Jumanne, 19 Julai 2016

NINI TATIZO?



NINI TATIZO?


Unaweza kukuta mtu anasema leo sijisikii kusema na mtu! au  Leo sijisikii kula chochote na huku haumwi au mabadiliko ya kibiolojia! hama Leo nataka niwe pekee yangu! au Leo sijisikii kupokea simu ya mtu yeyote wala kuingia katika mitandao ya kijamii!mh! Leo sitaki utani kabisa na mtu yeyote! Yaaani leo naomba mniache tu! Kwa kweli leo siku yangu haikuwa vizuri kabisa! Na mwingine ataenda mbali kidogo atahitaji dawa ya kutuliza maumivu ya kichwa! Na mwingine atasema Jamani leo mniombee tu maana moyo wangu siuelewielewi kabisa! Swali langu kwako  ni dogo tu JE! TATIZO NINI?

Unaweza kukuta mtu anatoa sababu ya kuvunja ahadi ya kukutana”samahani leo sijisikii vizuri kabisa” hata kama ni uongo atasema tu kwa sababu kuna kitu kime mvuruga ndani ya kichwa chake…mwingine atashindwa ata kwenda kazini na kutoa dharura ambayo haijaokoka maadamu apate tu aone mahali gani nitapata AMANI iliyotoweka ndani maana jambo hili silo la kawaida kwangu! Narudia tena nasema TATIZO NINI?

Unaweza kukuta mtu amekuwa bubu ghafla inawezekana mara tu baada ya kupokea simu au ya kutoka uko aliko toka na pindi utakapoanza kumuongelesha mdomo unaweza kuwa mzito na machozi yakatoa majibu yanaelezea hisia za moyo tafsiri ambayo ni ngumu kuielewa maana ni zaidi ya siri! Nauliza tena TATIZO NINI?

Unaweza kukuta mtu amefika chumbani kwake kajitupa ndani hanamaelezo kabisa ule ucheshi wake umepotea kabisa, lile tabasamu alipo tena na anaweza kujitaidi kukupa karatasi ikielezea yale aliyojibiwa na akapelekea kuamuru mwili wake kutoa maji yapitayo machoni! Nauliza kwa mara ya mwisho TATIZO NI NINI?

Ni kweli hali hii inaweza kukuta katika mambo mbalimbali ikapelekea kuwa na sura ambayo wewe mwenyewe kama ungajiangalia kwenye kioo ungejichukia sana….. inaweza kuwa ni tatizo la kifamilia au binafsi au jamaa ambao moyo wako ulimpa nafasi katika maisha yako kuwa ni rafiki yako hivyo lolote baya lililo mpata yeye wewe linakugusa kwa asilimia zote.

Karibu tuzungumze?

HIVI MNAPO AMUA KUVUNJA MAUSIANO YA KIMAPENZI NANI ALAUMIWE AU NANI NI CHANZO?
Je! Ni ninyi wenyewe? Shetani? Mungu? Ni nani wa kulaumiwa au hakuna wa kulaumiwa basi kama hakuna wa kulaumiwa sio vibaya mnaweza kupendana katika mwendelezo! Possible answer!
Wakati mwingine imekuwa ngumu kujua nani ni tatizo kwakua kila mtu atavutia kwake na kusema yule ni chanzo kwakua aliniambia mimi hivi! Na mwingine atasema yeye ndio chanzo kwakua yeye alinijibu hivi! Basi tukaamua hivi……..na maisha yanaendelea ni kweli hata kama msinge amua hivyo bado maisha yange endelea maadam uhai ungalipo.

 pindi mnapoingia katika ulimwengu huu mnakuwa mnaishi dunia nyingine inaitwa dunia ya wapendano na hapo mnaunganisha hisia zenu kwa ukali usio na maelezo ya kueleweka ila wenyewe mnaelewa sana kuliko maelezo.

Unaweza kuona mtu ana kuwa na huyu baadae anasema huyu anifai au moyo wangu ahujaridhika kabisa na baada ya kupumzika kwa kitambo kidogo anarudia tena na bado anasema bado moyo wangu haujapata tulizo lake! Hapa TATIZO NI NANI?  Unaweza kusema bado sio tatizo langu ila linaweza kuwa ni hisia zangu au la mtu mwingine.

Haya ni maisha ambayo hakuna mwanadamu anapenda kuishi maisha ya namna hii leo yuko na huyu na kesho yuko na yule na hata kufikia mtu mpaka anaoa au kuolewa mapaka anaanza kuwafananisha mtu aliye naye na mtu aliyewai kumjua mwanzoni.

Sikatai tatizo linaweza kuwa kwa mtu mwingine au kwako lakini lazima uchukue muda wa kutafakari sana kile unachokita katika akili yako ni kweli kipo na je! Hicho kinatengenezwa nawe au kinatengezwa na wengine na wewe unakitumia tu.

Ni muhimu kujiuliza kuwa kile kinachosemwa ni kweli kipo na kina uhusiano wa kweli na hayo mahusiano au kuna utofauti mkubwa na unajua kila hali inategemea na mtu husika.

Ninachoamini mimi kuwa UKIJUA KWELI UTAKUWA SALAMA NA UTASABABISHA USALAMA KWA WENGINE! 

Ni kweli hauwezi kuwaambia watu kitu ambacho wewe ukijui vizuri, kumlaumu mtu sio jambo jema ni bora ujitambue wewe binafsi kuweza kumudu mwili wako na ukiweka ustawi wa kudumu katika maisha yako na sio STAREHE ISIYO NA TIJA.

Katika hili uhitaji kuona Mungu akupendi au watu wanataka kukuchezea tu akili yako bali ni vizuri utambue USALAMA WAKO UNATEGEMEA UBORA WA AKILI YAKO!

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………0764 018535

TUNZA THAMANI YAKO!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni