Katika hali ya kawaida uwa mtu atulii tu! pasipo sababu inayomfanya atulie, inawezekana kuwa ni sababu iliyoanzia ndani yake iliyojaa na ubinafsi wake au yaliyosabishwa na mambo yaliyo nje yake.
Utulivu unaendana sana na subira au moyo wa kungojea kitu kwa matumaini makubwa!
“ kimya kina kishindo”
Na kuna utulivu kwa maana ya kupata pumziko la akili, ili ikusaidie kurudi katika ubora wa utendaji wako! Pia kuna utulivu wa lengo la kujiandaa na jambo na hatima kuushangaza ulimwengu yaani unafanya jambo au tukio ambalo masikio yakisikia yatawashwa na hata macho hayata amini kile kinachoonekana.
Mathalani, shambulio la magaidi dhidi ya marekani ( September eleven ) ni shambulio lililoweza kubomoa balozi za marekani zilizopo Kenya na Tanzania kwa wakati mmoja, hii mikakati ya shambulio hili lilikuwa la siri sana na kuchukua muda mrefu katika maandalizi yake hata kama mchunguzi wa mambo haya ungeweza kusema shambulio alipo au wameaghirisha.
Uwa ardhi inapoachwa kwa muda baada ya kupoteza rutuba yake au kuachwa kwa muda kwa sababu zingine lakini pindi muda utakapofika shughuli zinaweza kuanza tena au kuendelea kwa kishindo kisichokuwa cha kawaida au kupatikana kwa mavuno yakutosha japo wakati mwingine unapoona ardhi imeachwa unaweza kuhisi kuwa imetelekezwa lakini sivyo!
Unaweza kukuta mtu yuko kimya kama hayupo vile katika shughuli fulani isifanye ukafikiri kuwa ameshindwa, kumbe anatunza fedha au anarejesha nguvu zake ili aweze kufanya jambo kwa kishindo kingine cha ajabu.
Kwahiyo unapokaa na mtu usitishwe au usipotezee utulivu wake, endapo kama hautajua yapi yanaendelea katika utulivu wake maana kwa kujua hapo panaweza kufanya ujiamini au ukimbie.
“ ukiona kobe kainama ujue anatunga sheria “
Hivyo utulivu au ukimya wa mtu sio ukupe matumaini kwamba ameshindwa, kwani unaweza kujikuta uko katika mazingira magumu kwa kutokujua kinachoendelea katika utulivu wake.
Utulivu wenye kishindo haya ni maisha mazuri sana yanayokupa nafasi ambayo wengine awawezi kudhani kuwa utatokea hapo au kuwa mshindi.
“ yesu alipokuwa anaelekea kwenye kifo, kambi ya adui ilishangilia sana na kuamini imeshinda ule ukimya na upole wake pamoja na unyenyekevu wake alishajua ameshamaliza kila kitu, lakini awakutambua maana ya neno la yesu alilolisema “ imekwisha “ ila walielewa baada ya yesu kuingia katika himaya yake ya utawala wa giza hapo alishindwa kuamini kilichomtokea.
Ingawa mambo mengi yanapokuzonga hapo unaweza kuwaza mengi na maamuzi mengi yanaweza kuja katika akili zako lakini ukiingia katika ulimwengu wa utulivu na Roho mtakatifu hapo unakuwa hatari zaidi ya hatari yenyewe.
Usipende watu wakuelewe mapema subiri matokeo yatawaelewesha vizuri kuwa wewe ni nani?
INAITWA SIKU! BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson…………………………………………………………………………….0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni