Mahali / wakati ambapo unaweza kuona tabasamu la mgonjwa ni
pale anapoona anaanza kurejea katika hali ya uzima wake aliokuwa nao awali na hii
furaha uwa inaenda mbali hadi kwa wanao muuguza mgonjwa, kwani nao uwa na furaha
na matumaini uweza kuzidi kuimarika.
Na uzuri katika dunia tuliyonayo hakuna jambo ulilolipoteza
au uliloliona umelikosa lisiweze kurejea tena katika hali ya ubora zaidi na
mvuto wa kipekee maadamu tu unaishi.
Hichi ni kipindi ambacho majeraha na machozi ya moyoni
yanaanza kuwa adimu na furaha kuanza kuchipuka kwa namna nyingine.
Matendo 3:19 Tubuni basi,
mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako
kwake Bwana;
Na ni vizuri kukubali kuanza upya hata kama iki kugharimu kitu
gani kuliko kuendelea katika kukosea na maumivu.
Ni kama asubuhi yenye kuchipua tabasamu lililoadimika hama kupotea
kwa muda mrefu itakapo chipua hadi nywele na ngozi uweza kuhisi furaha.
Hakika ni kipindi kinachopendwa na wengi japo mchakato wake
usipokua mwangalifu unaweza usione kama kuna siku itafika ile raha uliyoipoteza
muda mrefu itarejea tena!
Kila mtu anarejesha furaha yake kutokana na jambo husika na sio
kila jambo tu linalomtokea mtu uweza kusababisha jibu katika maswali ya moyo
wake:
(a)
Wako watu waliokosa
watoto wakiwa katika ndoa zao kwa muda mrefu lakini pindi dalili za mtoto zilipoanza
na hatimaye kupata mtoto basi hapo furaha na shangwe uweza kuwa dhahiri na
mengine kubaki historia.
(b)
Pia wapo watu waliosota
sana katika kusoma na kupitia changamoto nyingi kiasi cha kupoteza matumaini
kama atakamilisha safari yao ya elimu inapotokea kufanikisha hazma yake (
kusudio la moyo wake ) basi hapo furaha isiyo ya kifani uzaliwa.
(c)
Inawezekana mtu
alikosa kazi kwa muda mrefu mara tu baada ya kuhitimu masomo yake hama alishawai
kupata kazi baadae akafukuzwa au kuacha mwenyewe baadae akapitia msoto mkubwa
kiasi cha kupelekea kujuta maamuzi ya awali lakini mwishoe akapata nafasi
iliyobora sana na hapo changamko la moyo uweza kuchipuka.
(d)
Sekta ya
mahusiano (sekta pendwa ) inawezekana ulipitia katika misukosuko mingi (
uliyoitegemea na usiyoitegemea ) na hata kutembea na wapenzi wako ili wafurahie
urembo wako ili waweze kutulia na wewe tu lakini mawazo yako haikuwa nia yao na
baada kufaidi uzuri wako waka kuacha solemba ( hewani pasipo kujua/kujali
utaangukia wapi ) pamoja na hayo bado ujana wako unaweza kuhuishwa kama tai na
kusahau jana, na kuipenda sana leo na kujiandaa kwa ajili ya kesho.
UREJESHO
WAKO UPO! NEVER GIVE UP.
INAITWA
SIKU! BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey
Nelson………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni