Jumanne, 6 Septemba 2016

HAUHITAJI KUMLAUMU!



HAUHITAJI KUMLAUMU


unaweza kuwa binadamu wa ajabu sana hasa katika Dunia ya sasa, pindi utakapo dhulumiwa au kukosewa hama kusababishiwa kukosa jambo fulani ambalo unaweza ukahisi kama ungelifanikiwa pale basi ungelikuwa mbali au usingelikuwa pale ulipo sasa hama wengine kusalitiwa na kujikuta kuishi maisha ya lawama.

Kulaumu kwa kiasi kikubwa yamekuwa ni maisha ya watu wengi kwa ujumla wao waliofanikiwa hata wasiofanikiwa, katika ulimwengu wa sasa ni watu wachache sana utakao kutana nao ambao wasiweze kumlaumu mtu na mbaya zaidi wako watu wameenda mbali zaidi wanawaza kumlaumu hata MUNGU.

Wako watu wanamlaumu Mungu wakisema ni bora nisingelizaliwa kuliko kupata aibu hii kutoka kwa mtu huyu au kwa watu hawa kwani kule ningekuwa salama ninge kuwa na wewe(Mungu) na mimi tu maisha yangeenda sawa kwakua najua kamwe nisinge kuumiza kwa maana yote ungenitendea ni mema tu hivyo moyo wangu unge furahi siku zote kuliko kuwepo katika dunia hii iliyo jaa machafuko ya kila namna yasiyochafua moyo tu bali hata ngozi kudhoofika/kukunjamana.

Kikawaida neno hili kulaumu limekuwa kama haki ya mtu aliyekosewa hama kuonewa na pindi ukianza kumlaumu mtu aliye kuumiza watu hawawezi kukuona kuwa umekuwa MJINGA bali zaidi sana watakuonea huruma na kukupa moyo wakisema leo imepita ujui kesho Mungu amekuandalia fungu gani katika maisha yako hivyo uwe na moyo wa subira.

Pasipo kuficha uwa naona kuna mateso makali na maumivu makali sana pindi mtu anapoingia katika maisha ya lawama, kwani kiu ya maji inaweza kutoweka ghafla, njaa ikakimbia pasipo kujua imeelekea wapi? maana unaweza kuitafuta pasipo kujua hivi kwanini imetoweka mbona sijaiambia iende, pasipo kujua hayo ni matokeo ya lawama kuota mizizi katika moyo wako.

Na hakika naweza kusema kuwa hakuna kitu cha maana sana kama kuishi pasipo kuweka misingi ya lawama, kwani yanafanya maisha yako kuwa rafiki wa furaha,amani na upendo hivyo yanapelekea kuwa ni rahisi kutimiza lengo katika maisha kwakua bidii na ufanisi kutokana na utulivu wa akili katika utendaji upelekea urahisi wa kutimiza lengo lako katika njia iliyo salama.

Najua swali kubwa ni kwanini nisimlaumu wakati yeye amechangia kuharibu maisha yangu?
Ni swali nzuri na kwa mtu mzima yeyote lazima ajiulize swali kama hili? Lakini nami naweza kukuuliza hivi ukisha mlaumu nini unafaidika katika maisha yako kitakacho kupa hatua bora katika maisha yako ya rohoni au ya mwilini.

Unaweza kusema nitaishi maisha ya kumlaumu ili niirizishe nafsi yangu je! ni kweli ndio njia sahihi ya kuirizisha nafsi yako?

Nikubaliane jambo lolote ambalo aliupendezi moyo wako basi ni wazi litaumiza moyo wako na hatimae kukupa sababu ya kumchukia au ya kumlaumu kwa kitendo alichokufanyia.

Yesu alipokuwa anapigwa mijeledi na kuteswa mpaka kufa nafikiri huyu alikuwa na sababu ya kuwalaumu watu tangu alipo mkamata hata wakamjeruhi mwili kwa mijeledi iliyo lalua mwili wake na kufanya kuwa kitu kisicho thaminika, kumbuka yesu alikuja kwa ajili ya kuwakomboa wanadamu lakini hao hao wanadamu walimjeruhi na kuhakikisha mpaka anakufa,
Lakini katika yote …………. Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.( Luka 23:34).

Ni kweli kuiga kitu kinachofanywa na watu wengine ni jambo baya lakini sio kila kitu cha kuigwa ni sawa kwako hata kama stori zenu zinafanana kwa kiasi gani kila mtu kuna mahali alipotokea anachimbuko lake na anauelewa wake hivyo anautatuzi wake.

Niseme kuwa hakuna kitu kizuri kama uhuru wa ndani kwani uhuru ndio matunda mazuri yanayoonekana nje yanayooshesha kushamiri na kunawiri kwa nje! Niseme uhuru wa ndani unatuzwa na mtu husika kwani kama furaha anaipata mtu binafsi na maumivu anayapata binafsi hivyo sio kila watu wanavyo fanya ndio usahihi wa kufanya zaidi ya kutenda katika kuhakikisha uhuru wa ndani unakuwa ni maisha yako.

IPENDE HATIMA YAKO KWA KUUTUNZA MOYO WAKO NA UTUNZE MOYO KWA KUMPENDA MUNGU WAKO BINAFSI!
Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni