MTEMBEO
WA KIMUNGU;
Kila mtu ujisikia fahari sana pindi anapotembea na
mtu maalufu au mwenyesifa njema katika jamii husika au katika eneo Fulani
mathalani kazini,shuleni. Lakini pamoja na kutembea nae anaweza kuwa msaada kwa
kitambo tu alafu hali yako ya mwanzo ikajirudia kama hapo awali.lakini uko
mtembeo wa Kimungu ambao mtu anatembea kupitia hiyo au mamlaka ya kimbingu
ndani yake.
Mtembeo wa kiMungu huu unadhihirishwa na mtu husika
angali akitembea hapa duniani watu wanamuona ni Mungu anatembea kwa namna isiyo
ya kawaida.tatizo linakuja pale ili mweze kutembea na Mungu lazima mkubaliane
na kushirikiana katika kila kona inayokuhusu ili kupata kibali chake.
MTEMBEO WA KIMUNGU UNAONEKANA KWA MTU
WA NAMNA GANI!
Sio kila mtu anayeshika biblia basi anaweza kutembea
mtembeo wa KiMungu au anajulikana sana mtaani basi anaweza kuonyesha mtembeo wa
KiMungu, kutumiwa na Mungu na mtembeo na Mungu ni vitu viwili vilivyotofauti
kabisa na kama watu wanakuwa hawawezi kukabiliana kwa namna yeyote kwani hapo
kila mtu anamwelekeo wake.
Mtu ambaye anayetembea katika mtembeo na Mungu huyu
anakuwa ni zaidi ya hatari kwa anaweza kusababisha mapinduzi yasiyo zuilika kwa
kua alienaye yeye azuiliki kwa chochote kwakua amejikamilisha na kujitosheleza.
Mtu ambaye anatembea katika mtembeo wa KiMungu huyu
ni mtu ambaye akili yake imekufa na mwili wake umepoteza utawala wake na hisia
zake pamoja na hofu za kibinadamu zimepoteza nafasi katika maisha ya mtu huyu,
anakuwa ni mtu ambaye yuko tayari kujitoa kwa ajili ya chochote pasipo
kuangalia gharama zipi atakazoingia baada ya tukio hilo.
Huyu ni mtu ajali anakokwenda anaamini anakokwenda
yuko tayari kukabiliana na jambo lolote ili mradi tu lile alilokusudia
linafanyika kwa ubora wake na kiufasaha au kwa muonekano wa kawaida anaonekana
kanakwamba ajali ya maisha yake bali ni kile kilichomzidi kinachomlevya.
Huyu ni mtu ambaye apatiusaidizi wa dunia( elimu,
heshima yake na msaada wake) bali atapingu iko nyuma yake katika kuyafanikisha
yale yote yaliyo kusudiwa kwa nguvu na msaada wa mbingu.
Nguvu ya mtu huyu inasimama yenyewe na inafanya kwa
ubora wa hali ya juu sana kwani hakuna kitu kingine kinachoweza kupingana na
nguvu hiyo asili ya nguvu hiyo haina hali ya kushindwa imeshikiliwa na mbingu
na tayari kwa ushindi na sio kwa kushindwa.
Mtu huyu amebeba dhamana ya mbingu ambayo
inamshikilia pasipo kuchoka wala kumuacha kwakua yeye ndio makao ya hiyo mbingu
yohana 14: 23
Hauhitaji kumsiliza ili uamini bali muonekano wake
tu utaona mbingu inashuka na kumfunika........na inadhihirika sana katika
utendaji wake kwakua ni Mbingu itakuwa ikitembea badala yake.
Imeandaliwa na;
Cothey Nelson...................................................................0764
018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni