Jumanne, 20 Septemba 2016

ULIYE KARIBU NAE!



ULIYE KARIBU NAE


Ni kawaida tu, ili kitu kiwe karibu na wewe, kuna uwezakano wa kuwa ni kitu kinachokuzunguka au wakati mwingine kinaweza kuwa ni kitu unachokiona kila siku pindi unapotembea au kukaa na hata unapofanya shughuli zako.

Ni kweli kabisa kuna mtu aliye karibu na wewe kwa maana anahusika na moyo wako na mwingine ujamusisha katika moyo wako ndomana jambo moja linaweza kuwa kuta wote lakini mwitikio wako utakuwa tofauti kwakua  utategemea nafasi yao  kwako.

Kwakua unaishi katika dunia ambayo ina vitu vingi mathalani miti, mabonde, milima, mito na maziwa yenye kupendezesha muonekano wa dunia na wenye tija katika maisha ya mwanadamu kwakua mwanadamu utumia maji na miti katika shughuli mbalimbali ili maisha yaende.

Japo binadamu tumezungukwa na vitu vingi vilivyopo dunia na vyeme mchango mzuri katika maisha yetu, lakini athari/matokeo yake haiwezi kuonekana mathalani katika kubadilisha tabia za mwanadamu kama alikuwa na asila basi awe na upendo na kinyume chake ni sawa!

Kwa kiasi kikubwa binadamu amezungukwa na wanadamu wenzake kwakua maisha yake yako mbali na wanyama pori wanapoishi japo wako watu wachache wanaishi misituni na kuzungukwa kwa kiasi kikubwa na miti, wanyama na milima na mabonde,

Japokuwa viko vitu ambavyo mwanadamu amezungukwa navyo lakini kitu pekee kinachoweza kuinua moyo, furaha, kusonga mbele, kuamasika, kupenda au kuchukia japokuwa viko vitu vingi  lakini kikubwa ni BINADAM mwenzake.

Kwa kiasi kikubwa utakuwa karibu na binadamu wenzako hata kama utakuwa unapenda mifugo kwa kiasi gani? Hama ulikuwa unapenda kilimo kwa kiasi gani naam hata gari au nyumba kwa vitu hivyo haviwezi kuongea na wewe katika lugha ambayo itakuwa rahisi kuielewa kwa haraka kama binadamu mwenzako akiongea.

Hivyo binadamu kwa kiasi kikubwa atakuwa karibu yako! Hivyo anaweza kufanyika changamko au huzuni katika moyo na wakati mingine anaweza kusababisha maswali katika ufahamu wako na kuanza kukufikirisha muda wote unapomuona na hata usipomuona.

Kama kuna watu/ mtu unatakiwa kuwa makini nae ni mtu uliyempa nafasi katika moyo wako( sio lazima awe mpenzi) na kumpa mambo yako nimeona uadui mwingi ukianzaia hapo kwa mtu uliye mwamini sana na hata kumuheshimu na baadae ukakuta ameweka wazi staha yako( siri) katika hali hii wako watu wamepata vilema vya maisha kama vile stroke, BP( blood pressure), vidonda vya tumbo na hata mtu kuwa na kichaa.

Katika michezo yoyote ogopa kucheza na mtu ambaye anakufahamu kwani uwa atumii muda mwingi anakuwa amesha upata ushindi mapema (ushindi asubui) na wakati mwingine ataukiwa una mazoezi ya kupambana na tembo au simba kama ujarekebisha mahali penye udhaifu huyo mtu wakati wote mpinzani wako atatafuta nafasi akuangushe kwa kugusa mahali penye udhaifu wako.

Mbali na Mungu………..mtu anayekufahamu ni JANGA kwako pindi mnapotofautiana unaweza kujikuta katika mazingira magumu sana ambapo ukuwai kuwaza kama utafika hapo mathalani mtu unaye fanya nae biashara kwa shirika( partnership) baada ya kujuana sana unaweza kukuta fedha zako zilizo kwenye benki hazipo na hatimae biashara ikafa na malengo yote yakawa mwisho.

Tukienda kwa upande wa usalama mtu yeyote anayesumbua kichwa sana katika uharifu lazima atakuwa mzoefu wa mahali hapo au mjuzi mzuri wa hayo mambo ndomana uweza kusumbua katika kupata utatuzi wa haraka.

Mtu anaye kufahamu unaweza kuwa ulipiga hatua kumi lakini ukajikuta unarudi hatua moja, ambayo kwa kiasi kikubwa itahitaji ukusanye nguvu tena katika kuanza hatua nyingine.

Kwa hakika aliye karibu nawe anaweza kuwa Baraka kwako au kuwa huzuni katika maisha yako!
Pamoja na yote bado neema ya MUNGU ipo kubwa sana katika kukupa mwendo pamoja na yeye kwakua huyo akiwa karibu yako na zaidi sana akiwa ndani yako basi UTAKUWA SALAMA!

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………………..0764 018535

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni