Katika jicho la Mungu hapo ndipo kuna umilele wako.
Hivyo unavyoishi hapo basi ujue unaishi katika asili yako na uhalisia wako.
Ni hali ya kawaida na ya wazi ili uweze kuwa kivutio kwa mtu fulani ni lazima uweze kuleta ushawishi katika macho yake yaliyobebwa na maarifa/ufahamu wa Mungu juu ya jambo hilo.
Ni kweli kila jicho la mtu litakavyo kuona litatoa tafsiri yake juu ya muonekano wako, wanaweza kuwa watu watano (5) , lakini inawezekana wawili wakakuona umependeza na wengine wakakuona hujapendeza.
Hivyo mtu mmoja unaweza kuwa na tafsiri nyingi kutoka kwa watu wanaokutazama kutokana na mtazamo wao juu yako.
Hivyo mmoja anavyokwaambia umependeza sio wote watakao kwambia umependeza haijalishi nguo umennunua kiasi gani?
Moja katika janga kubwa hapa duniani ni kufanya kitu ili KUFURAHISHA WATU au WATU WAKUKUBALI au WAKUPENDE.
Huu ni moja ya mtihani mgumu sana katika dunia ya leo, kwakuwa tendo lako moja linaweza beba tafsiri zaidi ya elfu moja kwa watu unao wafanyia na zingine zinaweza kuwa mbaya na zingine zinaweza kuwa nzuri.
Maana unawezafanya kitu sahihi na chema kwa watu na bado wasione huo wema.
Ndomana unaweza kukuta mtu anajigharamu sana kuhakikisha rafiki yake au mpenzi wake kuwa katika mazingira mazuri yatakayofanya yeye afurahie maisha yako na kuongeza upendo kwako, lakini unaweza kukuta wewe unafanya wema lakini yeye hatafsiri kama wema anaweza kutafsiri kama unajipendekeza au unapoteza muda ambao baadaye utakuja kujutia.
Kumbuka unapofanya wema kwa mtu huwa cha umuhimu ni hile tafsiri ya moyo wa mpokeaji na sio ukubwa au udogo wa jambo unalomfanyia.
Watu wengi wamejikuta katika kuhakikisha dunia inawafurahia pasipo kuangalia jicho la Mungu linawatazamaje?
Wako watu waliokuwa wazi wa kumfurahisha rafiki ,boss, ndugu ama wazazi lakini wamkose Mungu kwa kujua au kutokujua.
Na inapotokea huo wema unalipwa katika ubaya wakati wewe ulitegemea dunia itathamini wema wako lakini imekuwa tofauti bila shaka unaweza kujuta hata kwanini ulifanya huo wema.
Lakini pindi utakapofanya wema ukilenga kupata kibali katika jicho la Mungu bila shaka utapata malipo zaidi ya ule wema ulioufanya kwa watu haijalishi hao watu wameupokeaje?
Unapaswa kujua jicho la Mungu linapokuangalia katika wema unaoufanya kwa mtu au watu basi hapo unakuwa mahali sahihi.
Unapoishi katika jicho la Mungu unapata neema ya kutambulishwa na kuelekezwa ni nani umfanyie huo wema ili uwe msaada wa kudumu katika maisha yake.
Kumbuka wema unalipwa na Mungu na sio watu, hivyo wema unaoufanya kwa watu usitegemee malipo kutoka kwao hata kama watafanikiwa.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson …………………………………………………………………… 0764 018535