Zaburi 107:20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.
- Neno la Mungu lina uwezo kukutoa katika maangamizo yote endapo utalikubali na kulipa nafasi.
Kuna maisha uwa yanaanza pale mtu anapokombolewa, maisha ya kwenye vifungo hayana uhuru na amani timilifu.
Naam ukombozi ni jambo muhimu na baadhi ya wakristo wanaamini kufunguliwa kunakotokana na maombezi ( kwa kiasi kikubwa ) watu uamini hapo nami kwa kiasi kikubwa na kubaliana nao japo na amini ukombozi huu unaweza usiwe wa kudumu.
Lakini napenda kusema kufunguliwa kunakotokana na kumpenda Mungu uwa ni wakudumu kwa asilimia kubwa labda ukengeuke au kuiacha imani.
Uponyaji unaozaliwa katika kumpenda Mungu huu ni uponyaji unaoanza ndani yako ukiruhusiwa na ufahamu wako uliokubali mabadiliko hayo.
Huu uponyaji uwa unajijenga kwa ndani vizuri kabla ujaanza kudhihirika kwa nje na uwa ukipona unapona jumla ( sio ugonjwa wa kujirudiarudia ).
Kama ilivyokuwa uhitaji mkubwa kwa wanadamu ni kupendwa ndivyo ilivyo kwa Mungu haja yake kupendwa!
Na kama watu wanapopendana sana, uweza kupelekea kuishi pamoja, ndivyo hivyo ukimpenda Mungu uwa unaacha vyote na kuamia kwako jumla vile alivyo na vyote alivyonavyo anakuja na kukakaa kwako milele.
Kama unahitaji ufunguzi wa kweli na wakudumu unahitaji kumpenda Mungu kwelikweli, kwa kiwango kile unachompenda ndicho kiwango utaona mema yake katika maisha yako.
Unapompenda kwa kweli unafanya yeye kuwa jukumu la kuhakikisha maisha yako yako salama wakati wote.
Ni kama vile mtu anapougua utegemea dawa/ maelekezo ya daktari yanaseamje: wengine wataambiwa wameze dawa, na wengine kujichua n.k, pindi mgonjwa atakapopewa maelekezo ya kumeza dawa naye akaanza kutumia na baadae akaanza kuona unafuu katika mwili wake basi hizo dawa zimefanikiwa katika lile lengo lililokusudiwa endpo huo unafuu utakamilisha uzima mkamilifu.
Ndivyo ilivyo katika kusudi la Mungu kupitia neno lake unapolimeza/kulisoma linakwenda kupambana na vitu visivyosahihi kukaa ndani yako ikiwemo magonjwa ya kutupiwa/ya kawaida au tabia ngumu katika uwezo uliondani ya neno hakuna kitu kitabaki salama labda neno likose ushirikiano na wewe.
“ ukinipenda utalishika neno langu”
Yohana 14:23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
Unapoamua kulishika neno lake naye Mungu anashika maisha yako na kukufanya vile apendavyo yeye.
Kulishika neno kwa lugha nyepesi tunasema ni kulisikiliza vile linavyotaka na kuamua kufanya sawasawa na lilivyokukuagiza.
Ukiisha katika agizo lake hapo utaona utajiri wa neno ulizaidi ya duniani hata mbinguni.
Unahitaji kumpenda Mungu ili afanyike uzima na nguvu dhidi ya maradhi na uvamizi wowote wa giza.
“UKIMPENDA ATAKUPENDA”
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson……………………………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni