Ijumaa, 6 Desemba 2019

UZURI WA KUSUBIRI




“ subira yavuta heri” ni msemo uliozoeleka katika jamii! Na ulio na funzo ndani yake, japo ni kweli kwamba sio kila kitu unachosubiri kinakuwa na heri! Lazima utambue hicho unachosubiri kinasifa yakusubirika………….maana usije ukawa unasubiria yai viza ili upate kifaranga!

Karibu……………pindi unapomuona mkulima anachukua mbegu mathalani za mahindi na kuzifukia chini ( kupanda ) na kuondoka nyumbani kwake,pasipo kuwa na hofu au mashaka bali uwa na furaha sana hata katika uchovu wake, uweza kusikia raha katika mifupa na nafsi yake akijua subira yake itakuwa na matunda yatakayo rudisha nguvu yake na muda wake alioutumia.

Pia tunapomwangalia kuku ( wa kienyeji ) baada ya kutaga kwa hiari yake mwenyewe anayaatamia hayo mayai siku ishirini na moja ajali kuchelewa wala kuwai bali utegemea/kugonja miito ya watoto wake ( vifaranga ) pasipo kuchoka.

Vilevile uwa sipati picha kwa mwanamke wa kwanza kushika ujauzito sijui alikuwa katika hali gani aliyokuwa nayo kwa kile alichokibeba. ( kwakuwa apakuwa na muda maalum wa kusubiri, kwahiyo akujua wakati gani sahihi wa kukitoa kiumbe duniani )!

Napenda kukubaliana kuwa kusubiri sio jambo dogo , kwa maana wako watu walisubiri sana hata hatua ya mwisho lakini akakosa kile alichokuwa anasubiria naam hata asione tena maana ya kusubiri na wako waliosubiri mpaka mwisho lakini akashindwa kuvumilia hatimaye akakosa muujiza wake.

Moja ya sababu inayosababisha kushindwa kudumu katika kusubiri, ni hali ya mtu kuwa na subira yenye matumaini katika mwili mathalani hali ya kisasi-ngoja naye yampate tuone huo ujasiri ataupata wapi,  au wakati mwingine mtu kuwa na matarajio fulani kwa mtu mfano nilijua yeye atanioa hivyo inabidi nimvumilie hatakama hananidham amejaa kiburi wala anipendi najua atanioa maana najua moyo wangu umempenda,uwezekano wa kufanikiwa unakuwa ni mdogo.

Hama, Nimeishi katika ndoa miaka mingi nilijua ipo siku atatambua thamani yangu na kuanza kuniheshimu lakini wapi?

Nikubaliane kuwa moja ya kitu kinachoweza kufanya kushindwa kufika kileleni ni hali ya kushindwa kusubiri.

Naam sasa tuingie kwenye kiini cha somo “ uzuri wa kusubiri “ jambo lolote unalolisubiri lazima pawepo na raha ndani yako iliyobebwa na uhakika na maarifa uliyonayo au amani inayotokana na imani yako ( Ni muhimu iwe sahihi ).

Lazima uwe na uhakika wa furaha ya kweli kwa kile unachokisubiria na sio kwa wasiwasi wala mashaka.

Uzuri wa kusubiri ni njia rahisi ya kupata kitu sahihi kwa wakati sahihi japo kuna wakati mambo mengi yanakuzonga lakini moyo wa furaha katika hilo jambo ukupa maamuzi sahihi.

Hakuna raha katika kulazimisha jambo/mambo yatokee sawasawa na kuchuma  embe changa na kulivundika na uku ukitegemea liive na kuwa na radha nzuri.

Ni muhimu katika hali njema ya kusubiri utembee katika maongozi sahihi ( Mungu/Mtu ) ili ikurahisishie kufikia kile unachopaswa kuwa hama kuwa na hatua au nafasi unayotakiwa kuwa nayo!

INAITWA SIKU!BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………..0764 018535


Ijumaa, 1 Novemba 2019

ISHI KATIKA NDOTO YAKO!



Kuishi ni neema ambayo Mungu ametoa kwa kila kiumbe kilichokua hai.

Ninapozungumzia NDOTO! Katika muktaza huu Uwa sina maana mawazo yako ya siku nzima yanayojifunua usiku wakati umelala, bali ninazungumzia matarijio kamili ya Mungu katika kukufikisha kilele cha ustawi wako katika jambo Mungu ameliweka ndani yako.

Ni muhimu utambue kuwa kuna kuishi maadam unapumua, Napia  kuna kuishi kwa maana ya kuitumikia ndoto yako.

Hakuna maisha ya furaha kama ukiishi ndani ya ndoto yako, ni maisha yenye raha ni zaidi ya majigambo ya samaki akiwa majini.

Kama binadamu unaweza kutamani ndoto za wengine lakini kamwe usikubali kuishi humo kwani uwezekano mkubwa na kuangamia hapo upo! bali jifunze katika mema yenye mchango katika ndoto yako.

Unapoamua kuishi ndani ya ndoto yako hapo hakuna kushindana, manung’uniko wala majuto bali siku zote utaona deni la kufanya tu pasipo kuchoka.

Kuna maisha unayoweza kuishi ikapelekea ndoto yako kufa au kushamiri katika mwenendo wako wa maisha kila siku.

Moja ya kuwa faida katika dunia ni kuishi katika ndoto yako maana kwa kufanya hivyo itapelekea maana ya wewe kuishi duniani na utakuwa msaada kwa wengi.

Hauhitaji kuishi katika ndoto za wengine,kwani hali hiyo itapelekea kukosa mwelekeo unaweza kujikuta unafanya kitu ambacho akikuzaliwa ndani yako.

Moja ya sababu watu kuishi maisha ya mateso ni kuishi nje ya ndoto zao.

Ni muhimu utambue sio kila kitu unapaswa ufanye, bali ni kile kilichozaliwa ndani yako chenye tija katika ndoto yako na sio kuleta majeraha katika maisha ya wengine.

Mtu anayeishi katika ndoto yake uwa ajui nini maana ya kuchelewa katika hatma ya ndoto yako.
Usiruhusu jambo lolote hata liwe zuri kwa namna gani endapo utagundua litakutoa nje ya ndoto yako usifanye hata iki kugharimu kiasi gani au hasara ya muda fulani?

Unahitaji kujua kwamba maana ya wewe kuumbwa ni pale utakapoanza kutembea katika ndoto, utafanya Mungu ajivunie kwa kukuruhusu uje duniani.

Mungu afanyi jambo kwa hasara au kwa kumkomoa mtu bali ufanya yote ili kuhakikisha ufalme wake unaimarika.

Mungu anataka uwe faida kwa wengine kwa wewe kujizatiti katika kuishi ndani ya ndoto yako!
Nafuu usingezaliwa kuliko ukazaliwa alafu ukaishi nje ya ndoto yako inakuwa sawasawa na mtu ( mwanafunzi ) aliyefanya mtihani akaona kuwa ulikuwa rahisi baadae akagundua amefanya kinyume na swali linavyotaka/hitajika kwa kifupi ameenda O.P (Out of Point) na matokeo yake yaka gharimu maisha yake.

Unaweza kuwa na kila kitu ambacho binadam anapaswa kuwa nacho lakini ukiwa nje ya ndoto yako hivyo vitu hautaona radha ya maisha iliyokamili kuwa navyo japo unaweza kucheka, kufurahi na kujirizisha nafsi yako kwa maneno au kwa kufanya vitu vingi lakini kamwe haitasaidia.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………0764 018535

Ijumaa, 30 Agosti 2019

MBINGU INAJIWEZA!




ACHA UTENDAJI WA MBINGU UFANYE YAKE

Kuna mambo yanapotokea hisia, akili na mwili wote unahisi umesimama na haujui unatokaje!
Unaweza kukuta unaamini upotofu zaidi kuliko usalama maana uhakika wa njia sahihi hauna/ hauioni!

Na wakati mwingine hata mwenyehaki anapojikuta yuko hatiani uweza kufanya jambo lolote ili mradi maisha yake yawe salama pasipo kuzingatia usawa wa jambo husika.

Karibu sana!

Abramu alipokuwa na sarai  alipotaka kupita nchi ya ugenini alimwambia sarai mkewe aseme kuwa ni ndugu yake na sio mke wake…………!

Mwanzo 12:10 Basi kulikuwa njaa katika nchi ile; Abramu akashuka Misri, akae huko kwa muda maana njaa ilikuwa nzito katika nchi.
                      11 Ikawa alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, Tazama, najua ya kuwa u mwanamke mzuri wa uso;
                      12 basi itakuwa, Wamisri watakapokuona watasema, Huyu ni mkewe; kisha wataniua mimi na wewe watakuacha hai.
                      13 Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako.

Isaka alipokuwa akitembea , akamwambia Rebecca aseme kuwa ni ndugu yake na wala si mke wake!
Mwanzo 26:6 Isaka akakaa katika Gerari.
                     7 Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe. Akasema, Ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema, Ni mke wangu, watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso.
                    8 Ikawa alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, akachungulia dirishani, akamwona Isaka anacheza-cheza na Rebeka mkewe.
                   9 Abimeleki akamwita Isaka, akasema, Yakini huyu ni mkeo, mbona ulisema, Ni ndugu yangu huyu? Isaka akamwambia, Kwa sababu nalisema, Nisife kwa ajili yake.
                  10 Abimeleki akasema, Ni nini hii uliyotutendea? Labda mtu mmojawapo angalilala na mkeo bila kufikiri, nawe ungalitutia hatiani.
                  11 Basi Abimeleki akawaamuru watu wote, akisema, Amgusaye mtu huyu au mkewe lazima atauawa.
Wote ( Abraham & Isaka) walikuwa wanaogopa kufa kwakuwa wake zao walikuwa wazuri sura na muonekano!

Kuna mambo yanatokea na kupata ufumbuzi kwasababu ni asili ya dunia ilivyoumbwa kwa namna yake na Mungu sawa na mapenzi yake mathalani mtu aliyeonewa kwa muda mwingi na kunyanyaswa na mwisho akapata haki yake hata bila ya kutoa rushwa mwisho atasema “ MUNGU MKUBWA”!

Hakuna kitu bora au kizuri sana kama mahali ambapo mbingu imeamua kusema ni wazi ardhi lazima itikie maana sauti ya mbingu ardhi uielewa vizuri sana.

Ni muhimu kutambua ili mbingu iweze kukutetea lazima wewe uwe ndani ya mbingu ili yenyewe ijidhihirishe.

Kuna wakati unaweza kuona ni nafasi ya akili ya kutumika maana umemngoja Bwana kwa muda mrefu bila mafanikio/majibu na hali inazidi kuwa mbaya!

Mambo yanatokeaga na yakaathiri furaha ya maisha yako na hasa ukajua haukuhusika kabisa katika kosa hilo, mtu wa namna hii anakuwa na msongo wa mawazo “ stress” akiangalia kile kinachomkabili na uhalisia uliopo lakini ujue inawezekana katika mwili hauja husika lakini katika ulimwengu wa roho una husika ili uweze kutoka hatua moja na kwenda hatua nyingine na hatimaye kung’aa zaidi.

Kuna urahisi mkubwa pindi mambo yako pale mbingu itakavyoanza kuhusika na jambo linalokuhusu wewe.

Kitu pekee kinachoweza ruhusu mbingu kutenda kazi kwa urahisi/wepesi ni pale akili yako itakubaliana na sauti ya mbingu ( Roho mtakatifu).

Ili mbingu iweze kuingilia teso lako ni muhimu mbingu iwe ndani yako nawe uwe ndani ya mbingu ili ikupe urahisi wa kutambua hii ni sauti ya mbingu na hii sio sauti ya mbingu.

Unapoishi maisha ya mbingu kicheko kinakuwa maisha yako uwa haucheki/ufurahi kwakuwa kitatokea au kikitokea bali kikianza ndani ya moyo wako basi unajua kimeshatokea.

Wakati mwingine unaona kama hauna maisha yako binafsi lakini muhimu sio kuishi tu bali usalama wa maisha katika mikono ya Mungu.

Warumi 8:14………
“Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu”.
Ni muhimu na ni bora usiende na mtu yeyote lakini hakikisha umeenda na mbingu hapo utafika salama.

Kutoka 33:14……….
“Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha”.

INAITWA SIKU! BARIKIWA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………….0764 018535