UMASIKINI WA MACHO;
Siku zote macho yanaweza kukutia nguvu au kukufanya
dhaifu, hali hii inatokea mtu binafsi anapoona mwenyewe hali ya kutoweza au
kuogopa na hata kama watu wanaweza kuona tofauti na vile mtu anavyoona.
Kwasababu kile anachokiona mtu ndicho kinachokuwa na nguvu katika kutawala
katika maisha yake.
Ukiweza kuyaponya macho yako kuona tofauti na hali
ilivyo au namna unavyotakiwa kuona basi hapo ndipo kunakushinda au kushindwa,
watu wote walioweza kufanya mabadiliko katika dunia na jamii walikuwa na uwezo
wa kuondoa umasikini wa macho kwa sababu aliyaelekeza macho yake kuona upande
ulio mpelekea njia zaidi kuelekea upande wa kushindwa.
Kuna uwezekano wa kuondoa umasikini wa fikra au
akili sio rahisi kuondoa umasikini wa macho kwani umasikini mwingine uondolewa
na elimu mpya inayokukubaliana na akili yako lakini huu umasikini wa macho huu
unakuwa katika nafsi yako na pengine unaweza kuwa na mali nyingi lakini bado
ukawa na umasikini uliokushikilia katika macho yako.
Ninge penda ujue kwamba huu ni umasikini uliotanda
giza katika macho yako na hata kama ukitaka kuchukua hatua kutokana na akili
yako ilivyoelewa inakuwa shida kutokana na ukamilifu wa moyo katika kukubali
hali inakuwa bado ni ngumu sana.
Wakati mwingine umasikini huu wa macho unaondoa hali
ya bidii ndani yako na kuwa na shauku katika kufikia ngazi bora kuliko ulipo
japo wakati mwingine unaweza kutamani lakini katika kufanya maamuzi yaliyo
ubeba moyo inakuwa ni ngumu.na niseme wazi tu kuwa hali hii hakuoni mtu wala
hakujui mtu bali ni wewe pekee unayejihukumu na kuona ni mzigo katika maisha
yako na wala uwezi kuona fahari ya wewe kumwambia mtu mwingine kwakua hata huyo utafikiri kama atakuelewa na kukupa
pumziko ndani ya moyo wako. Utabaki nalo moyoni mwako litakua kama mzigo ambao
ujui kama ni mwepesi au ni mzito bali utaubeba.
Hali hii inabebwa na hali halisi katika upeo wa
macho yako yaliyo kidhi hali yako inayotakiwa katika kukufanya kuwa uwe chini,
ni wazi hakuna mtu anaipenda sana hali hii ila kunakuwa na shida kuwa kama hali
hii ni tatizo au ndio maisha tunayotakiwa tuishi hivyo siku zote.
Ilikuondoa umasikini wa macho lazima utambue WAZO LA MUNGU KWAKO.
Na sio wazo lako binafsi au wazo la watu wengine
wanaokuzunguka.Usihishi maadamu watu wanakaa duniani ndivyo wanavyoishi, bali
jitahidi kujua na kutafuta wazo la Mungu katika maisha yako ili ikutambulishe
wewe ni nani? Watu wengi utafuta kwa bidii kuwa na hali nzuri ya kielimu,
kufedha na mengine mengi lakini tambua kitu kimoja jinsi utavyojitmbua katika
kutambulishwa na Mungu hivyo ndivyo mazingira yatavyoambatana na wewe na sio
namna nyingine japo sipo mbali na kutia bidii katika kila jambo jema
unalolifanya.
Katika wazo la Mungu juu yako hapo ndipo
kunakusafishwa kutoka katika umasiki wa macho na kuwa utajiri wa macho uliojaa
utoshelevu wa kiMungu utakaoona wewe katika wakati sahihi na uliosimikwa na
Mungu mwenyewe.
Imeandaliwa na;
Cothey
Nelson............................................................................0764018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni