Jumanne, 5 Desemba 2017

UHITAJI WANGU!



UTATUZI KATIKA UHITAJI

UHITAJI! UHITAJI! UHITAJI

Hakuna kitu kizuri sana kama uhitaji na hakuna kitu kibaya sana  kama uhitaji lakini vyote ukutegemea wewe!

Unaweza kuona mtu akilia baada ya kupata kitu na unaweza sikia akisema  “ ilikuwa ndio hitaji na lilisababisha nitoe machozi kila siku”………………………………!

Na mwingine unaweza kukuta anasema “ uhitaji wangu ndio ulioniponza”

Amani hama tumaini la uhitaji utegemea sana uhakika wa utatuzi,

Sio kila njia unayoitumia katika kutatua tatizo ndio njia sahihi ya kutatua tatizo wakati mwingine unaweza hisi unatatua hama unalimaliza jambo kumbe ndio unaanzisha jambo jingine ambalo linakwenda kuwa zaidi ya tatizo na hata kufuta maana ya wewe katika kujitahidi.

Moja ya kitu kinachodhihirisha kwamba huyu mtu anajielewa ni namna anavyoshughulika na uhitaji wake.

Mtu mwenye akili au mtu aliyepitia hatua hiyo pindi anapomuona mtu anavyo shughulika na uhitaji wake uweza kugundua na kusema kuwa sasa huyu mtu anajielewa hama anapotea.

Japo katika uhitaji ( kwa maana ya jumla ) kuna uhitaji katika mambo ya msingi ( basic needs ) na uhitaji katika mambo yasiyokuwa ya lazima ( luxury needs ).

Namna unavyoshughulika na uhitaji wa aina zote uweza kuonyesha uimara/ uwezo wa akili yako katika kuyamudu mambo yanayokukabili.

Uhitaji wa watu wengi umefanyika maafa kwao, kwani watu wenye uwezo wa kukupa/ kutoa hama kusaidia watu, wengi wao wametumia nafasi hiyo kuumiza maisha ya wengine katika kuweka maslahi yao zaidi.

Kama ni mtihani basi utakuwa ni mtihani utakao endelea kuwa sumbua watu wengi duniani namna ya kupambana na uhitaji wao, kwakuwa unaweza ukakidhi leo uhitaji wako kwa njia moja lakini kesho kwa njia hiyohiyo ukashindwa (fail) na hapo ndipo panic na kichwa kuuma uanzia hapo ( mawazo yasiyo kuwa na kikomo ).

Ni muhimu ufahamu wako uwe umenolewa vizuri ili kukusaidia kumudu changamoto zilizopo na zitakazo kuja kwakuwa utatuzi wa kesho ni bora zaidi kuliko utatuzi wa leo. ( kama ulishiba jana alafu leo kukawa hakuna chakula basi hapo ujue shibe ya jana hauta ikumbuka/ kuionea ufahari )

Kwakuwa haiwezi kuwa na maana kama jambo ulitatua jana alafu leo likakushinda mathalani unaweza kukuta binti anasema mimi mwanzo nilikuwa makini sana atanikaweza kumudu vishawishi nisipate mimba lakini alitokea kijana mwenye maneno ya ajabu yakanivutia hatimaye nikapata mimba baadae yule kijana akanitelekeza ( ni kweli inakuwa ni stori lakini inakosa maana sana kwakuwa haionyeshi ushujaa wako).

Kama unataka kuwa na maisha yenye ushuhuda/ yenye kumdhihirisha Mungu usipende vitu vilivyo rahisi rahisi, penda kutumia vizuri akili yako ( akili ni pana sana na kuongezeka kwake inategemea namna unavyoishughulisha ). Ili baadae ujivunie jasho lako.

“ uwa hakuna maana ya jana kama leo haionyeshi ushuhuda wako “

Uhitaji upo kwa kufanya akili aliyokupa Mungu ikusaidie na Roho mtakatifu kuonyesha ubora wake na sio kuleta maangamizi.

“ mtihani haupo ili ufeli (ushindwe) bali kupima uwezo wa akili yako katika kukumbuka, kuchanganua na uelewa wako!”

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………..0764 018535


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni