Jumanne, 3 Septemba 2013

KWA NINI USILIE?



USILIE;
 
Usilie ni neno muhimu sana mtu uhitaji kulisikia pindi anapokuwa katika majonzi ndani  moyo wake na mateso ya jumla katika maisha yake kwa ujumla.

Watu pindi wanapo umizwa uwa wanalia kwa sababu mbalimbali moja kati ya sababu hizo ni kuondoa kitu ndani ya moyo wake hivyo uamini pasipo kulia lile jambo litazidi kumsumbua ndani ya moyo wake mathalani misiba,kusalitiwa na kutengwa.

Na njia ya kulia imekuwa ikitumika siku hadi siku katika kuleta pumziko ndani ya moyo wa binadamu, japo sio wote wamekuwa wakihitumia lakini siku baada ya siku hii njia imezidi kuwa katika nafasi ya juu.
Hivi sasa mtu akiwa analia sio swala la ajabu kwani katika jamii watu washazoea kuona watu wanalia ila imebaki kama kielelezo cha kumtambua mtu mwenye shida.

Ni kweli njia hii kutokana na imani zetu njia hii imekuwa ikitumika sana japo matokeo yake yamekuwa ni madogo tofauti na lile lengo lililokusudiwa. watu wamekua wanalia sana wakitegemea yatakwisha lakini badala yake yamekuwa yakinyamaza mambo ndani ya moyo kwa muda halafu baadae mambo yakaendelea kuwa magumu.

Hivi sasa imefika kipindi katika jamii yetu usipolia katika tukio la kulia jamii inaweza kukushangaa kwa kuona kwamba swala hili alijamgusa kwahiyo ishara ya wewe kukuguswa ni kulia.


Kwanini tusilie wakati yanayotokea yanaumiza moyo!!!!!!!

Ni kweli kila binadamu anayomachozi ndani yake na udhihirisho wake utokwa na machozi katika kipindi kigumu na kama yasipotoka hapo yatoke wapi?

Ni kawaida mtu anapolia kuna mambo mengi yanaendelea ndani ya moyo wa mtu na akili ya mtu uwa katika hali isiyoelezeka ni ishara ya kumpenda sana mtu ambae ametengana nae,aliyemsaliti au aliyetoka duniani(kufa).

Wakati mwingi sana mtu ulia sana kwakua pindi anapofikiri uwepo wa mtu huyo aliyetengana naye yako mambo angeyafanya kwake na hivyo kutoweka kwake kunaleta pengo ambalo hakuna mtu anaweza kulijaza.

Lile tumaini alilokuwa nalo kwa mtu husika ndicho kiwango cha maumivu atakayomuachia maumivu ndani ya mtu husika.


I.ulimtambue baada ya kutambulishwa:

Unaweza kutambulishwa na Mungu au mtu mwingine pia ata wazazi wako uliwatambua baada ya kutambulishwa.
Mtu yeyote uliyempenda kiasi gani ni pale tu ambapo ulipotambulishwa na yeye kukuonyesha upendo wake kwako.

Kulia ni jambo la kawaida sana lakini kubwa sana lazima utambue yuko ambae alikukutanisha nae ambae anaweza kutimiliza hisia zako na kukufanya kuwa bora kuliko wa leo na siku nyingine.

Bado mambo mengi utafanya hata pasipo yeye kwakua ata yeye alikuwa ana mambo yake ambayo yanamkabili hivyo sio kila kitu mtaona mko sawa.

Japo ungependa hata usikie ushauri wake katika mambo yako ambayo unafurahia kukutana nae mkashirikiana kwa pamoja.

Tambua bado kuna nafasi ambayo yeye aliruhusu litokee anayo njia nyingine iliyo bora kwako jua nina aliye fanya mkawa pamoja kama bado yupo jua kuna nafasi iliyo njema sana.

II.itambue nafasi ya Mungu ndani ya maisha yako

Mtu yeyote yule hakikisha achukui nafasi ya Mungu ndani yako bali nafasi ya mtu mpe nafasi yake na Mungu anayo nafasi yake ndani yako.

Lazima uwe na uelewa kuwa ni Mungu pekee ambae hawezi kukuacha ila wengine wote wanaweza kukuacha katika mazingira ya kuwapenda au kuwachukia.

Katika yote hakikisha kuwa Mungu anabaki kuwa na nafasi ya kwanza ndani ya maisha siku zote kwa kua ni yeye pekee ambayo anayeijua kesho yako na baada ya hiyo kesho(hatima yako).

Lazima utambue kuwa anajua kila kitu kinahusu wewe hata kama bado ujamwambia na antambua mahitaji yako kuliko vile wewe unavyofikiria.

Siku zote Mungu ndiye pekee ambaye anawatosheleza watu wote kwa kadili uweza wake ulivyo na yeye ndiye akulindiye kesho yako, mtu anaweza kukuahidi lakini asitimize kwa sababu mbalimbali moja wapo ni kifo.

Unapotambua nafasi ya Mungu ndani yako ndipo hapo machozi yako yanakuwa na matumaini na sio kukata tamaa.

Kilio mara nyingine kinaonyesha hali ya kukosa mwelekeo lakini pindi utakapo tambua kuwa unaye Mungu ambaye kwa yeye umetoka na utalejea.
Ayubu 1:22

Unahitaji kumuona Mungu akiwa mwema sana ili usije ukamkufuru yeye  lazima katika hilo bado Mungu bado mwema sana ila unahuzunika kwa vile ujajua kusudi lake kwa hilo.


Prepared by ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com


                      HAKUNA SWALI GUMU LISILO NA JIBU KWA MUNGU!!!!!!!!!!!!!
                                                      Just believe him………

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni