UTATUZI KATIKA UHITAJI
UHITAJI! UHITAJI! UHITAJI
Hakuna kitu kizuri sana kama uhitaji na hakuna kitu kibaya
sana kama uhitaji lakini vyote
ukutegemea wewe!
Unaweza kuona mtu akilia baada ya kupata kitu na unaweza
sikia akisema “ ilikuwa ndio hitaji na lilisababisha
nitoe machozi kila siku”………………………………!
Na mwingine unaweza kukuta anasema “ uhitaji wangu ndio
ulioniponza”
Amani hama tumaini la uhitaji utegemea sana uhakika wa
utatuzi,
Sio kila njia unayoitumia katika kutatua tatizo ndio njia
sahihi ya kutatua tatizo wakati mwingine unaweza hisi unatatua hama unalimaliza
jambo kumbe ndio unaanzisha jambo jingine ambalo linakwenda kuwa zaidi ya
tatizo na hata kufuta maana ya wewe katika kujitahidi.
Moja ya kitu kinachodhihirisha kwamba huyu mtu anajielewa ni
namna anavyoshughulika na uhitaji wake.
Mtu mwenye akili au mtu aliyepitia hatua hiyo pindi
anapomuona mtu anavyo shughulika na uhitaji wake uweza kugundua na kusema kuwa
sasa huyu mtu anajielewa hama anapotea.
Japo katika uhitaji ( kwa maana ya jumla ) kuna uhitaji
katika mambo ya msingi ( basic needs ) na uhitaji katika mambo yasiyokuwa ya
lazima ( luxury needs ).
Namna unavyoshughulika na uhitaji wa aina zote uweza
kuonyesha uimara/ uwezo wa akili yako katika kuyamudu mambo yanayokukabili.
Uhitaji wa watu wengi umefanyika maafa kwao, kwani watu wenye
uwezo wa kukupa/ kutoa hama kusaidia watu, wengi wao wametumia nafasi hiyo
kuumiza maisha ya wengine katika kuweka maslahi yao zaidi.
Kama ni mtihani basi utakuwa ni mtihani utakao endelea kuwa
sumbua watu wengi duniani namna ya kupambana na uhitaji wao, kwakuwa unaweza
ukakidhi leo uhitaji wako kwa njia moja lakini kesho kwa njia hiyohiyo
ukashindwa (fail) na hapo ndipo panic na kichwa kuuma uanzia hapo ( mawazo
yasiyo kuwa na kikomo ).
Ni muhimu ufahamu wako uwe umenolewa vizuri ili kukusaidia
kumudu changamoto zilizopo na zitakazo kuja kwakuwa utatuzi wa kesho ni bora
zaidi kuliko utatuzi wa leo. ( kama ulishiba jana alafu leo kukawa hakuna
chakula basi hapo ujue shibe ya jana hauta ikumbuka/ kuionea ufahari )
Kwakuwa haiwezi kuwa na maana kama jambo ulitatua jana alafu
leo likakushinda mathalani unaweza kukuta binti anasema mimi mwanzo nilikuwa
makini sana atanikaweza kumudu vishawishi nisipate mimba lakini alitokea kijana
mwenye maneno ya ajabu yakanivutia hatimaye nikapata mimba baadae yule kijana
akanitelekeza ( ni kweli inakuwa ni stori lakini inakosa maana sana kwakuwa
haionyeshi ushujaa wako).
Kama unataka kuwa na maisha yenye ushuhuda/ yenye
kumdhihirisha Mungu usipende vitu vilivyo rahisi rahisi, penda kutumia vizuri
akili yako ( akili ni pana sana na kuongezeka kwake inategemea namna
unavyoishughulisha ). Ili baadae ujivunie jasho lako.
“ uwa hakuna maana ya jana kama leo haionyeshi ushuhuda wako
“
Uhitaji upo kwa kufanya akili aliyokupa Mungu ikusaidie na
Roho mtakatifu kuonyesha ubora wake na sio kuleta maangamizi.
“ mtihani haupo ili ufeli (ushindwe) bali kupima uwezo wa
akili yako katika kukumbuka, kuchanganua na uelewa wako!”
INAITWA SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson………………………………………..0764
018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni