Jumapili, 4 Januari 2015

MTEMBEO WA KIMUNGU




MTEMBEO WA KIMUNGU;





Kila mtu ujisikia fahari sana pindi anapotembea na mtu maalufu au mwenyesifa njema katika jamii husika au katika eneo Fulani mathalani kazini,shuleni. Lakini pamoja na kutembea nae anaweza kuwa msaada kwa kitambo tu alafu hali yako ya mwanzo ikajirudia kama hapo awali.lakini uko mtembeo wa Kimungu ambao mtu anatembea kupitia hiyo au mamlaka ya kimbingu ndani yake.

Mtembeo wa kiMungu huu unadhihirishwa na mtu husika angali akitembea hapa duniani watu wanamuona ni Mungu anatembea kwa namna isiyo ya kawaida.tatizo linakuja pale ili mweze kutembea na Mungu lazima mkubaliane na kushirikiana katika kila kona inayokuhusu ili kupata kibali chake.


MTEMBEO  WA  KIMUNGU  UNAONEKANA  KWA  MTU  WA  NAMNA  GANI!

Sio kila mtu anayeshika biblia basi anaweza kutembea mtembeo wa KiMungu au anajulikana sana mtaani basi anaweza kuonyesha mtembeo wa KiMungu, kutumiwa na Mungu na mtembeo na Mungu ni vitu viwili vilivyotofauti kabisa na kama watu wanakuwa hawawezi kukabiliana kwa namna yeyote kwani hapo kila mtu anamwelekeo wake.

Mtu ambaye anayetembea katika mtembeo na Mungu huyu anakuwa ni zaidi ya hatari kwa anaweza kusababisha mapinduzi yasiyo zuilika kwa kua alienaye yeye azuiliki kwa chochote kwakua amejikamilisha na kujitosheleza.

Mtu ambaye anatembea katika mtembeo wa KiMungu huyu ni mtu ambaye akili yake imekufa na mwili wake umepoteza utawala wake na hisia zake pamoja na hofu za kibinadamu zimepoteza nafasi katika maisha ya mtu huyu, anakuwa ni mtu ambaye yuko tayari kujitoa kwa ajili ya chochote pasipo kuangalia gharama zipi atakazoingia baada ya tukio hilo.

Huyu ni mtu ajali anakokwenda anaamini anakokwenda yuko tayari kukabiliana na jambo lolote ili mradi tu lile alilokusudia linafanyika kwa ubora wake na kiufasaha au kwa muonekano wa kawaida anaonekana kanakwamba ajali ya maisha yake bali ni kile kilichomzidi kinachomlevya.

Huyu ni mtu ambaye apatiusaidizi wa dunia( elimu, heshima yake na msaada wake) bali atapingu iko nyuma yake katika kuyafanikisha yale yote yaliyo kusudiwa kwa nguvu na msaada wa mbingu.

Nguvu ya mtu huyu inasimama yenyewe na inafanya kwa ubora wa hali ya juu sana kwani hakuna kitu kingine kinachoweza kupingana na nguvu hiyo asili ya nguvu hiyo haina hali ya kushindwa imeshikiliwa na mbingu na tayari kwa ushindi na sio kwa kushindwa.

Mtu huyu amebeba dhamana ya mbingu ambayo inamshikilia pasipo kuchoka wala kumuacha kwakua yeye ndio makao ya hiyo mbingu yohana 14: 23

Hauhitaji kumsiliza ili uamini bali muonekano wake tu utaona mbingu inashuka na kumfunika........na inadhihirika sana katika utendaji wake kwakua ni Mbingu itakuwa ikitembea badala yake.



Imeandaliwa na;
            

                    Cothey Nelson...................................................................0764 018535

Alhamisi, 1 Januari 2015

UPENDO WA MASHAKA




UPENDO WA MASHAKA;




Kila mtu ujisikia huru na vizuri sana pindi anapotambua wako watu ambao wana mpenda lakini hali hiyo utoweka pindi anaposikia uhalakini wa upendo wake juu yake, hivyo baada ya kujiachia anaanza kuishi kwa tahadhari sana na sio kujiamini tena, katika hali hii mtu uona ni bora asiwe na mtu ambaye anayempenda kuliko kuwa na upendo usio na muafaka mzuri katika maisha yao.

Watu wengi wamekuwa wakiishi kwa tahadhari sana hasa katika ulimwengu wa sasa binti anamashaka na upendo wa baba yake, mvulana anamashaka na upendo wa mama yake hata kaka na dada wamekuwa wakiishi katika wasiwasi, na chimbuko hili linatokana na baada ya kutendwa au habari ya kusikia kwa watu ambayo inakupa hofu katika mausiano yoyote.

Upendo huu wa mashaka uwa upo katika sehemu zote katika urafiki na hata katika uchumba watu wamekuwa wakiishi kwa tahadhari sana katika maisha yao wako watu waliotendwa na marafiki zao mathalani binti kumwambia mchumba wake rafiki yake na baadae kusalitiwa na hata kwa wavulana katika kuambiana au kutambulishana mchumba wake unakuta watu wanasalitiana.

Sio katika hili tu hata katika shughuli mbalimbali watu waliaminiana katika shughuli Fulani mathalani muuza duka kumwibia boss wake au watu kudhulumiana fedha zao kutokana na utofauti uliopo katika maslai binafsi. Watu wengi wamekuwa wakishilikiana katika hali ya mashaka mpaka waaminiane inachukua muda mrefu sana lakini ni ngumu kuendelea kumwamini.

Katika dunia ya sasa watu wamekuwa wakiishi katika hali ya kutofurahi na kujiamini utafikiri watu wanafanya kazi za madawa ya kurevya katika hali siri na kutokuaminiana kwa hofu kubwa.
Ukweli dunia ya sasa kuwa na mtu katika upendo usio na wasiwasi ni ngumu sana ki ukweli kunavita kubwa sana katika kutambua yupi ni sahihi na yupi si sahihi!

Unaweza ukampata rafiki ambaye anaweza kuwa si urafiki wa mashaka kwanza lazima ujue jambo la kwanza na la muhimu sana WEKA UPENDO WAKO KWA MUNGU;

Hili ndilo kila kitu kwako unapo mpenda Mungu bila shaka Mungu atakupenda na hata kupa marafiki ambaye yuko sahihi ambaye atafanyika Baraka na amani katika maisha yako, na rafiki sio lazima akupe hela wala chochote bali ni vile alivyokupa nafasi ndani ya moyo na namna anavyokuelewa.

Lazima ujue kuwa hakuna wa maana sana kama URAFIKI NA MUNGU kwani ndilo jibu sahihi katika maisha yako. Ishi na Mungu katika maisha yako yote hakika utakuwa salama sana, na kila jambo.

Usichukue hasira ya haraka wala usiwe mtu ambaye unamawazo mabaya bali zaidi sana muelewe mtu kwa msaada wa Mungu, maana ni Mungu pekee ndiye anajua wewe unahitaji nini? Na atakuwa Baraka katika maisha yako.

Kingine lazima utambue kuwa ustawi wa maisha yako ni bora kuliko mtu yeyote kwakua ustawi wako umebebwa na Mungu na sio kitu kingine............yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana.



Imeandaliwa na;
     

                  Cothey Nelson......................................................0764018535