Akili njema ni zaidi ya akili yenye afya!
Ni akili isiyobeba lawama juu ya mtu yeyote, kuwa ndiye kikwazo katika maisha yake.
Bali ujiona yeye ndiye chanzo cha kwenda mbele au kurudi nyuma.
Akili njema mara zote ufanya jambo sahihi kwa wakati sahihi ( utembea katika hekima ).
Pia hii akili haina kukata tamaa wala kuchoka maana huona hali yoyote ya kushindwa kufanikisha jambo, yeye ndio muhusika wa kushindwa kukamilisha na wala sio mtu mwingine wa kulaumiwa nje ya yeye.
Akili njema utegemea sana chakula gani unakula ili kuilisha akili yako, maana ukila chakula kisichokuwa bora inaweza pelekea akili yako kukosa afya njema na kupelekea kushindwa kufanya lile unalopaswa kulifanya kwa ukamilifu.
Ikumbukwe kuwa kuna tofauti kati ya chakula cha mwili na chakula cha akili, chochote kinachoongeza tija katika ufahamu wako basi hicho ni chakula cha akili na chochote kinachoongeza tija katika mwili wako basi ni chakula cha mwili, japo kuna wakati chakula cha mwili kinaweza kuwa na tija katika ufahamu wako/akili yako.
Akili hii upelekea kuwa na hali ya kujitegemea au kijisimamia mwenyewe haigemei kwa mtu yeyote!
Maamuzi yanayotokana na akili hii siku zote yanakuwa thabiti yenye nia njema isiyobebwa na mashindano.
Unahitaji kuwa na akili njema ili kuona yasiyowezekana kuwa yanawezekana maana akili njema uwa inatoa mwanga palipo na giza.
Na hili uweze kumtegemea Mungu katika viwango vyake ni lazima uwe na akili safi/njema.
Nini maana ya akili njema?
i. Ni hali ya kujitambua na kusimamia yale unayopaswa kuyafanya kwa uaminifu.
- Unapaswa kujitambua wewe kuwa una majukumu tayari na wewe ndio muhusika kufanikisha hayo majukumu, na unahitaji akili njema ili uweze kufanikisha yale unayopaswa kufanya.
Unapaswa kuyasimamia majukumu yako kutoka kwenye akili yako iliyo njema pasipo kuwa tegemezi popote.
ii. Ni hali ya akili yako kumuhusisha Mungu kwa asilimia mia moja katika utendaji.
- Kuna wakati akili yako inakosa majibu kwa namna yake, kwasababu inamipaka hivyo kushindwa kutoa jibu linalopaswa.
Hapa Mungu anaitengeneza akili yako katika akili yake na kufanya yale yaliyoshindikana kutoka kwenye akili yako.
Na hapa ndipo Mungu ufanya ili kuleta maajabu ya mbingu hapa duniani ili kuutangaza ufalme wake.
Unahitaji kumsikiliza sana Mungu katika utulivu na utayari ili paweze kuleta wepesi wa akili yako kuielewa akili ya Mungu hivyo kupelekea utendaji wake kufanikiwa.
Unapaswa kuuelewa utendaji wa Mungu ili uweze kuuruhusu kuwa na nafasi katika akili yako.
Unapokuwa na akili njema hata mwili wako unaweza kuwa na afya njema, maana kuna baadhi ya magonjwa yanazaliwa pale akili yako inapokosa majibu au utatuzi uliosahihi mathalani magonjwa ya pressure au kupalalaizi ( stroke ) yanaweza kuathiri mifumo ya mwili wako na kufanya kuwa dhaifu.
Usipopambana kuwa na akili njema bila shaka utaishi katika akili mbaya.
INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson ……………………………………………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni