Jumatatu, 8 Desemba 2014

KESHO SIHITAKI


KESHO INA NILILIA



Biblia inasema....lakini mtu huyu ndiye nitakaye mwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka atetemikaye asikiapo neno langu. Isaya 66:2b

Kulia ni jambo la kawaida katika dunia japo kuna kulia kwa kupenda na kulia kutopenda katika haya yote inabaki neon lile hili KULIA. Tena kubaliana kwa pamoja kuwa katika sehemu kubwa katika maisha ya mwanadamu uwa hawapendi kulia na katika kulia kunakuwa na sababu ya mtu kumfanya jambo hili.

Ni wazi kama jana haitakulilia sio jambo la kujivunia sana kwani kesho inaweza kulilia haya mambo uwa kwa sehemu kubwa na utaratibu au mfumo uliokuwako unakutengeneza au unaweza kuetengeneza au kuulekebisha.

Ni jambo lisilopingika mambo ambayo yanayosababisha kesho yako inaweza kutawaliwa na kilio sio kicheko japo inawezekana kuwa ulikuwa haupendi lakini uhalisia wake utajitokeza na kuchanua matawi yake;

I.umbali wa wewe na Mungu

Ninapozungumzia umbali wako na Mungu si zungumzi umbali unao onekana lakini nazungumzia umbali usionekana bali unauhalisia mkubwa na unadhihirika kwake ni mkubwa sana.

Ni bora uwe mbali na wazazi, walezi, marafiki,ndugu au jama wakiroho japo siku hizi mtu yuko radhi kuwa mbali na Mungu lakini awe karibu na marafiki,ndugu au mpenzi.

Uwezi ukawa mbali na mtu halafu ukategemea yale yake ya husike katika maisha yako hivyo unavyokuwa mbali na Mungu tegemea vya Mungu kupita mbali na maisha yako japo unaweza kuvipenda lakini utaratibu wake utasimama kama ulivyopangwa kwakila jambo la Mungu limebeba kusudi lake hivyo linafanya vile lilivyotumwa.

Kuwa na Mungu ni mbali na kusema mimi na mwamini Mungu na yupo kwakua naishi kwa nguvu zake bali kuwa karibu na Mungu ni zaidi ya chochote na vilevile sio swala la kuhisi tu bali ni udhihirisho ulio wa kutisha uliojaa mema mengi yanayo kuhusu wewe.

Mluhusu Mungu aitawale siku yako ili akutengenezee kesho yako iliyojaa matumaini isiyokoma na iliyokamilifu sana na iliyobeba ukamilifu usio pungua.

Na mluhusu vipi!-Nguvu ya sauti yake katika maisha yako;
Je katika maisha yako kipi kina nguvu kuliko kingine au cha maana sana kuliko sauti ya Mungu ndani yako, unahitajikujua kuwa kile unachokisiliza na kukikubali inatoa dira katika maisha yako inaweza kuwa dira sahihi au isiwe sahihi.

Je! Sauti ipi inatisha au ina nguvu kwako; mwenzi,mchumba,fedha,elimu au ushirika mwingine wowote!

Biblia inasema....lakini mtu huyu ndiye nitakaye mwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka atetemikaye asikiapo neno langu. Isaya 66:2b

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson.......................0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni