UNASIKIA NINI?
Unapoona mtu anafanya jambo lolote au kuongea jua
kama alijaanza ndani yake basi amesikia na kulikubali na kulifanya kuwa sehemu
ya maisha yake au kama sivyo basi kusikia kumechochea kitu katika kufanikisha
swala Fulani. Lakini leo siitaki kuzungumzia kusikia tu bali na zungumzia
unasikia nini kwakua kile unachokisikia kina mchango mkubwa katika maisha
yako............kwakua kwa sehemu kubwa mwanadamu ubadilika kutokana na kile
anachokisikia na hata kukiona.
Ni ukweli wako watu wanafurahia maisha yao leo
kutokana na kusikia jambo Fulani na akalifanya kuwa katika maisha yake na vilevile wako watu ambao wanalia sana
kutokana na kile alichokisikia sasa amekuwa na maumivu katika maisha yake, ni
kweli kusikia sio kitu kibaya bali swala unasikia nini! Na kwa nini umeamua
kusikia.
Sitazungumzia faida na hasara za kusikia bali
nitazungumzia namna kusikia kunaweza kukutengeneza kama vile ilivyokutengeneza
leo vile ulivyo, ukweli kuna mambo mengi yanafanyika kutokana na kusikia maneno
kutoka kwa mtu mathalani mtu anakuwa mke au mume wa mtu kutokana na maneno ya
mwenzi wake au mtu anaingia katika biashara haramu kutokana na kusikia kama
vile ukahaba, madawa ya kulevya na mengine.
Ni jambo la kawaida usitegemee kuwa watofauti na
jinsi vile unavyosikia kwakua kile unachokisikia ndicho kina kutengeneza wewe
na kuwa na nafasi ambayo uko nay oleo, wako watu ambao ni wakubwa sana katika
kiuchumi kutokana na kile walichokisikia kuwa katika maisha yao hivyo jua
mafanikio yako yame bebwa na nini ukisikiacho..........nikupe mfano mmoja kuna
ndugu na mfahamu alikuwa anapenda kufuatilia maradhi mbalimbali katika
mtandaoni ikatokea akavutiwa sana kuuelewa ugonjwa wa kisukari hivyo mwisho
akajikuta ule ugonjwa unaanza kushamiri katika mwili wake...........! narudia
tena sio swala la kusikia tu bali nini unasikia kinaweza kukufanya chochote
sawa na zima ya kile ulichokisikia.
Bila shaka umeona watu wakiwalaumu rafiki zao na
wengine wakiwalaumu wenzi wao japo sijajua wewe unaye soma ujumbe huu unamlaumu
nani au kumshukuru nani kwa kua lazima pawepo na mawili kati ya kulaumu au
kukshukuru kwa maana nyingine ikikosekana moja basi kunalingine litafuata
haiwezi ukawa tofauti na hapo! Kwa kusema hivi si chochei swala zima la
kulalamika au kuchukia bali mimi na zungumzi namna nguvu ya kusikia
ilivyobadilisha maisha yako.
PENDA KUSIKIA NENO LA
MUNGU WAKATI WOTE
Kwani hilo neno limebeba ustawi wa Mungu katika
maisha yako
Imeandaliwa na;
Cothey
Nelson..........................................................0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni