Jumatano, 31 Desemba 2014

KUNATOFAUTI KUBWA KATI YA MIEMKO YA MWILI NA NDOA





KUNA TOFAUTI KUBWA KATI YA  MSUKUMO WA NDOA 
 ( MIEMKO YA MWILI) NA NDOA YENYEWE!!!




Ni kweli jambo lolote ambalo unaliingia ni wazi kabisa lazima uone haja ya jambo hilo na endapo hutaona haja ya jambo hilo ni wazi hautaitendea haki hali yako na nafsi yako binafsi. Ni kweli ndoa ni jambo la heri sana lakini ni pale tu utatambua kwa usahihi uku ukisaidiwa na Mungu mwenyewe katika kukuwezesha kuyafikia yale uliyo yakusudia.

Katika dunia ya sasa ndoa nyingi zimekuwa ni safari au mapitio tu lakini sio maisha ya wawili hao ya milele, tumekuwa tukishuhudia harusi kubwa lakini mwisho tukiona upweke ukiendelea kuthibitika au watu wakiama kutoka kwa mtu mmoja na kwenda kuanzisha ndoa na mtu mwingine, watu wengi wamekuwa wakiishi katika ndoa kwa misingi mfumo wanaojua wao mathalani mfumo dume, mila na desturi.

Vijana wengi wanaona kuwa sio rahisi kuishi pasipo kuwa na mwenzi ili kuweza kupunguza makali ya mwili au kwenda sawa na miemko ya mwili inafika kipindi ambacho watu hawaaminiani wala kukubaliana kuwa kunauwezo wa kuvimudu vishindo vya mwili katika mabadiliko yao. Wako watu katika kupunguza miemko yako katika mwili katika kwenda kwa dada poa( changudoa) na wengine kutokana na kuogopa maradhi mbalimbali wamekuwa wakishaurina kuwa basi waoe ili waweze kumudu miemko yao katika miili yao.

Niseme wazi miemko katika mwili ni muhimu sana japo sio kigezo cha wewe kuingia katika ndao ningependa kusema kuwa miemko katika mwili wako ni ishara tu mwili wako kujiweka sawa kutokana na hatua uliyonayo kwani kuna hatua ya watoto kuna kuota meno na mengine mengi lakini kuna hatua ujana katika kuimalika na homoni kujipanga katika hali stahiki ni kitu kizuri sana hivyo napenda sana kusema miemko ni maandali yaliyo katika mwili na sio kigezo cha maandalizi ya ndoa, maandalizi ya ndoa yana husisha maandalizi ya AKILI na UCHUMI na sio mabadiliko ya mwili.

Tumeona ndoa nyingi za watoto wakiingia katika ndoa pasipo kujua wapo katika ndoa bali msukumo wao mkubwa unategemea sana msukumo wa mwili katika kuingia katika ndoa, niseme wazi ndoa ni zaidi ya adhabu ya kihama endapo hauta ielewa au hautua kubali kuelewa inaweza kuwa ni zaidi ya majanga lakini ukiingia katika hali stahiki inakuwa nizaidi ya asali au chochote.

Lakini watu wengi wamekuwa wakiingia katika ndoa kutokana na ushauri na rafiki wanaowazunguka katika kuwaambia kuwa mmeshakua mnafaa kuishi na mwanamke na wanaweza kukuaminisha kuwa utaweza tu tena wengine wanaweza kukusifia kwa upeo ulionao.

Nipende kusema kuwa mabadiliko ya mwili ukuanza wewe na wala Mungu akuweka mabadiliko ili uingie katika ndoa.

Lazima ujue miemko ni ishara ya kukua lakini sio swala la kusukma kuingia katika ndoa kwani inaweza kuwa ni jambo zaidi ya hatari kwakua KUJUA KUSIMAMA SIO KUJUA KUKIMBIA.
Ni wazi swala zima la ndoa lina muhitaji Mungu kupita kawaida unavyofikiria na hasa katika dunia ya sasa ilijaa mlundikano wa maisha yasiyo kuwa halisi na wenye ustawi uliokusudiwa.

Miemko ni radha katika ndoa ambayo inaweza kukupa raha kuona uhitaji wa mwezako katika ndoa katika wakati sahihi lakini sio swala la kukuumiza kichwa likaondoa usingizi likaondoa kiu yako na Mungu au bidii katika elimu yako, ni pende kusema kuwa jambo sahihi uja kwa wakati sahihi unahaja ya kukulupuka.


Japo sio kauli nzuri sana kwako lakini kwangu ni nzuri sana inayonipa nguvu NDOA ONA KAMA KIFO.............kama kipo kipo kitakuja tu, kwani kuna mtu anaweza kukikimbilia kifo na kukifurahia ila kama kipo kipo tu.


BARIKIWA RAFIKI!!!!!!!!



 Imeandaliwa na;
      

                          Cothey Nelson....................................................................0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni