Jumanne, 8 Machi 2016

USISUMBUKIE NYONGEZA



USISUMBUKIE NYONGEZA



Nyongeza ni shukrani ya muuzaji au ishara ya kujali na  kukukaribisha kwa mara nyingine tena kwani wewe ndio maendeleo ya biashara yake au shughuli zake!

Nyongeza ni matokeo ya kununua kitu, na ukubwa au wingi wa nyongeza utegemea ukubwa au wingi wa bidhaa ulizonunua lakini kwa kiasi kikubwa utegemea maamuzi ya muuzaji, japo watu wengi wanapofanya manunuzi bila shaka utegemea nyongeza kana kwamba mtu aliyefanya kazi anadai mshahara wake na pindi anapokosa nyongeza uweza kusema moyoni mwake kuwa hapa sirudi tena!
Sikatai nyongeza inaleta raha katika moyo wako na kujua kuwa muuzaji anatambua na kuthamini mchango wangu katika shughuli yake au biashara yake.

Sikatai kitu kimoja kinachoweza kuwavutia wateja ni nyongeza na vilevile kitu pekee kinachoweza kuwapunguza wateja ni kukosa nyongeza, japo kuna maeneo unaenda na bila shaka unatambua kwa uhakika kuwa hapa hakuna nyongeza  lakini kuna bidhaa nzuri bila shaka itakulazimisha na kukushawishi kwenda na kupata hiyo bidhaa japo kunawezekana kuwa na punguzo ambalo unaweza kulifananisha na nyongeza kama ushawishi wa kuzidi kununua bidhaa hapo katika siku nyingine.

Japo kuwa nyongeza inaweza kutafsiriwa kama msaada kwa masikini kwani kunatofauti kubwa katika masikini anavyo lalamika na tajiri anavyolalamika kwani sauti zao ni tofauti na fikra zao ni tofauti kwani yuko mwenye uhakika atakama asipoongezwa bado anaweza kushiba vizuri na kutosheleza kiu yake lakini sio wote, maskini wengi pindi wanapokosa nyongeza na huku wakitegemea nyongeza basi hapo manung’uniko uweza kuufinika moyo wake.

Mathayo 6:  31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

                     32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

                    33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

                    34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake
Katika dunia ya sasa mambo mengi tunayoona dunia inavyoangaika na hivyo hivyo wana wa Mungu wanaangaikia, kila siku usiku na mchana, mateso yao yanazidi hata wamataifa kwakua hao dunia inawapatia bali walio wa Mungu wanasumbuka kwakua hawajaijua njia sahihi yakupata.

Maombi ya mtu anayesema anamwamini Mungu ndio anaomba mtu asiyeokoka mathalani utakuta mtu mtu anataja sifa za mwenzi anayetaka kuwa naye na hata kumshawishi Mungu aseme na mwenzi ambaye yeye anamuona kuwa anafaa.

Viko vigezo ambavyo kiukweli sio vya kweli kwa mtu kutambua mtu ananipenda kweli mathalani hataweza niruhusu nilale njaa, chochote nitakachomwambia  atakubali kwakua ananipenda, atajigharimu kwa ajili yangu tu kwa kila kitu, ataangalia mambo yangu na kuandaa mkakati wa kunisaidia, atahusika na maisha yangu kwanza, salama itatawala kwangu, nitamsumbua nione kweli ananipenda kama hataweza basi atakuwa ANIPENDI KWA DHATI, hivyo sitakubali kuwa mchumba wake.

Hali hii imepelekea kwa mtu kuwa mchaguzi sana na kushindwa kupata mahali atakapo dondokea patakapo leta raha ya kudumu katika maisha yake.

Mbali na hilo muonekano umekuwa ni tatizo kwa watu wengi kutokana jamii kuibua kitu ambacho kwa uhalisia hakina maana yoyote katika ndoa mathalani six parts, magari, hela za kutosha, asiwe mbaili,sexy(mwenye mvuto) lakini ukweli wanaujua walio katika ndoa kama hivi vyote vinamchango katika kuboresha ndoa au la!

Katika haza za kila siku mathalani mtu anapokuwa amepanga nyumba au chumba basi hapo kutokana na kero za mmiliki au jirani yake uweza kusema eheMungu nisaidie na mimi nijenge nyumba yangu na moyo wangu utatulia na kustarehe hayo mawazo kila mtu uweza kuwa nayo awe ameokoka au ajaokoka anaweza kuzungumza tena kwa machozi.

Unaweza kukuta mwanafunzi aliyeokoka anatumia njia zisizo halali ilikufauru mtihani wake mathalani kuandaa dhana ili kuweza kumsaidia katika mtihani ili pindi anaposhindwa aweze kutumia dhana hiyo kama mkombozi wake.

Jambo hili kwa kiasi kikubwa limetoa tofauti kati ya mtu anayemwamini Mungu na asiyemwamini Mungu kwani mwendo wao katika mambo mbalimbali umekuwa sawa tu wala hakuna utofauti wowote

Ni jambo ambalo ni teso la moyo wa Mungu kuona lilealilolikusudia limekuwa ni tofauti au kuwa kinyume kabisa na vile alivyokusudia kwani Mungu anatamani kuona moyo wako unaambatana na yeye lakini imeambatana na vitu vingine.

Mwanzo 6:6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo

Mungu kuna jambo analolitaka tulifanye katika kumwamini Mungu ili yeye ajidhihirishe katika maisha yetu kwani yeye Mungu anapenda kujidhihirisha kupitia sisi kwani ndio fahari yake kuona sisi tunamwelekeo uliojaa matumaini na uhakika katika njia yake sio ya ulimwengu huu.

Jifunze kwenda na wingu la Mungu na sio wingu la dunia japo ni ukweli mwili utaona uko nje ya mwelekeo uliosahihi lakini ni kuhakikishie kuwa hapo uko SALAMA. Ni kweli watatangulia lakini mwisho watakuhitaji na kuona wewe ndio mshauri wao mkuu.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni