pamoja na mwili lakini bado atawaza kesho kwenda tena.
Ø Vilevile unaweza kukuta mtu asubuhi na mapema tayari yuko barabarani akigombania magari/mabasi ya kwenda kwenye shughuli zake ( hasa maeneo ya mjini ) uwaacha jamii inayomzunguka na kumtegemea/kumuhitaji anaenda kutafuta kwa ajili yao, mvua na jua vyote vinaishia katika mwili wake lakini anakubali hali zote ili mtu mmoja awe salama hama jamii yake kwa ujumla iweze kukaa katika hali njema.
Naam!
- Hakuna raha unayoipata kama ukisikia au kujua kuwa haya yote mtu anayafanya ni kwa ajili yako tu na wala sio kwa mtu mwingine hama jamii yeyote, na wala sio kwa ajili yake! Amekubali adhalilike au aibike au pengine hata mwili wake kupata shida ili wewe uwe katika namna njema.
- Bila shaka hakuna mtu asiyependa kuwa na mtu wa namna hii, mtu mwenye kuhakikisha furaha yako haipungui/ huzuni inapita mbali na maisha yako bali utulivu na raha unakuwa matuo ndani yako.
- Naamini kama ungetambua mtu wa namna hiyo yupo duniani hata kama anaishi pembeni mwa dunia amini ungejipanga kwenda kukutana naye hata kama sio leo au kesho hama wakati muafaka ili siku ukikutana naye maisha yako uyaweke mikononi mwake kwa kuwa utajua maisha yako yatakuwa salama katika matunzo mema.
- Na ukweli huo ndio mtihani unawakumba wanadamu katika dunia ya leo….anapoona hapa ndipo barafu anashangaa moto umeanza kumchoma na anapofikiri hapa ni sehemu salama ya kupumzika anakuta majani yameanza kumuwasha mpaka inampelekea machafuko kutokea, mauaji na hata chuki iliyokithiri inakuwa katika mioyo ya watu, watu wanatembea huku mioyo yao inavuja damu kwa sababu uliye muamini hakuweza kudumu katika kuaminika.
- Uzuri ni kwamba yuko Mungu anayekujua na alishakujua kabla ujaja duniani na anajua kuwa ni nani yuko tayari kuibeba aibu yako na kukustili katika hali yoyote utakayo kuwa nayo.
- Kiukweli una muhitaji Mungu kwanza yeye ndiye anaweza kukutanisha na yeye aliyemkusudia ambaye atakuwa kimvuli salama kwako na sio jangwa.
- Bidii utakayoitumia katika kumtambua yeye naye atakutambulisha katika mtu atakayekamilisha ndoto yako na sio kuhiharibu.
INAITWA KESHO! BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………………………………..0764 018535