Jumanne, 29 Agosti 2017

TATIZO TUNDA!






Katika dunia ya sasa sio ajabu kwa mambo haya kutokea;

Ø  Watu walioamua kuwa mwili mmoja na kuapizana kuwa ni kifo tu ndicho kitakacho watenganisha lakini sio ajabu baada ya muda si mrefu unaweza kuta wameachana!

Ø  Unaweza kukuta vijana wenye lengo la kuoana ( wachumba) walio tayari na kutambulishana kwa wazazi wao na hata kuwekeana viapo kuwa mimi ndo wewe na wewe ndio mimi (upendo wa hali ya juu-kama kweli kinachosemwa kinatoka moyoni na kimebeba dhamira njema) na unaweza ukute wamepelekana makaburini, milimani, maporomoko ya ajabu na hata kwenye maji yenye kina kirefu wakidhihirisha upendo wao lakini utoshangaa kufumba na kufumbua upendo umekwisha wamekuwa kama mtu na jirani yake!

Ø  Pia unaweza kukuta watu ni marafiki tu wazuri(walioshibana) wanashirikiana katika hali zote lakini pamoja na hali hiyo sio ajabu muda si mrefu wakawa maadui wa kubwa.

Ø  Mbaya zaidi unaweza kukuta mzazi anamfukuza mwanae aliye mzaa na kumwambia “ sitaki ni kuone katika macho yangu” katika ulimwengu wasasa hili jambo ni swala linaloweza kutokea tu.

Sote tunatambua hakuna jambo linafanyika pasipo sababu labda mtu awe amejawa na mapepo na yana mwendesha katika kufanya mambo mbalimbali, miongoni mwa sababu hizo ni hali ya mtu kutopata kile anachokita ( matunda), inawezekana ni katika ujinga hama usahihi.

Kwani wako watu walio kuwa katika ndoa waliona fahari hama kupenda kuwa na watoto na ikatokea watoto kuchelewa hama uwezekano wa kuzaa kukosekana kabisa basi hapo uweza kuona hakuna maana ya ndoa, mbali na hilo pia kuna watu waliokuwa marafiki/ wapenzi wakiwa na matarajio fulani labda kusikia maneno mazuri kutoka kwa mwenzake hayasikii hama vitu na zaidi sana kujaliwa(kupetiwapetiwa) vyote hasipo vipata anaona bora awe na gogo kuliko kuwa na mtu kama huyo.

Katika karne ya sasa uwepo wako unatambulika baada ya watu kuona matunda yanayotokana na uwepo wako sio nyumbani tu, hata ofisini kile unachozalisha kinaweza mfanya mwajiri wako awaze mtu mwingine au kukuwekea mazingira bora ya wewe kuzidi kufanya kazi kwa ufanisi.

Hivyo popote ulipo/ mtu uliye lazima hautamani uwepo wako kwa yale yanayo zalishwa baada ya wewe kuwepo, hakika thamani yako inaongezeka kutokana na kile unachokizalisha.

Karibu ……………………………………………………………

Mungu naye unapokuwa katika himaya yake atapenda kuona matunda yake aliyo yaweka ndani yako yakitoka na kuwa faida kwa ulimwengu wote sawa na kusudi lake.

Na hii imekuwa tatizo kwa watu wengi hasa jamii ya waaminio kuona utofauti ulio miongoni mwao na kuibua chuki baada ya kujifunza/kusaidiana……..wapo watu wana onyesha uhai wao mbele za Mungu kwa kutumika kwa faida ya kristo hivyo Mungu husika sana na maisha yao kwakua wana ugusa moyo wake na wengine wanaona kama wanakandamizwa pasipo kujua kuwa wanapaswa kutoa matunda yanayo faa .

Hata Mungu upenda kuona mtu anatoa matunda ambayo yeye aliyaweka ili aendelee kukutunza na kama hautoi matunda aliyo kusudia anaweza asione haja ya kuendelea kukutunza na hapo ndipo unaweza kuona hali ngumu ukiwa kama mwamini.

Yohana 15:1 Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
                   2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.
 
Ili ukae mahala popote na mtu yeyote hasa mwenye akili njema jaribu kuzalisha matunda ambayo yeye anayategemea toka kwako ili azidi kuufurahia uwepo wako na kuzidi kuhusika na maisha yako,
 
INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………........……………0764 018535

Jumanne, 22 Agosti 2017

NGUVU YA UTULIVU.







Utilivu ni moja ya hali inayopendwa na watu wengi kama sio wote, hutoshangaa ukisikia maneno toka katika kinywa cha mtu akisema  “ ningepata sehemu nzuri yenye utulivu wa kutosha ni pumzike nafikiri akili yangu itakuwa vizuri ”….. watu wengi wamekuwa wakiamini kuwa kama wakipata eneo zuri la utulivu na hatimaye akapumzika anajua mwili wake utakuwa katika hali nzuri na kuzidi kuimarisha afya yake.

Na wako wanao jikuta hawa pumziki vizuri sio kwa sababu sehemu sio nzuri bali ni kwa sababu ya kukosa utulivu unawezekana ukawa ni utulivu wanje au wa ndani,

Ni muhimu kutambua kuwa na UTULIVU katika jambo lolote sio lazima mazingira yawe yametulia, mazingira yanaweza kukosa utulivu kabisa yaani yamechafuka sana lakini wewe unaweza ukawa na utulivu wa kutosha sana endapo tu utatambua SIRI ILIYO KATIKA UTULIVU.

Ina aminika kuwa jambo lolote linalokukabili unapoingia katika utulivu kuna utatuzi/maamuzi ya busara yatatoka hapo, japo sio kila utulivu utapelekea maamuzi ya busara au ya maana kwakua wakati mwingine utegemea kinachoendelea ndani yako na kilicho ujaza moyo wako.

UTULIVU KATIKA MUNGU KAMA NJIA SAHIHI YA KUFIKIA HATMA YAKO?

Ni muhimu kutambua kuwa hatuwi watulivu kwasababu tunashida au tuna uhitaji fulani, huu sio msingi mzuri wa kutulia bali tunakuwa na utulivu ndani kwakuwa Mungu anataka tuwe watulivu maana yeye ndiye mleta utulivu.

Unapofanya utulivu kuwa ni maisha yako unakuwa na nafasi nzuri katika utatuzi uliobora kuliko kuanza kujikunja na kutafuta utulivu katika hali mbaya au mazingira magumu hali hii uwezi kushangaa mtu kuibuka na maamuzi ambayo Mungu, shetani na hata wanadamu watashangaa.

Tunapozungumzia utulivu  ni kitu cha kawaida sana, lakini neno hili unaweza usione maana pindi utakapo kosa sababu kutulia katika jambo fulani, na wakati mwingine unaweza kuona njia nyingi za kufanya kuliko kutulia japo baadae zinaweza kukugharimu,

Hali ya kutulia mbele za Mungu katika jambo lolote alijarishi hilo jambo ni kubwa hama ni zito kiasi gani Mungu atakupa njia rahisi ya kutoka hapo!

Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

Mungu akishikilia hisia zako na kukupa utulivu katika akili yako na kuweka mwanga katika macho yako moyo wako ili uweze kuona ile picha kamili iliyojaa utoshelevu wako katika yeye.

Eneo atalikiwa ni la namna gani aliwezitoa utulivu ulio bora kama utulivu ulio jikita katika Mungu maana yeye atakupa utulivu wake, akili yake na hatimaye kupata njia ya kupita.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………..0764 018535