NGUVU YA MUNGU NDANI YA MWAMINI;
Siku zote mtu ufanya jambo kutokana na nguvu yake
kwahiyo mwisho wa nguvu zako ndio mwisho wa utendaji wako.kwakua hauwezi fanya
jambo ambalo litakuwa zaidi ya nguvu yako
Hivyo nguvu zako ilivyo ndivyo usalama wako ulivyo
na ndivyo utanuzi wako ulivyo kwahiyo nguvu uliyonayo ndiyo inaamua wewe uweje?
Kila mtu anacho kitu kinachomfanya ajivunie wako
watu wanajivunia PESA,MALI na hata wengine wanajivunia WATU.
Kwa hiyo kila mtu anachojionea fahari na sio kitu
kibaya kwakua kila jambo limebeba furaha ya mtu husika kwa sababu ni mmiliki
wake.
Duniani ili uishi vizuri lazima kiwepo kitu ambacho
kinacho kupa nguvu ya wewe kuendelea kuwepo la sivyo utaishi hauwezi
kuyafurahia maisha ya dunia.
Japo zipo nguvu mbalimbali ambazo wanadamu uzitumia
katika kufanikisha mambo yao wapo watu wanatumia nguvu za giza(makabulini,bahari,miti
na mizimu) na wengine hali ambayo Mungu amewajalia na wapo ambao wame mweka
Mungu katika utendaji wao.
Nguvu ni mahali ambapo maisha yako yameegemea ambayo
kwa hapo unapata faraja,amani na mwendelezo mzima wa maisha yako.
Ni kweli kuna nguvu nyingi ambazo kila binadamu
wanazo ziamini na kwa hizo wamezielekezea maisha yao LAKINI sio kamwe kama mtu ambaye ndani yake kuna nguvu ya Mungu.
Hii ni nguvu ambayoikiamua kufanya jambo hakuna
nguvu yeyote ambayo inaweza kuzuia au kushindwa kutokeza. Hii ni nguvu ambayo
ndani yake kunakuwa na MUNGU mkamilifu pasipo kupungua,
Hii nguvu ndiyo kwahiyo dunia ilipata kuwepo,mbingu
ikafunguka,kuzimu kukataharuki,wafu wakafufuliwa na mengine hata usiyo waza
lakini Mungu anatenda.
Hii nguvu haibahatishi bali inapotumwa lazima
ikayatimilize yale yaliyo tumwa kwa ukamilifu wake na hakuna ambalo
litashindikana kwake.
Unapo mwamini Mungu lazima uziamini nguvu zake
ambazo kwa hizo zina kuwa na nguvu katika utendaji wake.
Namna
ya kuwa na nguvu ya Mungu ndani yako;
Hii ni nguvu ambayo haina mashariti katika hali ya
kukuganamiza bali katika hali ya kuinua maisha yako kuwa katika hali njema
zaidi.
I.Neno la Mungu ndani yako.
Waebrania 4:12
Nguvu ya Mungu hiko ndani ya neno lake mahali ambapo
kuna neno lake basi kuna mamlaka yake,utoshelevu wake.
Kwahiyo ndani yako kama hakuna neno lake usitegemee
ukapata hiyo nguvu kwa kuombewa au kwa namna nyingine yoyote. Kwakua nguvu yake
inaingia ndani yako kupitia neno lake.
Katika kujenga nguvu ya Mungu kuzidi kutawala ndani
yako ni muhimu sana ndani yako pawepo kuwa na hali ya neno la Mungu ndani yako
siku zote.
Wakolosai 3:16
Lazima uamue katika kujaza neno la Mungu ndani yako
katika hali stahiki kama inavyotakiwa katika ufasaha zaidi ndani yako ili nguvu
ya Mungu izidi kuimarika ndani yako pasipo kuchoka ndani yako.
Mathayo 7:24-27
Hakikisha neno la Mungu linazidi ndani yenu kwa
ubora na nguvu zake kila siku hakikisha neno la Mungu linakuwa la pekee ndani
yako na pia uhakikishe unalipa nafasi katika ukamilisho wake.
Unapoamua kulisoma neno ni kuamua kumsikiliza Mungu
hii hatua ya muhimu lakini ni muhimu kutafuta utendaji wa lile ulilolisikia
toka kwake.
Pasipo hilo hakuna maana yoyote kwako ya wewe
kuwatayari kumsikiliza lakini usiwe tayari
wa kutenda katika yale aliyokuagiza.
Prepared by ;
Nelson, Cothey – 0764 018
535 or cotheyn@yahoo.com
Katiti, James - 0713 398 042
or james.adili19@gmail.com
BARIKIWA RAFIKI………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni