Jumatatu, 9 Machi 2015

JIFUNZE KUSAHAU



JIFUNZE KUSAHAU na sio kupotezea!



KUSAHAU NI ZAIDI YA KUSAMEHE

Uwa hakuna ulazima wa kujifunza kitu ambacho sio kigumu au kinaeleweka kwa wote au kwa urahisi pasipo usaidizi wa mtu mwingine,na ni wazi pindi unapojifunza kitu uwa kinakuwa sio kigumu tena…….mathalani mtu anayejifunza kuendesha inawezekana hapo awali aliona kuwa ni kitu kigumu sana japo nae alikuwa anatamani ndani yake lakini baada ya kujifunza uweza kuona uwezekano wa kujua zaidi na mwisho uona kuwa ni kawaida sana.

Hili ni jambo ambalo watu wengi utamani kuwa nalo, japo naamini yapo ambayo binadamu yeyote ambayo apendi kuyasahau na yapo ambayo uweza kuyasahau……….lakini twende mbele na kurudi nyuma tambua kusahau kutokana na uwezo wa ubongo mtu husika sio kitu rahisi labda awe na shida katika ubongo wa mtu husika.

Ningependa kusema kuwa kusahau ni chanzo kimoja wapo katika kufanya mambo kiufanisi zaidi na uwanja mzuri katika kujenga kitu chema katika akili yako(ubongo) wako watu wanapita katika kipindi kigumu sana kwa sababu hawataki kusahau bali utaka kubaki katika kumbukumbu katika ufahamu wao na ni wazi inakuwa teso baada ya kuwa Baraka………..ninge penda ujue kwamba yako mambo ukiyakumbuka au kusahau hayaletishida katika akili yako ila yako mambo ambayo pindi unapoyakumbuka yana haribu hata utendaji wako wa kazi na kufanya kazi kuwa ngumu hata kama ilikuwa nyepesi.

Kulia kila siku hii ni ishara kubwa sana ya mtu kutotaka kusahau au kutoona umuhimu wa kusahau au kutojua kwanini nisahau, siwezi kukataa baadhi ya matendo yaliyo athiri yanaweza baki katika mwili wako na kuweka alama ambayo kila ukiyakumbuka yanarudisha nyuma kukupeleka katika lile tukio ambalo likasababisha jambo hilo litokee….na jua katika mazingira haya kusahau inakuwa ni ngumu tu kwani ukiangalia yale uliyokuwa ukiyafanya hauwezi kuyafanya tena mathalani ulemavu.

Wako waliofanikiwa katika maisha yao kwa kukubali kusahau na kujikubali na hali waliyonayo na kuanza kufanya jambo ambalo mwisho wake likawa Baraka katika maisha yao, kwa mtu huyu ana fikiria katika yale yanayomkabili kuliko yale yaliyomkabili………..najua kuna wakati unaweza kupitia jambo ambalo kwa kiasi kikubwa likachanganya akili yako kwa kiasi kikubwa sana lakini ujajua hatima yako inaweza kuwa kubwa kuliko ilo jambo linalo kukabili au lililo kukabili.

Lazima utambue ikiwa kweli unamtumikia Mungu na wala ndani yako hakuna unafiki jua mazingira ,teso shida na hata hadha sio Mungu japo yeye anaweza kuyaruhusu kufanya jambo likawa Baraka katika maisha yako kuliko vile unavyofikiria.

Imeandaliwa na;

        Cothey Nelson…………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni