Alhamisi, 25 Julai 2024

MAAMUZI SAHIHI HUKUPA UKOMBOZI WA KWELI

 



Ni jambo linalojulikana kuwa kila tendo unalolifanya linaashiria maamuzi uliyoamua ndani yako, na hayo maamuzi yanaweza kuwa ni mabaya au mazuri, na hiyo hali udhihirika katika matokeo ya matendo yako kama yalikuwa mabaya basi  matokeo yake yatakuwa hasi…!

Maamuzi ni kitu ambacho mtu ukifanya karibia kila siku ambayo Mungu anampa uhai, maana nje ya uhai hakuna maamuzi yako binafsi bali unaamliwa na wengine ila unapokuwa na uhai unakuwa na uhuru wa kuamua nini ufanye na nini usifanye.

Ni ukweli kabisa kuwa unaweza kubadili maamuzi lakini sio rahisi kubadili matokeo ya maamuzi mathalani unapopata mawazo ya kuua na ukaamua kufanya hayo maamuzi pindi utakapo maliza hilo tukio la kuua bila shaka hautakuwa na nafasi ya kurudisha uhai wake yule uliye muua.

Bila shaka unapokuwa na mawazo sahihi unakuwa na raha na changamko la kweli katika moyo wako au changamko la kudumu katika maisha yako, japo kuna wakati unaweza ukawepo mahali fulani iwe ni kazini au katika hali ya mahusiano au ndoa hata rafiki tu wa kawaida ukajikuta anakushurutisha kufanya mambo ambayo yanatia doa ndani ya moyo wako kwa mfano katika ndoa mara nyingi mwanamke anapojua ameshika mimba uwa anajisikia vizuri sana maana anaona anaongeza heshima yake katika jamii na familia yake  husika lakini pindi inapotokea mume wake kusema yeye hayuko tayari kulea kwa sasa bila shaka inakuwa ni huzuni katika moyo wa mwanamke na anaona kama huyu mwanaume amekuwa katiri na wakati mwingine anaweza kukushurutisha ukatoe huo ujauzito hali hiyo inaweza kumfanya kuwepo mahali pasipo kuwa na furaha ya kweli na majuto yakaanza kuchukua nafasi ndani yako.

Lakini hali hiyo ikiendelea na usipopata maamuzi sahihi ya kutoka hapo bila shaka unaweza kufunikwa na giza ukakosa nuru na hatimaye hata kupelekea kuibuka magonjwa ndani yako yasiyo kuwa na tiba.

Unapaswa kujua maamuzi sahihi ni kitu muhimu sana katika maendeleo yoyote maana bila kuwa na maamuzi sahihi kukamilisha ndoto yako ni kitu kigumu maana unaweza kwenda usijue unakwenda wapi?

Ili ujikomboe katika hali yoyote unahitaji kufanya maamuzi yaliyo sahihi yatakayokupa mwanga katika safari yako haijalishi hata kama yatakugharimu kiasi gani au muda gani ili mradi ni sahihi basi utakuwa salama.

Maamuzi sahihi ni kwa ajili yako wewe na maisha ya kizazi chako hata utakapo ondoka hapa duniani kizazi chako kitafurahia kwa maamuzi sahihi uliyo yafanya.

Pia maamuzi hautufanyi tu kwasababu tunataka kufanya maamuzi bali tunafanya kwa ajili ya ustawi wetu wa kesho japo wakati mwingine unaweza usieleweke vizuri na watu, lakini la kuzingatia hayo maamuzi ni lazima ya bebe nia njema kwa watu sio kwa ubaya.

Yakupasa kujua maamuzi sahihi yanaweza kukutambulisha wewe uliye kamili katika hazina ambazo Mungu aliziweka ndani yako, na zile hazina zinapoanza kushamiri ndivyo hivyo wewe unaanza kushamiri.

Katika lugha ya dunia wanasema umejipata au umejivumbua!

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………

…………0764 018535

Ijumaa, 12 Julai 2024

IPENDE KONA YAKO



Ni muhimu kutambua kila mtu ana kona yake ( mahali alipowekwa/alipojiweka ) hivyo anapaswa kuliendea ili aweze kulitumikia hilo eneo.

Unapozungumzia kona unazungumzia mahali unapotoshea, mahali unapofanya jambo huku mwili wako ukiwa unajua kwanini unafanya au nao unaoshughulika ( mahali unapo pafurahia )!

Kona ni mahali ulipokusudiwa kuwepo au uliandikiwa kuwepo ni kamavile samaki kona yake ni mahali penye maji ambapo anapafurahia na wala hajuti kuwepo hapo hata akikaa siku elfu moja katika maji hayo bado furaha yake haipungui.

Kuipenda kona yako ni kujipenda vile ulivyo pasipo kuangalia muonekano gani unakuvutia  zaidi, maana wapo baadhi ya watu wakiangalia viungo vyao wanaona kama wameonewa na wengine wakijiangalia katika viungo vyao wanaona kama wamependelewa, kwa wale wanaojiona hawako vizuri huwa wanajiona wametengenezwa pasipo kuwepo kwa umakini mathalani wako watu wakiangalia pua zao, midomo au kosogo chao wanakuta wanajichukia na watu wengine huishia katika mawazo yao mabaya.

Ni lazima uipende kona yako ili uweze kuifaidi na kujisikia vyema katika hali hiyo, pindi utakapo amua kuipenda au kuifurahia kona yako bila shaka utaanza kunawiri na kuwa kivutio kwa watu wengi.

Hauhitaji kuzielewa sana kona za wengine kuliko kona yako, kwakuwa thawabu yako hutegemea katika kuitumikia kona yako.

Ni muhimu kuelewa mahali popote unapowekwa basi ujue baraka zako zimeelekezwa hapo katika kona hiyo sio sehemu nyingine ni lazima uwe hapo ili uweze kupata baraka zako maana zitakuja katika njia hiyo na kukupata endapo zitakukuta katika njia hiyo na ukiwa nje ya kona hiyo hauwezi kuzipata hizo baraka.

Ni muhimu utambue kuwa nyumba inakuwa imara kwakuwa kila kitu kipo kwenye mahali/kona yake, hivyo vitu vinavyokuwa sawa basi hapo utaanza kuona ubora na uzuri wa nyumba, hitilafu yoyote itasababisha kushindwa kuhimili vishindo na kutokaa kwa muda mrefu.

Unapokuwa katika kona yako bila shaka kuna mtu mmoja atakuwa salama kwa wewe kukaa katika kona yako kama vile ambavyo mbao zinapokaa katika namna yake basi mabati huweza kukaa katika namna nzuri na iliyobora.

Unapojikita zaidi katika kuijua kona yako unawezesha na kuimarisha utendaji wako uliobora katika wewe kutoka na mapana, ukubwa na nguvu ya uelewa ulionao.

Hauhitaji kujifananisha au kutamani kona ya mwingine hata kama ukiona kona yako haina mng’ao / kushamiri kama wengine.

Unapaswa kujua kuwa hupo hapa dunia kwasababu ya kuishi katika kona hiyo na sio kutazama au kupongeza kona za watu tu.

Wakati mwingine unaweza kuwa unapitia kipindi kigumu na ukaona wale walioshamiri hawakupitia kipindi hicho bali ni muhimu kujua wako wengi walipitia kipindi kigumu kuliko wakati ulionao wewe, ni muhimu ujue kama Mungu amekuweka hapo atakupa mng’ao  wake kwa majira yake.

Yakupasa kujua muunganiko wako mkubwa na Mungu upo kwa wewe kuishi katika kona yako nje ya kona yako utendaji wa Mungu utakuwa mdogo wako kuuona.

Yakupasa kujua KONA YAKO ndio maisha yako hivyo yakupasa uipende kwa ustawi wa maisha yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………………0764 018535