Ijumaa, 13 Machi 2015

UZURI USIO HARIBIKA



UZURI USIO HARIBIKA


Uzuri ni kitu au jambo au ni hali? Yote haya ni maswali ambayo mtu anajiuliza pindi anaposikia neno hili……..wako wanazuoni na wataalamu mbalimbali wanajaribu kutoa maana ya neno hili UZURI wengine wa kimaanisha ubora au hali ya kung’aa au hali ya kustahimili au kushamiri katika yote… haya bado kuna maswali ya watu na utofauti wao katika kunyambua hili neno………na sijui wewe msomaji wangu pindi unaposikia neno hili sijui akili yako inapata picha gani? Au dhana ipi lakini yote nakuachia wewe!

 Ki kawaida hili ni neno zuri ambalo pindi unapolisikia mtu anakwambia basi moyo wako unakuwa na changamko la furaha mathalani mtu akikwambia wewe ni mzuri au umefanya jambo Fulani ukaambiwa umefanya vizuri! Ni wazi moyo wako utajawa na furaha sana….na sijajua neno hili mzuri uambiwa wanawake tu au hata wanaume na kama wanaume wanaambiwa katika muktaza upi au kwa dhana iliyo sawa na mwanamke katika muonekano ulio bora na wenye kung’aa.

Ni wazi kila mtu anapojitazama ujiona kuwa yeye ni mzuri japo naamini kuna watu wakijiangalia kwenye kioo wanaweza kusema wao ni wabaya inawezekana kwakukosa maboresho au vile anavyojiona au vile alivyoambiwa, na amini hata Yule mwenye kujiona sio mzuri sana huwa apendi kuambiwa kuwa yeye ni mbaya……..vilevile kwa mtu asiyejitambua kunakipindi anaweza kuambiwa yeye ni mzuri akakubaliana na hali hiyo kwa asilimia zote na pia kunakipindi anaweza kuambiwa kuwa yeye ni mbaya bado akakubaliana na hali hiyo kwakuamini kuwa mwanzo alikuwa mzuri na sasa amekuwa mbaya akakubaliana kuwa kuna mabadiliko.

Pia katika haya yote tukumbuke kuwa kuna uzuri wa ndani na uzuri wa nje yaani upo uzuri usio onekana na uzuri unaoonekana, lakini ningependa sana kuuzungumzia uzuri usio onekana kama ndio matokeo ya kunawirisha uzuri unaonekana, na ni wazi unapo ujali uzuri wa ndani basi uzuri wa nje utakuwa unaujali sana japo inawezekana kwa kujua hama kutokujua.

Na uzuri wa Mungu unanawilishwa na ufalme wa Mungu ukaao ndani yako katika kufanya maboresho na ushamiri wa makazi ya ki Mungu katika himaya yako ya ndani katika kutoa muungozo wa uzuri wako wa nje, kwakusema hivyo uwa si maanishi watu wa sijigharamie katika mapambo yao ya nje ila fanya yote kuustawi wa muonekano wako kuwa vyema.

Ila niseme kitu kuwa muonekano wako wa nje utegemea sana na muonekano wako wa ndani kwakua tunaona watu mambo yanapo wachanganya hata muonekano wa nje ubadilika kabisa na hali ya kutojijali uanzia hapo.

Lakini ukiutunza uzuri wako wa ndani kwa kuhakikisha maamuzi yako yote yanamleta Mungu kuzidi kujengeka katika utu wa ndani bila shaka Mungu atawezesha kuyamudu mazingira yote ya nje yasiweze kuharibu uzuri wa ndani na wanje.

Imeandaliwa na;
Cothey  Nelson……………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni