UPENDO
WA MASHAKA;
Kila mtu ujisikia huru na vizuri sana pindi
anapotambua wako watu ambao wana mpenda lakini hali hiyo utoweka pindi
anaposikia uhalakini wa upendo wake juu yake, hivyo baada ya kujiachia anaanza
kuishi kwa tahadhari sana na sio kujiamini tena, katika hali hii mtu uona ni
bora asiwe na mtu ambaye anayempenda kuliko kuwa na upendo usio na muafaka
mzuri katika maisha yao.
Watu wengi wamekuwa wakiishi kwa tahadhari sana hasa
katika ulimwengu wa sasa binti anamashaka na upendo wa baba yake, mvulana
anamashaka na upendo wa mama yake hata kaka na dada wamekuwa wakiishi katika
wasiwasi, na chimbuko hili linatokana na baada ya kutendwa au habari ya kusikia
kwa watu ambayo inakupa hofu katika mausiano yoyote.
Upendo huu wa mashaka uwa upo katika sehemu zote
katika urafiki na hata katika uchumba watu wamekuwa wakiishi kwa tahadhari sana
katika maisha yao wako watu waliotendwa na marafiki zao mathalani binti
kumwambia mchumba wake rafiki yake na baadae kusalitiwa na hata kwa wavulana
katika kuambiana au kutambulishana mchumba wake unakuta watu wanasalitiana.
Sio katika hili tu hata katika shughuli mbalimbali
watu waliaminiana katika shughuli Fulani mathalani muuza duka kumwibia boss
wake au watu kudhulumiana fedha zao kutokana na utofauti uliopo katika maslai
binafsi. Watu wengi wamekuwa wakishilikiana katika hali ya mashaka mpaka
waaminiane inachukua muda mrefu sana lakini ni ngumu kuendelea kumwamini.
Katika dunia ya sasa watu wamekuwa wakiishi katika
hali ya kutofurahi na kujiamini utafikiri watu wanafanya kazi za madawa ya
kurevya katika hali siri na kutokuaminiana kwa hofu kubwa.
Ukweli dunia ya sasa kuwa na mtu katika upendo usio
na wasiwasi ni ngumu sana ki ukweli kunavita kubwa sana katika kutambua yupi ni
sahihi na yupi si sahihi!
Unaweza ukampata rafiki ambaye anaweza kuwa si
urafiki wa mashaka kwanza lazima ujue jambo la kwanza na la muhimu sana WEKA
UPENDO WAKO KWA MUNGU;
Hili
ndilo kila kitu kwako unapo mpenda Mungu bila shaka Mungu atakupenda na hata
kupa marafiki ambaye yuko sahihi ambaye atafanyika Baraka na amani katika
maisha yako, na rafiki sio lazima akupe hela wala chochote bali ni vile
alivyokupa nafasi ndani ya moyo na namna anavyokuelewa.
Lazima ujue kuwa hakuna wa maana sana kama URAFIKI
NA MUNGU kwani ndilo jibu sahihi katika maisha yako. Ishi na Mungu katika
maisha yako yote hakika utakuwa salama sana, na kila jambo.
Usichukue hasira ya haraka wala usiwe mtu ambaye
unamawazo mabaya bali zaidi sana muelewe mtu kwa msaada wa Mungu, maana ni
Mungu pekee ndiye anajua wewe unahitaji nini? Na atakuwa Baraka katika maisha
yako.
Kingine lazima utambue kuwa ustawi wa maisha yako ni
bora kuliko mtu yeyote kwakua ustawi wako umebebwa na Mungu na sio kitu
kingine............yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana.
Imeandaliwa na;
Cothey
Nelson......................................................0764018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni