Ijumaa, 20 Juni 2025

ATAKUFICHA UTAKUWA SALAMA.

 



Ni kusudi la Mungu usiaibike au aibu isifanye makao kwako.

Wakati mwingine mambo yanapokuwa magumu unatamani kukaa mahali au katika hali ya kujiona kuwa uko salama japo unaweza usiwe sawa..

Watu wengi hawatamani kujificha tu au kuji hifadhi tu bali wanatamani mahali hapo watakapo jisitiri basi usalama wa kutosha uwepo.

Mahali pa kujisitiri ambapo usalama sio wa kudumu hilo nalo jangwa mahali hapo ulipo bado  mabaya yatakupata na kamwe hautajiona au maana ya kujificha au kujisitiri hapo.

Yakupasa ujue maficho ya aina yoyote bado unaweza usiwe salama hata kama utachukua muda wa watu kujua wapi umejificha na namna ya kukufikia lakini tambua ipo siku watakufikia tu,

Mathalani, Osama alijificha mahali ambapo aliamini kuwa yuko salama dhidi ya wa marekani lakini pindi marekani walipotambua pale alipo waliweza kujipanga na kumvamia hatimaye na kuondoa usalama wake au kinga yake na kupelekea kifo chake.

Hivyo ulinzi hauhitaji kujiona uko salama tu, bali uhakikishe huo salama.

Ni Mungu pekee mwenye uwezo wa kukuficha dhidi ya hatari mbaya nawe ukawa salama katika ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili.

Maficho yote yaliyobebwa na watu huwa usalama wake unakuwa sio wa kudumu maana watatokea watu wengine wenye uwezo zaidi yao watayaharibu hivyo maisha yako.

Lakini Yesu alipofichwa na Mungu/Mbingu katika ujio wake wa kuwa kumboa wanadamu alikabaliwa na kifo dhidi ya herode lakini mbingu ilipomficha alikuwa salama na hatimaye akalitimiza lile kusudi alilolijia japo katika vita kali lakini aliibuka mshindi.

Usalama unaozaliwa na Mungu ni mkamilifu kuliko kitu kingine sio watu au ushirikina unao uwezo wa kukupa usalama kudumu.

Ni Mungu kujua wewe unapokuwa wake inakuwa ni sawa na mazazi mwenye akili ambaye hataki kuiona aibu ya mwanaye impate.

Unahitaji wewe kuwa na Mungu ili maficho yake yawe juu yako katika vita dhidi ya huduma yako, uchumi au mahusiano yako yeye atakufanya uwe mshindi na usalama uzidio katika maisha yako.

Unaweza kujikuta umeingia katika mazingira ukaona vita ni kubwa na usione wapi pa kutokea na ukajikuta unamlaumu Mungu kwanini ameruhusu aibu ikupate bila shaka ni muhimu utambue mazingira yapo kukuvunja nguvu dhidi ya Mungu unayemwamini……………..

Daudi hata alipoingizwa katika mazingira magumu ya kupambana na Goliath bado alisimama katika kumwamini Mungu na Mungu akamuonekania,

Hauhitaji watu zaidi ya kumwihitaji MUNGU!

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson ……………………………………………………………………………………0764 018535

Ijumaa, 6 Juni 2025

ACHA AKUONE VILE ULIVYO:

 



Hakuna kitu kizuri kama mtu kukuona vile ulivyo!

Maana ni hatari sana mtu kukuona nje ya uhalisia wako, unaweza kuishi maisha ya mateso bila kutarajia na ukajikuta umeingia humo bila kutaka.

Mathalani unaweza kukuta umetoka na wenzako na mkiwa sehemu ya kupata vinywaji, ki ukweli unaweza kuwa ulikuwa na  uhitaji wa kunywa soda lakini ukakuta rafiki zako wote wanakunywa maji, hivyo nawe ukaagiza maji badala ya soda na hali hiyo ikapelekea kunywa maji pasipo kuyafurahia, ukanywa maji utafikiri unakunywa dawa yenye uchungu uliopitiliza.

Naam pia unaweza kuulizwa kuwa unajua kuendesha gari? Nawe kwa kuona usimwangushe yeye aliye kuuliza ukamwambia unaweza lakini ukweli unajua huna uwezo mzuri wa kulimudu gari! Lakini mwishowe unaweza pata madhara makubwa hata ikapelekea kujuta na kujilaumu kwamba ni vyema ungesema ukweli tu ungekuwa salama kuliko kuisababishia hasara kubwa taasisi husika.

Pasipo kujua unapokuwa wazi unakuwa ni rahisi kusaidika kuliko kutokuwa wazi maana unaweza usisaidike au ukachelewa kusaidika.

Unapotambua uhalisia wako ( vile ulivyo ) unampa urahisi hata mtu anayetembea na wewe mathalani unapotembea na mtu ukajua anashida ya miguu bila shaka utatembea na yeye kwa taadhari kubwa huku ukihakikisha ufanyiki teso juu ya huyo ndugu lakini ukakuta mtu ni anashida ya miguu lakini anataka usijue kuwa yeye anashida hiyo nawe ukatembea naye kama mtu asiye mdhaifu wa miguu naye akajitahidi kama mtu aliyemzima kabisa bila shaka ikitokea amemaliza salama safari yake atakuwa na maumivu makali sana na inaweza kupelekea hali yake kuwa mbaya zaidi kuliko awali.

Mtu kukujua vile ulivyo ni ishara ya utayari wa dhati na usiyependa kumsumbua katika safari yake.

Ndivyo hivyo hata kwa upande wa Mungu…………….

Usitafute Mungu kukuona kama watu wanavyokuona utapata shida na unaweza kujikuta unafurahia  kitu ambacho hakifurahishi.

Usitake kuona kama Mungu ameona umevaa wigi la gharama kiasi gani? Nguo kiwango gani?, Ukienda kwa Mungu kwa jinsi hiyo bila shaka kuna kipindi kitafika utataka Mungu akuabudu badala ya wewe kumwabudu Mungu.

Mungu haitaji sana kuona maendeleo yako ya mwilini japo wewe uweza kujifurahia lakini hasa anahitaji kuona maendeleo ya roho yako.

Unahitaji kuwa mbele za Mungu vile ulivyo maana yeye anakujua vizuri zaidi sana, na maana wewe kuwa vile ulivyo mbele za Mungu ni ishara kubwa kuwa uko tayari yeye Mungu kufanyika kuwa utoshelevu wako na stara yako.

“ Isaya alipogundua midomo yake michafu”

Isaya 6:5 Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.

 6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu;

 7 akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.

 8 Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.

 9 Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione.

 10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.

Japo alikuwa nabii mkubwa anayeaminika lakini alienda mbele za Mungu na kujidhiri vile alivyo na kuonyesha uhalisia wake mbele za Mungu naye Mungu akatakasa kinywa chake ili kizidi kufaa.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson……………………………………………………………………………………….0764 018535

 

Ijumaa, 23 Mei 2025

AKILI YA MUNGU

 


Kitu pekee kinachoweza kumtambulisha mtu na hata kumweka katika nafasi ya ustawi wake ni MATUMIZI SAHIHI YA AKILI YAKE.

Hivyo akili yako inaweza kukutambulisha katika mazingira ya juu au ya chini.

Hivyo watu wanapoyaangalia mazingira yako inatoa tafsiri ya maarifa uliyo nayo yanayopelekea matumizi ya akili yako.

Kinachoonekana kinaongea zaidi kuliko kile unachokiongea.

Naam sote tunajua……Akili ya Mungu haiwezi kushindwa wala haina tabia ya mashindano.

Pia moja ya sifa kubwa ya akili ya Mungu ni KUTOCHOKA.

 Warumi 12:2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Namna unavyoendesha mambo inatoa tafsiri juu ya akili yako jinsi ilivyo.

Katika dunia ya leo kuna mifumo mingi……Mfumo unaweza kukutengeneza na kukupa akili yake nawe ukakuta unatembea humo kwa kujua au kutokujua.

Bila shaka unapopata kuielewa akili ya mtu ndivyo unavyoweza kumwakilisha vyema, kwa kuwa utafanya sawasawa na matakwa ya akili yake naye atakuwa wewe.

Unapoivaa akili ya mtu basi unabeba na utendaji wa mtu, ndo maana unaweza kusikia mtu akisema “ jinsi anavyofanya ni kama mjomba wake alivyokuwa akifanya”

Akili ya mtu imebeba utendaji wa mtu husika.

Na maajabu ya mtu katika utendaji utegemea uwezo wa akili yake.

Katika akili ya Mungu unapopata tabia za Mungu ambazo unadhihirika katika utendaji wako.

Tabia za akili ya Mungu:

(a) Haina tafsiri/ maana ya kushindwa

(b) Ina matumaini yasiyozuilika

(c) Mashaka/ hofu/ wasiwasi haupo ndani yake.

Unahitaji kuamini kuwa unaweza kufanya mambo mengi pindi utakapotembea kwenye akili ya Mungu.

Tuna pozungumzia akili ya Mungu tunazungumzia ni upeo ambao Mungu anakupa katika kufanya mambo mbalimbali ili kuleta ufumbuzi katika jamii yako unaweza kuwa umeokoka au hujaokoka.

Lakini akili ya Mungu kwa uhalisia tuna maana ni ROHO MTAKATIFU yeye huyu ana magawanyo mengi lakini moja wapo ni kukupa akili ya Mungu ili uweze kufanya yale uliyopaswa katika kiwango cha Mungu.

Ili upate matokeo ya KIMungu ni lazima utembee katika akili yake, maana ndani ya akili ya Mungu kuna maajabu yake.

Hauwezi kutembea katika akili ya Mungu alafu ukawa mtu usiye na athari katika ufalme wa giza.

Akili ya Mungu inakupa kuishi katika yale unayopaswa/ ulivyo kusudiwa kuishi,kwa kuwa ndani yake kuna kujitambua na hatimaye kuwa kile Mungu anachokitaka.

Ili umuone Mungu katika maisha yako ni lazima utembee katika akili ya Mungu na sio yako.

Natembeaje katika akili ya Mungu:

i. Ni lazima uwepo katika mazingira ya yeye yuko ili afanye mageuzi ya akili yako na kukupa akili yake.

ii. Ni lazima uonyeshe kuwa unahitaji akili ili uweze kuishi, maisha yako yanaanza pale akili ya Mungu inapoanza kufanya kazi.

Yohana 15:5b…maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

iii. Ni lazima uipe nafasi ya utendaji kuliko akili yako ili ianze kuimarisha utendaji wake.

Maana unapoipa nafasi ni kuruhusu ifanye kazi hata kama akili yako haielewi kumbuka hapo ndio mchakato wa wewe kuzaliwa kiumbe kipya.

 2 Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Unapokuwa na akili ya Mungu hapo sasa unaweza kuwaza, kuongea na kutenda kama Mungu.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson……………………………………………………………………………..0764 018535