NGUVU YA HAZINA
Unaweza kuona mtu
upenda kuchelewa katika mambo mbalimbali, unaweza usijue kwanini mtu
anachelewa? mathalani Ukiona mtu ananunua bidhaa alafu anasema chenji ibaki
ukouko hakuna shida,ukabaki na maswali kichwani? Au Unaweza kuona mtu anaangusha kinywaji alafu
anakiacha na kwenda kuchukua kingine, unaweza kuwa na maswali mengi pamoja na
majibu yako binafsi unaweza kuona mtu huyu ajaona alichododosha au aibu hama
anajiona?
Sikatai Ana B yanaweza
kuwa majibu lakini kuna uwezekani kuwa NGUVU YA HAZINA, kwa kiasi kikubwa
inawezakana kuwa siyo yeye bali NGUVU YA HAZINA inampa ujasiri wa kufanya kile
anachokifanya pasipo kuogopa huku akiamini kuwa kile anachofanya ndicho
anachotakiwa kukifanya na sio kingine ambacho wengine wanaona kuwa ni sahihi.
Unaweza kuona mtu
anasumbua mtaa, anachosha watu, anaboa watu analeta maswali katika kichwani mwa
watu lakini kubwa kumbe inaweza kuwa ni nguvu ya hazina inayomsukuma kufanya
kile anachokifanya na kuona ni sawa watu kumuongelea kwakua yeye anazo fedha na
wengine hawana(maskini) hivyo wacha wamuongelee yeye azidi kupeta, kwa kawaida
mtu wa namna hii upenda sana kupigiwa magoti na kumuona kuwa yeye anastahili
sana kuliko asiye hadhi yake!
Ukitaka kupata shida
kutana na mtu mwenye hazina yenye nguvu alafu hazina inamwendesha au
inamtaalakisha au inamsukuma kufanya mambo………….unaweza ona ni bora ukutane na simba
akakutafuna basi historia ya maisha yako ikaishia hapo kuliko kuishi na mtu wa
namna hii inakuwa ni zaidi ya mateso.
►Asante
karibu………………………….!!!
Tunafahamu kuwa hazina
ikiwa njema bila shaka maisha yanakuwa njema! Na furaha itokanayo na utoshelevu
utazani kumbikumbi wakati wa mvua basi bila shaka inaweza kuchomoza furaha
inayoambata na uwepo wa fedha.
Bila shaka namna
unavyoishi kwa kiasi kikubwa uweza kuamliwa na hazina uliyonayo ukiona mtu huyu
anapanda katika gari lake na huyu anapanda daladala hapo kunatokana na utofauti
wa uchumi kati ya mtu husika na kwa kiasi kikubwa kinachoamliwa hapo sio
kupenda bali hazina ya mtu.
HAZINA ni usalama wa
mtu katika kumudu mahitaji yake, hivyo ukubwa wa hazina ndio ukubwa wa kuimarika
kwake. Na bila shaka kila mtu upenda kuona hazina ikiongezeka na sio ikipungua.
Upaswi kupatashida
kuumia kuwa matumizi yamekuwa mengi bali ni vizuri kutambua kuwa shida yote
unayopata kwa kiasi kubwa ni kutokana na hazina kutotosheleza mahitaji husika.
Hivyo ni vizuri usipange safari ya kutoka kawe kwenda gongo la mboto (700)
wakati nauli yako ni kutoka kawe kwenda kariakoo tu (400).
Mathayo
7:24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa
na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
Mathayo 7:25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba
ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
Nazungumzia
hazina ambayo ambayo haijawaitokea ikakupoteza au kukuacha bali hii hazina
inaweza kukupa fedha, uzima, nguvu na maarifa na yote ambayo dunia haiwezi
kukupa kwakua yenyewe imebeba ukamilisho.
Hii hazina
ndio asili na ustawi wa hazina zote maana inakuwa imeshikwa na Mungu mwenyewe
na hakuna hawezaye kuharibu.
Mathayo 6:20 bali
jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi
hawavunji wala hawaibi;
Imeandaliwa
na:
Cothey Nelson……………………………………………0764 018535