Kuongozwa ni jambo la uhiyari!
Na uwa hatufurahi kwasababu tunaongozwa tu bali tuna furahi kwasababu anayetuongoza anaijua njia na katika maongozi yake usalama unaambatana na wewe,
Ni rahisi kwa njia isiyo na maporomoko mengi kuona kuwa kuna uwezekano wa kufika unakoelekea lakini endapo utakuta kuna njia sio rafiki bila shaka wasiwasi utakuwa na sehemu yake ndani yako.
Haupaswi kuogopa mazingira yasiyo kuwa rafiki ukaona kuwa haufiki bali hakikisha tu unapata maongozi yaliyo sahihi ili ikuweza kupita salama katika mazingira yasiyokuwa rafiki, Ni kama vile unavyoona giza lililozito haupaswi kuliogopa hilo giza lakini hapo ili uwe salama ujue unahitaji mwanga ( maana mwanga ni mbabe wa giza ).
Unaweza kuwa na kitu kizuri ama nafasi nzuri lakini ikatokea ukakosa mwelekeo sahihi unaweza ukajikuta unapoteza ule uzuri au nafasi uliyonayo, mathalani wastaafu wanaopata kiinua mgongo chao au mafao yao endapo wasipopata mwelekeo sahihi ya hizo fedha uweza kujikuta wanapoteza fedha zao na kupelekea kuishi maisha ya majuto na kuruhusu magonjwa yaanze kushamiri ndani ya miili yao.
Kama binadamu uliye na pumzi ya Mungu maadamu unaishi basi kuna mahali unaelekea, mbali katika hali ya ukuaji utoto kwenda ukubwani pia kuna maisha unayoishi sawasawa na ndoto uliyonayo wewe binafsi au ndoto ya familia yako.
Hivyo unahitaji maongozi sahihi ili uweze kufika sehemu sahihi, hivyo ukikosa maongozi sahihi ni vigumu kutimiza lengo katika safari yako.
Roho mtakatifu ni kiongozi pekee aliyebeba usalama wako kwa ajili yako.
Huyo Roho anajua mifumo yote ya dunia na usiri uliojificha ndani ya moyo wa mwanadamu hakuna asichokijua au kilicho kificho katika yeye.
Nje ya yeye usalama ni mdogo sana haijalishi nini kinaonekana kuwa kina usalama basi jua usalama huo sio wa kudumu.
“ Roho atawafundisha na kuwaongoza………….”
Yohana 16:13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Unahitaji kuokoka ili uweze kumpa nafasi aweze kuchukua madhaifu yako au kuchoka kwako na yeye akupe uimara wake na nguvu zake.
Ni kweli mtu anaweza kuajiriwa na kupewa mshahara mzuri sana lakini anaweza asione wapi anaelekea na kesho yake ni ipi?
Na wakati mwingine unaweza kuwa na mipango mizuri kutokana na kipato chako lakini ukashindwa kuyafanya hayo kuwa hai kutokana na hali ya uzito ya kuchukua hatua au vipingamizi unavyo viona.
Pia unaweza fanya kazi binafsi au kuajiriwa ukajikuta moyo wako ni mzito umechoka kabisa na hata ukakosa muelekeo lakini pindi utakapopata muelekeo sahihi wa Roho mtakatifu unaweza kutoka hapo katika hali ya kushindwa na kuwa mshindi.
Yakupasa kujua maongozi sahihi ni afya ya maisha yako.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson …………………………………………………………………………….0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni