ANAONDOA ILI
UMTEGEMEE
Isaya 54:7 Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya.
Sio
kitu rahisi kutambua kuwa mtu huyu ananifanyia hivi ili na mimi baadae
nijitegemee binafsi hasa inapokuwa katika mtazamo usiopendeza machoni mwako
unaweza kuwaza kuwa anakuonea, amekuchoka hama hakuhitaji sawasawa na
mwanafunzi anapoadhibiwa kwa ajili ya utovu wa nidhamu au jambo lolote ambalo
mwalimu ataona njia nzuri ya kumrekebisha mtoto huyu ili baadae aweze kuwa mtu
wa maana katika jamii basi uamua kumuadhibu kwa fimbo, lakini katika kipindi
hiki picha zinakuwa tofauti kati ya mwalimu na mwanafunzi, mwalimu anaweza kukusudia
jambo jema lakini kichwani mwa mwanafunzi anaweza kuwaza mambo mengi kamavile
mpenda sifa, mnoko, hama uweza kumwita mwalimu wa mahasira.
Ila
inapotokea unatambua kuwa yote ananifanyia mimi ili kwamba nami wakati ukifika
niweze kujitegemea na hasa inapokuwa katika upande unao onekana vizuri
mathalani unafanya na mtu kwenye kampuni(mmilki) akakwambia jitahidi kufanya
vyema maana muda si mrefu nitakuachia hii kampuni iweze kuendesha maisha yako,
kwa maana rahisi wewe utakuwa ndio mmilki wa hii kampuni na mimi nitaenda
kufanya shughuli zingine!
Siku
zote mtu anapokuwa katika kipindi cha mpito na asijue kuwa hiki ni kipindi cha
mpito inakuwa ni shida sana, lakini kwa yule anaye pita katika kipindi cha
mpito na akaelewa kwanini anapitia hapo inakuwa ni ahueni kubwa kwake……..mathalani
mtu anajinyima kwasababu ya kutaka kufanya jambo kubwa hama kuna kitu amekianza
hivyo anajinyima ili kukamilisha hicho kwanza, inawezekana kuwa anajenga hivyo hali
hiyo upelekea kupunguza matumizi ya family/binafsi ili kukamilisha
alilokusudia,
Unaweza
ukajikuta una uhaba wa fedha(fedha hazitoshelezi mahitaji) ukapashida lakini
uwezi jua inawezekana kuwa ni Mungu
anataka kukupeleka katika kiwango kingine cha kumtegemea.
KARIBU!
Mungu
kama baba hama zaidi ya baba na hasa kwa mtoto wake ampendaye hawezi kukaa na
kuwaza jambo lisilo na faida kwa mtoto/mwanae, fahari ya mzazi ni kuona mtoto
anakuwa vile anavyotamani kuwa tena wakati mwingine ujitahidi kufanya kila
anachofanya ili kuhakikisha anatimiza ndoto ya mtoto wake kwa gharama yoyote
ataikibidi yeye kusimamisha mipango yake yote.
Luka 11:11
Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au
samaki, badala ya samaki atampa nyoka?
12 Au akimwomba yai, atampa nge?
13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu
mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana
kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?
Tatizo
kubwa kwa Mungu sio kukupa bali ni namna anavyokuandaa kuweza kukupa kitu
kitakachokuwa faida kwako na sio tatizo kwako, kitu kinaweza kuwa ni hichohicho
lakini usipokuwa na uwezo wa kukitumia vibaya
kitakuwa akina thamani na hapo Mungu apendi kufanya jambo kwa hasara.
Kumbuka
wanaisraeli walikuwa watoke misri kwenda kwa kanani kwa muda wa wiki mbili tu!
Lakini kutokana uwezo wao mdogo wa kuweza kumilki na kutumia tunu iliyopo
kanani ilibidi wachukue miaka 40 wakiwa safarini kuelekea kanani badala ya wiki
2,
Kinachosumbua
watu wa Mungu ni namna Mungu anavyokuandaa hama kuongeza hatua ya kumtegemea yeye kwa
hiyo hapa panakuwa na mtihani sana kwakua baadhi ya vitu uweza kuviondoa kwanza
kuipima akili yako je! Itafanya nini? Mathalani kukatwa mshahara, kufukuzwa
kazi, kipato kushuka katika biashara zako.
Na
wakati mwingi Mungu anavyokuandaa sio vile unavyopenda wewe hama vile mwingine
alivyoandaliwa bali inakuwa ni yanamna yako kwahiyo usipojua kuwa ni Mungu
anakuandaa unaweza kulaumu watu! Kuchukia na hata kusengenya.
Katika
mazingira hayo hapo uweza kuona mtu bidii yake kwa Mungu inapungua na asipokuwa
makini uweza kujikuta inapotea kabisa, lakini hali haitakuwa na nguvu sana
katika kuendesha maisha yako kama kweli UTAMJUA MUNGU!
Ayubu 22:21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo
mema yatakavyokujia.
Mtu anayemjua Mungu asumbuki kwasababu tu kipato kimeshuka hama
pesa hakuna bali upata tabu sana kuona Mungu hayupo. Ujitia nguvu kuona kama
Mungu ninaye basi vilivyo vyake vitakuja kwangu!
ANAITWA MUNGU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey
Nelson…………………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni