Jumanne, 20 Septemba 2016

ULIYE KARIBU NAE!



ULIYE KARIBU NAE


Ni kawaida tu, ili kitu kiwe karibu na wewe, kuna uwezakano wa kuwa ni kitu kinachokuzunguka au wakati mwingine kinaweza kuwa ni kitu unachokiona kila siku pindi unapotembea au kukaa na hata unapofanya shughuli zako.

Ni kweli kabisa kuna mtu aliye karibu na wewe kwa maana anahusika na moyo wako na mwingine ujamusisha katika moyo wako ndomana jambo moja linaweza kuwa kuta wote lakini mwitikio wako utakuwa tofauti kwakua  utategemea nafasi yao  kwako.

Kwakua unaishi katika dunia ambayo ina vitu vingi mathalani miti, mabonde, milima, mito na maziwa yenye kupendezesha muonekano wa dunia na wenye tija katika maisha ya mwanadamu kwakua mwanadamu utumia maji na miti katika shughuli mbalimbali ili maisha yaende.

Japo binadamu tumezungukwa na vitu vingi vilivyopo dunia na vyeme mchango mzuri katika maisha yetu, lakini athari/matokeo yake haiwezi kuonekana mathalani katika kubadilisha tabia za mwanadamu kama alikuwa na asila basi awe na upendo na kinyume chake ni sawa!

Kwa kiasi kikubwa binadamu amezungukwa na wanadamu wenzake kwakua maisha yake yako mbali na wanyama pori wanapoishi japo wako watu wachache wanaishi misituni na kuzungukwa kwa kiasi kikubwa na miti, wanyama na milima na mabonde,

Japokuwa viko vitu ambavyo mwanadamu amezungukwa navyo lakini kitu pekee kinachoweza kuinua moyo, furaha, kusonga mbele, kuamasika, kupenda au kuchukia japokuwa viko vitu vingi  lakini kikubwa ni BINADAM mwenzake.

Kwa kiasi kikubwa utakuwa karibu na binadamu wenzako hata kama utakuwa unapenda mifugo kwa kiasi gani? Hama ulikuwa unapenda kilimo kwa kiasi gani naam hata gari au nyumba kwa vitu hivyo haviwezi kuongea na wewe katika lugha ambayo itakuwa rahisi kuielewa kwa haraka kama binadamu mwenzako akiongea.

Hivyo binadamu kwa kiasi kikubwa atakuwa karibu yako! Hivyo anaweza kufanyika changamko au huzuni katika moyo na wakati mingine anaweza kusababisha maswali katika ufahamu wako na kuanza kukufikirisha muda wote unapomuona na hata usipomuona.

Kama kuna watu/ mtu unatakiwa kuwa makini nae ni mtu uliyempa nafasi katika moyo wako( sio lazima awe mpenzi) na kumpa mambo yako nimeona uadui mwingi ukianzaia hapo kwa mtu uliye mwamini sana na hata kumuheshimu na baadae ukakuta ameweka wazi staha yako( siri) katika hali hii wako watu wamepata vilema vya maisha kama vile stroke, BP( blood pressure), vidonda vya tumbo na hata mtu kuwa na kichaa.

Katika michezo yoyote ogopa kucheza na mtu ambaye anakufahamu kwani uwa atumii muda mwingi anakuwa amesha upata ushindi mapema (ushindi asubui) na wakati mwingine ataukiwa una mazoezi ya kupambana na tembo au simba kama ujarekebisha mahali penye udhaifu huyo mtu wakati wote mpinzani wako atatafuta nafasi akuangushe kwa kugusa mahali penye udhaifu wako.

Mbali na Mungu………..mtu anayekufahamu ni JANGA kwako pindi mnapotofautiana unaweza kujikuta katika mazingira magumu sana ambapo ukuwai kuwaza kama utafika hapo mathalani mtu unaye fanya nae biashara kwa shirika( partnership) baada ya kujuana sana unaweza kukuta fedha zako zilizo kwenye benki hazipo na hatimae biashara ikafa na malengo yote yakawa mwisho.

Tukienda kwa upande wa usalama mtu yeyote anayesumbua kichwa sana katika uharifu lazima atakuwa mzoefu wa mahali hapo au mjuzi mzuri wa hayo mambo ndomana uweza kusumbua katika kupata utatuzi wa haraka.

Mtu anaye kufahamu unaweza kuwa ulipiga hatua kumi lakini ukajikuta unarudi hatua moja, ambayo kwa kiasi kikubwa itahitaji ukusanye nguvu tena katika kuanza hatua nyingine.

Kwa hakika aliye karibu nawe anaweza kuwa Baraka kwako au kuwa huzuni katika maisha yako!
Pamoja na yote bado neema ya MUNGU ipo kubwa sana katika kukupa mwendo pamoja na yeye kwakua huyo akiwa karibu yako na zaidi sana akiwa ndani yako basi UTAKUWA SALAMA!

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………………..0764 018535

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

Jumanne, 6 Septemba 2016

HAUHITAJI KUMLAUMU!



HAUHITAJI KUMLAUMU


unaweza kuwa binadamu wa ajabu sana hasa katika Dunia ya sasa, pindi utakapo dhulumiwa au kukosewa hama kusababishiwa kukosa jambo fulani ambalo unaweza ukahisi kama ungelifanikiwa pale basi ungelikuwa mbali au usingelikuwa pale ulipo sasa hama wengine kusalitiwa na kujikuta kuishi maisha ya lawama.

Kulaumu kwa kiasi kikubwa yamekuwa ni maisha ya watu wengi kwa ujumla wao waliofanikiwa hata wasiofanikiwa, katika ulimwengu wa sasa ni watu wachache sana utakao kutana nao ambao wasiweze kumlaumu mtu na mbaya zaidi wako watu wameenda mbali zaidi wanawaza kumlaumu hata MUNGU.

Wako watu wanamlaumu Mungu wakisema ni bora nisingelizaliwa kuliko kupata aibu hii kutoka kwa mtu huyu au kwa watu hawa kwani kule ningekuwa salama ninge kuwa na wewe(Mungu) na mimi tu maisha yangeenda sawa kwakua najua kamwe nisinge kuumiza kwa maana yote ungenitendea ni mema tu hivyo moyo wangu unge furahi siku zote kuliko kuwepo katika dunia hii iliyo jaa machafuko ya kila namna yasiyochafua moyo tu bali hata ngozi kudhoofika/kukunjamana.

Kikawaida neno hili kulaumu limekuwa kama haki ya mtu aliyekosewa hama kuonewa na pindi ukianza kumlaumu mtu aliye kuumiza watu hawawezi kukuona kuwa umekuwa MJINGA bali zaidi sana watakuonea huruma na kukupa moyo wakisema leo imepita ujui kesho Mungu amekuandalia fungu gani katika maisha yako hivyo uwe na moyo wa subira.

Pasipo kuficha uwa naona kuna mateso makali na maumivu makali sana pindi mtu anapoingia katika maisha ya lawama, kwani kiu ya maji inaweza kutoweka ghafla, njaa ikakimbia pasipo kujua imeelekea wapi? maana unaweza kuitafuta pasipo kujua hivi kwanini imetoweka mbona sijaiambia iende, pasipo kujua hayo ni matokeo ya lawama kuota mizizi katika moyo wako.

Na hakika naweza kusema kuwa hakuna kitu cha maana sana kama kuishi pasipo kuweka misingi ya lawama, kwani yanafanya maisha yako kuwa rafiki wa furaha,amani na upendo hivyo yanapelekea kuwa ni rahisi kutimiza lengo katika maisha kwakua bidii na ufanisi kutokana na utulivu wa akili katika utendaji upelekea urahisi wa kutimiza lengo lako katika njia iliyo salama.

Najua swali kubwa ni kwanini nisimlaumu wakati yeye amechangia kuharibu maisha yangu?
Ni swali nzuri na kwa mtu mzima yeyote lazima ajiulize swali kama hili? Lakini nami naweza kukuuliza hivi ukisha mlaumu nini unafaidika katika maisha yako kitakacho kupa hatua bora katika maisha yako ya rohoni au ya mwilini.

Unaweza kusema nitaishi maisha ya kumlaumu ili niirizishe nafsi yangu je! ni kweli ndio njia sahihi ya kuirizisha nafsi yako?

Nikubaliane jambo lolote ambalo aliupendezi moyo wako basi ni wazi litaumiza moyo wako na hatimae kukupa sababu ya kumchukia au ya kumlaumu kwa kitendo alichokufanyia.

Yesu alipokuwa anapigwa mijeledi na kuteswa mpaka kufa nafikiri huyu alikuwa na sababu ya kuwalaumu watu tangu alipo mkamata hata wakamjeruhi mwili kwa mijeledi iliyo lalua mwili wake na kufanya kuwa kitu kisicho thaminika, kumbuka yesu alikuja kwa ajili ya kuwakomboa wanadamu lakini hao hao wanadamu walimjeruhi na kuhakikisha mpaka anakufa,
Lakini katika yote …………. Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.( Luka 23:34).

Ni kweli kuiga kitu kinachofanywa na watu wengine ni jambo baya lakini sio kila kitu cha kuigwa ni sawa kwako hata kama stori zenu zinafanana kwa kiasi gani kila mtu kuna mahali alipotokea anachimbuko lake na anauelewa wake hivyo anautatuzi wake.

Niseme kuwa hakuna kitu kizuri kama uhuru wa ndani kwani uhuru ndio matunda mazuri yanayoonekana nje yanayooshesha kushamiri na kunawiri kwa nje! Niseme uhuru wa ndani unatuzwa na mtu husika kwani kama furaha anaipata mtu binafsi na maumivu anayapata binafsi hivyo sio kila watu wanavyo fanya ndio usahihi wa kufanya zaidi ya kutenda katika kuhakikisha uhuru wa ndani unakuwa ni maisha yako.

IPENDE HATIMA YAKO KWA KUUTUNZA MOYO WAKO NA UTUNZE MOYO KWA KUMPENDA MUNGU WAKO BINAFSI!
Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………..0764 018535