Jumamosi, 20 Desemba 2014

SIKU YANGU



SIKU YANGU;



Ilikwa ni siku ambayo sitaweza kuisahau na wala sihitamani kuikumba kwanamna ilivyotokea. Ilikuwa siku ambayo ilianza kwa furaha sana lakini mwisho ulikuwa tofauti na nilivyoitegemea hakika ilikuwa ni siku ya ajabu na kushangaza sana kwani ilianza kwa kusababisha furaha halafu mwisho ikiwa ni mateso............... nilikuwa na mdogo wangu tukielekea vijijini kwetu ambako tulikumbuka sana na tuna amini sana hata wao walitukumbuka sana pasipo shaka........kwani  wazazi wetu walipiga simu na kuwataarifu ndugu zetu waliopo kijijini Mbeya  walijawa na shauku sana na tarajio kutuona.

Nasi tuliamka mapema sana mimi na mdogo wangu vick tuliamka asubui sana na wazazi wetu walitusindikiza mpaka ubungo na kututakia safari njema na umakini tuwapo safarini na kipindi hicho na kumbuka mimi na mdogo wangu tulikaa pamoja tayari kuelekea kijiji kwetu, na kumbuka safari ilianza asubui mnamo saa 12 asubuhi na kipindi hicho abiria wote walikuwa wamekaaa katika siti zao wakiwa watulivu sana kila mtu akiwa na mawazo tofauti katika kule alikuwa anaelekea wapo walikuwa wanaenda katika shughuli za kibiashara, kidini na kuwatembelea wapendwa wao kama sisi tulibeba hilo kusudi la kuwa salimu ndugu kwani mimi nilitoka mjini Mbeya ni kiwa mdogo sana yapata miaka 3 na sasa narejea ni kiwa na umri wa miaka 25.

Tulipofika Morogoro maeneo ya mbuga ya mikumi gari letu lilipata shida na kushindwa kuendelea na safari yake, hivyo abiria baada ya kusubiri kwa muda wakaanza kushuka taratibu katika kupata hewa nje.........ila mimi na mdogo wangu tuliofia kushuka chini kwani tulikuwa tunakumbuka yale maneno ambayo tulioambiwa na wazazi wetu tuwe makini sana pamoja na kuwa angalifu sana................ITAENDELEA!!!

Imeandaliwa na;

                      Cothey Nelson...............................................................0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni