Ijumaa, 23 Oktoba 2020

SWALI LINAKOSA MAANA!

 



 

Kama binadamu uliopata neema kuingia katika mifumo mbalimbali ya elimu na kufanya mitihani, utakuwa ulishakutana na maswali katika mitihani yaliyokosewa au yasiyo na majibu!

Wakati mwingine swali lililokosewa uweza kurekebishwa ili liwe na MAANA au kubadilishwa na pengine kutoa alama za bure (free masks) ikiwa hilo swali alikujulikana mapema wakati wa mtihani ila baada ya kusahihishwa mtihani likagundulika.

Karibu!!!

Maswali yamekuwa ni rafiki wa akili na hasa katika kupasha joto ubongo, na upelekea hali nzuri kwa akili kupanuka na kupata uelewa mwingine.

Na wakati mwingine mtu anapokosa jibu hali hiyo uweza kuingia ndani ya moyo na kuleta usumbufu, usumbufu wa mtu kuwa na maswali mengi kwa kile kinacho mkabili pasipo kujua niende kushoto au kulia, hali ya swali kuwa na jibu zaidi ya moja na hatimaye kushindwa kupata jibu linalojitosheleza na hata kujikuta uko njia panda.

Pindi inapotokea mtu anapokuwa na maswali mengi kichwani mwake kwa kiasi kikubwa inategemea hulka ya mtu husika wako watu wanapokuwa katika hali hii upenda kucheza mziki, au kupiga makelele,kuongea sana, kukaa kimya na mwingine upenda kulala hama kulewa na mambo mengine yafananayo na hayo lakini bado unaweza kukosa jibu sahihi au lililojitosheleza katika swali husika.

SWALI LINAKOSA MAANA PALE UNAPOPATA JIBU!

Kama samaki anapo poteza makeke yake au usumbufu wake ni pale utakapo fanikiwa kumtoa nje ya maji na kumweka nchi kavu………………………………………………..!

Ndivyo ilivyo pindi utakapopata majibu katika maswali yanayo kukabili hapo akili uweza kutulia na hali ya ushwari uweza kuingia ndani ya moyo wako.

Ndomana waswahili usema “ atafutae achoki na akichoka amepata” hivyo utashangaa pindi mtu atakapo choka wakati ajapata japo yote yanawezekana kutegemea na hali ya ndani ya mtu husika .

Na wakati mwingine unaweza pata majibu lakini sio utatuzi wa leo wala kesho bali utakuweka katika hali njema ya matarajio ya uhakika wa kweli katika majira yajayo.

Usiruhusu maswali yawe maisha yako maana yatautesa ufahamu wako! Bali tambua kwa kila jambo/swali linalokuja katika maisha yako uwa tatizo linaisha ni mpaka ujue majibu ya maswali hayo yanapatikana wapi? Maana ukikosa kujua sehemu husika hauwezi pata majibu ya uhakika.

“ hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea”

 

1 Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Endapo ikatokea ukakosa majibu ya maswali yako kwa wanadamu ( watu unao waamini) usihofu wewe fungua hazina ya mbingu hiyo uwa haikosi majibu maadam mbingu hipo basi mwenye mbingu yupo na majibu yapo.

Haya ni majibu yanayoleta amani ya kudumu, maana hicho ndicho chanzo sahihi cha majibu ya maswali yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………0764 018535

Jumanne, 6 Oktoba 2020

SEHEMU SALAMA!

 



 

Sehemu salama ni hitaji la kila binadamu mwenye kujielewa na kujithamini, ni kama fedha isivyokuwa na adui bali kila mmoja uhitaji kwa matumizi yake binafsi sawa na halmashauri ya ulimwengu wa fikra zake.

Wakati mwingine ni ngumu kutambua hapa ni sehemu salama au si salama kwa muonekano tu, kwani kuna mahali panaweza kuonekana kuwa ni sehemu salama kwa macho lakini usalama unaonekana hapo kinaweza kuwa ni kichaka cha kuficha uharibifu.

Ni kweli kuna sehemu panawezeka kuonekana kuwa hapo usalama ulizaliwa hapo kutoka na ulinzi mkali na mitambo ya kutosha iliyopo! Lakini uharibu wa siku moja unaweza ukaharibu hiyo sifa ya sehemu hiyo.

Usalama mbali na sehemu/eneo husika pia unaweza kuhuamishia kwa mtu,ukafikiri ninapokaa au kuongea naye siri zako basi maisha yangu yatakuwa salama hali hiyo inaweza kuwa kwa kitambo tu baadae anaweza asiwe salama kwako bali akatumia nafasi hiyo kukuharibu kabisa.

Katika hali ya dunia inavyoaminika na kusema sehemu hii ni salamu au mtu huyu ni salama hali hii inazidi kupungua kutokana na matokeo yasiyotegemea kutokea na kuzidi kuushangaza ulimwenguni,yale ambayo ukutegemea kutokea sasa yanatokea na kuwa ni mambo ya kawaida.

Mathalani wapo waliweka imani kubwa kwa wazazi wao wakitegemea kwao hapo ni sehemu salama lakini mwisho wakatolewa kafara.

Sasa sehemu salama utaipata wapi? Utaijuaje? Ili uweze kuwa salama isiyokuwa na maswali yoyote!

Ili upate usalama wa kudumu na wa uhakika ni lazima urudi kwa yeye aliye asili ya vyote vinavyoonekana na visivyoonekana “ SIR GOD “

Mbali na usalama huu hakuna mahali pengine penye usalama wa kudumu, kwa maana usalama mwingine utengenezwa na akili za wanadamu au mazingira yanayokushawishi kusema sehemu hii ni salama lakini hali hizo zinaweza kubadilika na kuleta maafa.

Ninao ushuhuda wa mtu aliyefikiri kuwa sehemu hii ni salama kwake au kwa mtu ukafikiri kuna usalama kwake lakini baadae akakengeuka kabisa na kusababisha majeraha makubwa ndani ya moyo wa mtu lakini sijawai kuona kwa mtu aliyemfanya Mungu kuwa ni sehemu salama kwake alafu Mungu akawa si sehemu salama kwake.

Ukimfanya Mungu kuwa ni salama kwako naye atakuletea salama yake katika kila jambo na kamwe hawezi kukudhuru kwa kuwa teso la moyo wako ndio teso lake.

“ Nitakuwa pamoja nawe taabuni”

Mfanye Mungu kuwa salama yako hauwezi juta, atakufanya uyafurahie maisha yako kwa maana ni yeye alikutambua kabla ujatokea duniani na kizuri zaidi anampango mwema juu yako.

Hautaji kuchoka katika usalama wako na Mungu bali wewe kubali kufuata maelekezo yake naye atakupa usalama wake na kuzidi katika maisha yako.

“ msikilize uwe salama ndani yake “

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………0764 018535

 jibu

Jumamosi, 12 Septemba 2020

NENO LAKE NDIO UTOSHELEVU WAKO!




Yohana 21:1…….
1 Baada ya hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi wake, penye bahari ya Tiberia, naye alijidhihirisha hivi.
 2 Simoni Petro, na Tomaso aitwaye Pacha, na Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, na wana wa Zebedayo, na wengine wawili wa wanafunzi wake, walikuwapo pamoja.
 3 Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.
 4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.
 5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.
 6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.

Masumbuko ya wanafunzi wa yesu yalitatuliwa baada ya kufuata neno lililotoka katika kinywa cha yesu “ litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata”

Moja ya sababu za harakati za wengi hasa katika dunia tuliyopo ni hali ya kutafuta utoshelevu ( hali ya juu katika kukizi mahitaji binafsi ).

Kuna aina mbili ya utoshelevu katika dunia ( ulimwengu );
i.                    Utoshelevu wa nafsi
ii.                  Utoshelevu wa mali
Unaweza kuwa na kila kitu lakini bado nafsi ikajisikia bado ina uhitaji mkubwa, unaweza kuoneka kwa macho au wakufukirika tu lakini uhalisi unabaki kwako.

Unaweza kukuta mtu atulii kuanzia mwili hata akili, na hali hii uweza kumtokea katika harakati za kuhitaji kukizi uhitaji alionao ili utoshelevu uweze kudhihirika katika maisha yake.

Wako watu wanaacha kazi, huduma au shughuli binafsi baada ya kuona kitu anachokifanya akimletei utoshelevu anaoutaka, na hata wakati mwingine hata kule alikoamia kunaweza bado pasimpatie utoshelevu anaoutaka/alioukusudia akabaki kung’ang’ana tu.

Moja ya jambo au kitu kinachoweza kuwafanya watu kushindwa kufikia katika utoshelevu wa jambo lililokusudiwa ni mtazamo usio sahihi wa jambo husika ( matarajio ya kufikirika yasio na uhalisia ).
Wakati mwingine unaweza kukuta unaacha kitu sahihi ulichotakiwa kukifanya kilicho sahihi kabisa na ukaenda kufanya kufanya kitu kingine kabisa ambacho ukutegemewa kufanya lakini ukaona neema za Mungu zikizidi kukuzingira na kukupa mkate wa kila siku hali hiyo haina maana kuwa Mungu anafurahia.

Yohana 21:15…………..
Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda.  Akamwambia,  Lisha wana-kondoo wangu.

Baada ya yesu kuhakikisha simon petro ameshakula ndipo akamuuliza swali “ je! Simon wa yohana, wewe wanipenda…………………. Akamwambia chunga kondoo zangu” ( maana petro baada ya kupewa samaki na kula ndipo yesu akamkumbusha jukumu lake la msingi la kukaa na kuendelea kumsubiri bwana hata ujio wa Roho mtakatifu utakapofika au kuajilia.

-          Ndomana yesu anajaribu kumsisitizia asisahau kuishi kwenye kusudi lake hata kama hali ikiwa ngumu kiasi gani? Atulie hapo maana yeye aliyekupa neema ya kuwa hapo atakupa utoshelevu wake.

Uhitaji wowote ulio katika mwili ( uhitaji wa nafsi ) uwa hauna kikomo na ukisumbukia hauwezi kudumu katika lengo kuu uliokusudiwa na hivyo kupelekea kushindwa kupata utoshelevu usioisha.

Ni muhimu utambue utoshelevu uliobebwa na neno lililo katika kinywa cha yesu, anachosema ndicho kinachobeba utoshelevu kinachoshikiliwa na yeye mwenyewe.

Penda kuishi sawa na neno linalotoka katika kinywa cha yesu mwenyewe na sio sawa na wimbi la dunia linavyokwenda, kwakua linavyokwenda linakwenda  na kishindo cha kukutisha hama kukufanya uweze kupata wasiwasi juu ya mstakabali wa maisha yako husika.

Wewe ni asili ya NENO unapolikubali linaenda kutibua na kuanzisha utoshelevu wake na sio wa kufikirika katika akili?

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………… 0764 018535

Ijumaa, 14 Agosti 2020

NAMNA YAKE!

 


“ Namna yake”  ni hali inayoonyesha vile alivyo au namna anavyoendesha mambo yake!

Na imekuwa ni msemo wa kawaida katika ulimwengu wa sasa katika mambo mengi;

i)                    Ili upate kile kitu basi wewe enenda kwa namna hii alafu muda si mrefu itakuwa ya kwako.

ii)                  Ukitaka “ kuwin ili game” ni lazima uende kwa namna hii nje ya hapo “ utafail- utashindwa”

iii)                Ukitaka kumpata huyu binti au kijana wewe fanya hivi tu alafu atakuwa wa kwako.

iv)                Ukitaka kuipata ile “tenda” wewe fanya hivi au andika “ proposal” iliyo ya namna hii basi utaipa.

Mwisho wa siku tunatambua kila jambo lina namna yake ili uweze kulipata/kufanikiwa sio kwenda vyovyote tu ukutegemea kupata kila kitu.

Ni kweli unaweza kukosa vingi kwasababu ujui jinsi/namna yake ili uvipate hama unaweza kujikuta unakosea kila siku kwasababu ujui jinsi/namna ya kukifanya kiufasaha.

Hii hali ya namna ya kufanya kitu imeleta shida sana katika jamii tuliyonayo; mathalani unaweza kukuta kila mtu ana namna yake ambayo yeye binafsi anataka asalimiwe au atendewe, utoshangaa kusikia watu wakisema huyu mtu ili aitike salamu yako amekutathmini kwanza kwa muda wa kutosha mbali na hilo, pia katika salamu wako watu wanapenda uwakumbatie pindi unapowasalimia hapo ndipo wataona umewasalimia na kuna wengine ukiwapungia mkono kama ishara ya kuwasalimia wanaona sawa tu hawana shida bali wengine wanaweza ona kuwa umewadharau…….mbali hayo pia yako mambo mengine namna tofauti tofauti ya kuongea na watu kutokana na hadhi ( status ) yao, rika lao pia kwa namna mbalimbali hata katika upande wa mapishi inaweza kuwa wote mnapika mchele lakini namna ya kupika mkatofautiana kutokana na sababu mbalimbali inaweza kuwa kutokana na ushauri wa daktari kuna vitu vitaongezwa au kupunguzwa kwa mgonjwa, hama kutokana na mapenzi ya mtu husika anapenda apike kwa namna ipi?

Kuna namna ya vitu/mtu kuvifanya vilivyo asili kwakuwa ni lazima vipitie katika hali hiyo ili viweze kuwa katika hali yake ( vitu vilivyo asili vinaenenda kwa asili ) lakini kwa jambo ambalo si sawa katika mwenendo au baadhi ya watu unaweza kukuta mtu amejiwekea namna yake katika kuendesha mambo yake utafikiri hiyo  namna walikaa na Mungu wakakubaliana, ila hiyo ni namna ya ubinafsi iliyo tawaliwa na matakwa ya mtu husika lakini watu wa namna hii upenda kutembea kwa namna hiyo akiitafsiri kuwa hiyo ndio namna yake.

Bila shaka unaweza kukuta namna hiyo inabadilika ghafla pindi moyo utakapo pata mwelekeo mwingine pia kuishi kwa namna yako ni kitu kizuri lakini kuwa mwangalifu isije ikawa kero kwa watu wengine.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………….0764 018535