Kuishi ni
neema ambayo Mungu ametoa kwa kila kiumbe kilichokua hai.
Ninapozungumzia
NDOTO! Katika muktaza huu Uwa sina maana mawazo yako ya siku nzima yanayojifunua
usiku wakati umelala, bali ninazungumzia matarijio kamili ya Mungu katika kukufikisha
kilele cha ustawi wako katika jambo Mungu ameliweka ndani yako.
Ni muhimu
utambue kuwa kuna kuishi maadam unapumua, Napia kuna kuishi kwa maana ya kuitumikia ndoto yako.
Hakuna
maisha ya furaha kama ukiishi ndani ya ndoto yako, ni maisha yenye raha ni
zaidi ya majigambo ya samaki akiwa majini.
Kama
binadamu unaweza kutamani ndoto za wengine lakini kamwe usikubali kuishi humo
kwani uwezekano mkubwa na kuangamia hapo upo! bali jifunze katika mema yenye
mchango katika ndoto yako.
Unapoamua
kuishi ndani ya ndoto yako hapo hakuna kushindana, manung’uniko wala majuto
bali siku zote utaona deni la kufanya tu pasipo kuchoka.
Kuna maisha
unayoweza kuishi ikapelekea ndoto yako kufa au kushamiri katika mwenendo wako
wa maisha kila siku.
Moja ya kuwa
faida katika dunia ni kuishi katika ndoto yako maana kwa kufanya hivyo
itapelekea maana ya wewe kuishi duniani na utakuwa msaada kwa wengi.
Hauhitaji
kuishi katika ndoto za wengine,kwani hali hiyo itapelekea kukosa mwelekeo
unaweza kujikuta unafanya kitu ambacho akikuzaliwa ndani yako.
Moja ya
sababu watu kuishi maisha ya mateso ni kuishi nje ya ndoto zao.
Ni muhimu
utambue sio kila kitu unapaswa ufanye, bali ni kile kilichozaliwa ndani yako
chenye tija katika ndoto yako na sio kuleta majeraha katika maisha ya wengine.
Mtu
anayeishi katika ndoto yake uwa ajui nini maana ya kuchelewa katika hatma ya
ndoto yako.
Usiruhusu
jambo lolote hata liwe zuri kwa namna gani endapo utagundua litakutoa nje ya
ndoto yako usifanye hata iki kugharimu kiasi gani au hasara ya muda fulani?
Unahitaji
kujua kwamba maana ya wewe kuumbwa ni pale utakapoanza kutembea katika ndoto,
utafanya Mungu ajivunie kwa kukuruhusu uje duniani.
Mungu afanyi
jambo kwa hasara au kwa kumkomoa mtu bali ufanya yote ili kuhakikisha ufalme
wake unaimarika.
Mungu
anataka uwe faida kwa wengine kwa wewe kujizatiti katika kuishi ndani ya ndoto
yako!
Nafuu
usingezaliwa kuliko ukazaliwa alafu ukaishi nje ya ndoto yako inakuwa sawasawa
na mtu ( mwanafunzi ) aliyefanya mtihani akaona kuwa ulikuwa rahisi baadae
akagundua amefanya kinyume na swali linavyotaka/hitajika kwa kifupi ameenda O.P
(Out of Point) na matokeo yake yaka gharimu maisha yake.
Unaweza kuwa
na kila kitu ambacho binadam anapaswa kuwa nacho lakini ukiwa nje ya ndoto yako
hivyo vitu hautaona radha ya maisha iliyokamili kuwa navyo japo unaweza
kucheka, kufurahi na kujirizisha nafsi yako kwa maneno au kwa kufanya vitu
vingi lakini kamwe haitasaidia.
INAITWA
SIKU! BARIKIWA
Imeandaliwa
na:
Cothey Nelson………………………………………………0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni